KWELI Mwanamke anaweza kubeba Ujauzito wa watoto mapacha wenye baba tofauti

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana.

Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti.

black-pregnant-woman-getting-doctor-checkup_3x2 (1).jpg

Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
 
Tunachokijua
Ujauzito hutokea baada ya kuungana kwa mbegu ya kiume na yai la mwanamke, tendo ambalo kitaalam huitwa urutubishaji (Fertilization). Tendo hili hutokea kwenye siku maalum katika mzunguko wa hedhi ya mwanamke.

Baada ya kutokea kwa urutubishaji huu, yai pamoja na mwili wa mwanamke kwa ujumla hutengeneza mfumo imara usioruhusu kutokea kwa urubishwaji wa mara ya pili kwenye yai moja. Ni mwanzo wa takriban siku 280 za kulea ujauzito mpya hadi pindi ambapo muda wa kujifungua utafika.

Katika hali ya kawaida, ujauzito wa mwanamke huhusisha baba mmoja wa mtoto. Hii inatokana na ukweli kuwa wanawake wengi hutoa yai moja lililopevuka katika kila mzunguko mmoja wa hedhi.

Ujauzito wa watoto wawili wenye baba tofauti
Kwa mujibu wa Taasisi ya Afya ya Marekani (NHI), baadhi ya wanawake hutoa yai lililopevuka zaidi ya moja kwenye mzunguko mmoja wa hedhi.

Ikiwa mwanamke atashiriki tendo la ndoa na mwanaume mmoja kisha wakafanikiwa kufanya urutubishaji, baadae mwanamke huyo akashiriki tena tendo la ndoa na mwanaume mwingine baada ya kutolewa kwa yai lingine ndani ya mzunguko huo mmoja, urutubishaji mwingine wa mara ya pili unaweza kutokea.

Tendo hili huitwa Heteropaternal superfecundation, humaanisha kuwa mwanamke amepata ujauzito wa watoto wawili (mapacha), kwenye mzunguko mmoja wa hedhi uliohusisha mayai mawili, ambao baba zao ni tofauti.

Utafiti wenye kichwa cha habari "How frequent is heteropaternal superfecundation?" wa Wenk RE et al, unabainisha kuwa visa hivi huwa havitokei kwa namba kubwa. Mathalani, katika utafiti wao uliohusisha wazazi 39,000 wenye watoto mapacha wasiofanana, ni 2.4% ndio waligundulika kuwa na baba tofauti.

Hivyo, kwa kuzingatia rejea hizi muhimu, pamoja na mazungumzo tuliyofanya na madaktari bingwa wa Masuala ya uzazi, JamiiForums inakubaliana na hoja kuwa hali hii ipo, na inaweza kutokea kwa wanawake wachache sana.
mapacha wasiofanana na wanaofanana sababu Yao ni nn
Mapacha wasiofanana wanatokana na mayai mawili au zaidi kurutubishwa

Mapacha wanaofanana wanatokana na yai moja kumeguka na kuwa mawili au zaidi.... hawa hata DNA zao zinakuwa nearly identitical
 
mapacha wasiofanana na wanaofanana sababu Yao ni nn
Mapaca wanaofanana wametokana na yai moja nililorutubishwa na mbegu moja,katika uundaji wa mbegu za uzazi kuna hatua mbili zinahusishwa ambazo ni Mitosis na Meiosis,Meiosis imegawanyika katika hatua mbili ambazo ni Meiosis I na Meiosis II,sasa kwa mwanamke meiosis I hukmilika prior wakati wa fertilization,na ndio katika hatua hiyo yai moja lina undergo nucleus cleavage na kutengeneza double zygote na hatimaye tunapata watoto wenye sifa zinazofanana.

kwa wasio fanana hutokea pale ovari zote 2 kuzalisha mayai katika mwezi mmoja(ynaweza kuzalshw kwa pamoja ama kwa nyakati tofuti ila yatapishana kwa muda mfupi sana n mayai yote yatarutubishwa ila kwa mbegu tofauti.

kwa kesi ya mapacha wa 4 inaweza kuwa ni chnzo cha yai 1 ama 2,na 8 mara nyingi nii mayai 2 ambayo kiila moja hugawanyika mara 4.

mwanamke ndio anahusika zaidi katika matokeo ya watoto mapacha na sio mwanaume.
 
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana.

Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti.


Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
swali ni sawa kuamini kila mapacha wasio fanana wanaingia kundi hilo la mapacha wenye baba tofauti?
 
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana.

Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti.


Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
Binadamu siyo paka ndugu.
 
Nyie acheni Mungu aitwe Mungu, Mungu fundi sana.

Kuna shuhuda mbalimbali zinaelezwa kuwa kuna wanawake waliweza kupata ujauzito wa pili huku wakiwa tayari wana ujauzito. Yaani leo mwanamke anapata ujauzito, na siku 15 mbeleni anadaka ujauzito wa pili.

Naamini hii hutokea kwa nadra sana na kila mtoto wakati wa ujauzito huu wa pili, watakuwa na viwango tofauti vya makuzi yao tumboni, watakuwa na damu tofauti, na inaelezwa wanaweza kutofautiana kabisa vitu vingi.

Mimi si mtaalam wa masuala ya uzazi, ngoja niwasikilize wadau kwamba hii inaweza vipi kutokea!
 
Nyie acheni Mungu aitwe Mungu, Mungu fundi sana.

Kuna shuhuda mbalimbali zinaelezwa kuwa kuna wanawake waliweza kupata ujauzito wa pili huku wakiwa tayari wana ujauzito. Yaani leo mwanamke anapata ujauzito, na siku 15 mbeleni anadaka ujauzito wa pili.

Naamini hii hutokea kwa nadra sana na kila mtoto wakati wa ujauzito huu wa pili, watakuwa na viwango tofauti vya makuzi yao tumboni, watakuwa na damu tofauti, na inaelezwa wanaweza kutofautiana kabisa vitu vingi.

Mimi si mtaalam wa masuala ya uzazi, ngoja niwasikilize wadau kwamba hii inaweza vipi kutokea!
HII INAWEZEKANA MUDA HUO NI MFUPI SANA,MARA NYINGI MULTIPLE OVULATION HUWA ZINAPISHANA MUDA KIASI ,SIKU AMA MASAA ILA SIKU NDIO SANA.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom