Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,886
- 6,883
Eneo moja wapo ambalo vigumu kwa wanawake wengi
kupata ukombozi kamili
Mwanamke anapojiruhusu kudhalilishwa na kujidhalilisha ni pale anapoamua kuwa chombo cha kutumiwa kwa malipo mojawapi ikiwa ni kufanya ngono kwa kubadilishana na pesa au vitu, na mtu uamuapo kutumika kwa malipo pasipo ridhaa ya moyo wa kuridhiana dhana kamili na halisi ya mapenzi yenye kuwaburudisha wote ni kujigeuza bidhaa. Hata wawili mnaporidhiana kimapenzi na kupendana lakini mmoja kuhitaji ziada ya raha wanazopata wote pamoja akirimiwe malipo kwa kustarehe wote ni dhana ya kutumia maungo ya mwili wake kwa minajili ya kufanya ngono kwa malengo ya kibiashara. kupata ukombozi kamili
Bila malipo hayuko radhi kufanya ngono hata kama wamependana, hivyo dhana ya mapenzi kwa msichana wa aina hiyo ni biashara ya mapenzi /ngono aina ambayo kwa tafsiri nyepesi ni uasherati. Uasherati ni msamiati usioleta maana nzuri katika jamii lakini ni wengi tu wanaofanya uasherati kwa maana lete pesa tufanye ngono maana hakuna mwasherati anayeweza kufanya ngono bila malipo kwa vile ameshajiruhusu kuwa ni bidhaa ya kunadi mwili wake kwa ngono ili alipwe. Hali kadhalika mwenye kutumia chambo cha pesa kama njia ya kukodi mwili wa mwezie kufanya mapenzi ni uasherati pia. Hawa wanaokodi mtu kwa minajili ya kutumia maungo yao kwa kujiridhisha kingono ndio wanaofanya wenye kufanya biashara hii iimarike.
Mwanaume mwenye kuridhia mahusiana na mfanya biashara huyo wa kukodisha maungo yake kwa ngono pengine huishia kufanya hata yasiyotegemewa ili mradi pesa yake itumike kwa namna anavyoona imemtosheleza hata kama ni kuharibu afya yake.
Kwa wenye upendo wa kweli wanajisikia haki sawa na kusaidiana iwe mdada au mkaka vyo vyote wanahitaji kwa pamoja kuwekana sawa iwe kimapenzi hali kadhalika kiuchumi. Mdada yuko tayari kumsaidia mkaka katika hali na mali na mkaka hali kadhalika. Ipo siku mdada anam-take out mkaka na siku nyingine mkaka anam-take out mdada, hao ndio wanajua maana ya mapenzi ya kweli na uwajibikaji wa kila mmoja kwa mwenzake.
Ukishaona mdada anatanguliza dalili za deal ya mapenzi kibiashara ujue moja tu maisha yote hata mkioana utabaki kununua huba kwa sababu utaratibu wake kufanya mapenzi ni kukodisha mwili wake kwa malipo, na pengine ukawa na ziada peke yako financial kwa familia na yeye asijisikie kama ni sehemu ya jukumu lake.
- Nini maana ya bf/gf au mume na mke?
- Inajenga dhaba gani katika mapenzi ya kweli kuwa kukodishana kwa malipo?
- Kwa nini wasichana wakiwa na shida ya kutimiziwa hamu ya ngono hawawakodi wanaume kwa malipo?
Kati ya wawili wanaojamihiana nani anayenufaika au kufurahia? Wote pamoja wanajisikia raha na kufarijika na kujisikia faraja toka kwa mwenzie. Iweje wakati wote mmeonja raha sawa halafu mwingine akamuliwe? Hii ndiyo hali ya mwanamke kujiruhusu kuwa chombo cha kutumiwa kibiashara kwa kukodisha mwili wake kwa muda utumiwe na mwanaume kuwa source ya mapato ya mwanamke kwa njia ya zinaa/ngono. Nakumbuka kuli ya mzee ruksa alipowaasa watanzania: "tuache ngono jamani, ukimwi utatumaliza, nawasihi tuache ngono jamani."
Kuna dalili wazi nyingine mojawapo ya msichana kuomba hili mara lile hata kama hamjafahamiana kutosha, maana yake amejitosheleza kwa kila anachohitaji hata kuhusu mwenza anaye, ila ni njia tu ya kukukatalia. Mwanaume kuendelea kubembeleza basi dau linapanda na kujikuta mwanaume laini na mwepesi kujiruhusu nusu ya mshara wake amalizie kwa starehe ya mahaba ya dakika chache. Pengine wengine licha ya kuwa na mwenza hugeuza nje ya mwenza kuwa kitegea uchumi, rejea paragraph ya kwanza niliyosema kujidhalilisha na kujiruhusu kudhalilika kwa kutumia maungo ya mwili wake kukodisha kama chambo cha kuwatega wanaume wammuminie michuzi ya kuishia.
:cheer2::cheer2::cheer2:
Ukombozi wa wanawake walio wengi bado
Inamfikisha mfanya biashara kulegeza ugo kwa wateja kadhaa,
au Mwanaume kupitia bidhaa kadhaa
kwa sababu tu kukubali uteja, au kujiruhusu kuwa bidhaa.
:cheer2::cheer2::cheer2: