Mwanamke anapojidhalilisha kwa kujifanya bidhaa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,886
6,883
images
images
images
images
Eneo moja wapo ambalo vigumu kwa wanawake wengi
kupata ukombozi kamili
Mwanamke anapojiruhusu kudhalilishwa na kujidhalilisha ni pale anapoamua kuwa chombo cha kutumiwa kwa malipo mojawapi ikiwa ni kufanya ngono kwa kubadilishana na pesa au vitu, na mtu uamuapo kutumika kwa malipo pasipo ridhaa ya moyo wa kuridhiana dhana kamili na halisi ya mapenzi yenye kuwaburudisha wote ni kujigeuza bidhaa. Hata wawili mnaporidhiana kimapenzi na kupendana lakini mmoja kuhitaji ziada ya raha wanazopata wote pamoja akirimiwe malipo kwa kustarehe wote ni dhana ya kutumia maungo ya mwili wake kwa minajili ya kufanya ngono kwa malengo ya kibiashara.

Bila malipo hayuko radhi kufanya ngono hata kama wamependana, hivyo dhana ya mapenzi kwa msichana wa aina hiyo ni biashara ya mapenzi /ngono aina ambayo kwa tafsiri nyepesi ni uasherati. Uasherati ni msamiati usioleta maana nzuri katika jamii lakini ni wengi tu wanaofanya uasherati kwa maana lete pesa tufanye ngono maana hakuna mwasherati anayeweza kufanya ngono bila malipo kwa vile ameshajiruhusu kuwa ni bidhaa ya kunadi mwili wake kwa ngono ili alipwe. Hali kadhalika mwenye kutumia chambo cha pesa kama njia ya kukodi mwili wa mwezie kufanya mapenzi ni uasherati pia. Hawa wanaokodi mtu kwa minajili ya kutumia maungo yao kwa kujiridhisha kingono ndio wanaofanya wenye kufanya biashara hii iimarike.

Mwanaume mwenye kuridhia mahusiana na mfanya biashara huyo wa kukodisha maungo yake kwa ngono pengine huishia kufanya hata yasiyotegemewa ili mradi pesa yake itumike kwa namna anavyoona imemtosheleza hata kama ni kuharibu afya yake.

Kwa wenye upendo wa kweli wanajisikia haki sawa na kusaidiana iwe mdada au mkaka vyo vyote wanahitaji kwa pamoja kuwekana sawa iwe kimapenzi hali kadhalika kiuchumi. Mdada yuko tayari kumsaidia mkaka katika hali na mali na mkaka hali kadhalika.
Ipo siku mdada anam-take out mkaka na siku nyingine mkaka anam-take out mdada, hao ndio wanajua maana ya mapenzi ya kweli na uwajibikaji wa kila mmoja kwa mwenzake.

Ukishaona mdada anatanguliza dalili za deal ya mapenzi kibiashara ujue moja tu maisha yote hata mkioana utabaki kununua huba kwa sababu utaratibu wake kufanya mapenzi ni kukodisha mwili wake kwa malipo, na pengine ukawa na ziada peke yako financial kwa familia na yeye asijisikie kama ni sehemu ya jukumu lake.
  • Nini maana ya bf/gf au mume na mke?
  • Inajenga dhaba gani katika mapenzi ya kweli kuwa kukodishana kwa malipo?
  • Kwa nini wasichana wakiwa na shida ya kutimiziwa hamu ya ngono hawawakodi wanaume kwa malipo?

Kati ya wawili wanaojamihiana nani anayenufaika au kufurahia? Wote pamoja wanajisikia raha na kufarijika na kujisikia faraja toka kwa mwenzie. Iweje wakati wote mmeonja raha sawa halafu mwingine akamuliwe? Hii ndiyo hali ya mwanamke kujiruhusu kuwa chombo cha kutumiwa kibiashara kwa kukodisha mwili wake kwa muda utumiwe na mwanaume kuwa source ya mapato ya mwanamke kwa njia ya zinaa/ngono. Nakumbuka kuli ya mzee ruksa alipowaasa watanzania: "tuache ngono jamani, ukimwi utatumaliza, nawasihi tuache ngono jamani."

Kuna dalili wazi nyingine mojawapo ya msichana kuomba hili mara lile hata kama hamjafahamiana kutosha, maana yake amejitosheleza kwa kila anachohitaji hata kuhusu mwenza anaye, ila ni njia tu ya kukukatalia. Mwanaume kuendelea kubembeleza basi dau linapanda na kujikuta mwanaume laini na mwepesi kujiruhusu nusu ya mshara wake amalizie kwa starehe ya mahaba ya dakika chache. Pengine wengine licha ya kuwa na mwenza hugeuza nje ya mwenza kuwa kitegea uchumi, rejea paragraph ya kwanza niliyosema kujidhalilisha na kujiruhusu kudhalilika kwa kutumia maungo ya mwili wake kukodisha kama chambo cha kuwatega wanaume wammuminie michuzi ya kuishia.
:cheer2::cheer2::cheer2:​

Ukombozi wa wanawake walio wengi bado

Inamfikisha mfanya biashara kulegeza ugo kwa wateja kadhaa,
au Mwanaume kupitia bidhaa kadhaa

kwa sababu tu kukubali uteja, au kujiruhusu kuwa bidhaa.

:cheer2::cheer2::cheer2:
 
hivi kwani wanaume wanaojiuza nao wanafanya biashara ama yakwao ni halali?
kuna wale ambao hujiuza kwa wanawake hao nao tuwaiteje?
 
kupanga ni kuchagua

'kalia uchumi wako ufe maskini'

ila siku hizi hata wanamme wanajiuza, mashoga na walio straight.
naona leo akili yangu haiwazi vyema ila hebu nikuulize jambo Kongosho hivi wanaume wanalazimishwa kununua hizi bidhaa? je wasingekuwepo wakanunua unajua kwamba zisingefanyika? je wasingekuwa wanunuzi wafkiri wanawake wangekosa kitu chza kufanya ili wamudu maisha yao?

hivi umewah kuwaza kama mm kwamba yawezekana kabisa kwamba kuna kitu ambacho kiko unexploited simply kwasababu matumizi yake kwa sasa hayajulikan lkn ikatokea kitu kimoja kikatolewa kwenye system kitu hiki ambacho kiko dormant kigetake place???? sijui kama umenielewa .............
 
Last edited by a moderator:
hivi kwani wanaume wanaojiuza nao wanafanya biashara ama yakwao ni halali?
kuna wale ambao hujiuza kwa wanawake hao nao tuwaiteje?

Ye yote anayetumia mpango wa Mungu wa zaeni mkaongezeke kuwa biashara na bidhaa ni kundi hilo hilo. Bora wanyama mwitu ni ridhaa ya mapenzi ya kweli kuliko bidamu tunapogeuza utu na haki za maumbile kuyafanya bidhaa.
 
naona leo akili yangu haiwazi vyema ila hebu nikuulize jambo Kongosho hivi wanaume wanalazimishwa kununua hizi bidhaa? je wasingekuwepo wakanunua unajua kwamba zisingefanyika? je wasingekuwa wanunuzi wafkiri wanawake wangekosa kitu chza kufanya ili wamudu maisha yao?

hivi umewah kuwaza kama mm kwamba yawezekana kabisa kwamba kuna kitu ambacho kiko unexploited simply kwasababu matumizi yake kwa sasa hayajulikan lkn ikatokea kitu kimoja kikatolewa kwenye system kitu hiki ambacho kiko dormant kigetake place???? sijui kama umenielewa .............

Note nukuru hii toka kwenye mada:
Inamfikisha mfanya biashara kulegeza ugo kwa wateja kadhaa,
au Mwanaume kupitia wateja kadhaa
kwa sababu tu kukubali uteja, au kujiruhusu kuwa bidhaa.

Soma vizuri wote wameguswa katika mada hii kama nukuru ifuatayo:
Hali kadhalika mwenye kutumia chambo cha pesa (MWANAUME) kama njia ya kukodi mwili wa mwezie kufanya mapenzi ni uasherati pia. Hawa wanaokodi mtu kwa minajili ya kutumia maungo yao kwa kujiridhisha kingono ndio wanaofanya wenye kufanya biashara hii iimarike.
 
hivi kwani wanaume wanaojiuza nao wanafanya biashara ama yakwao ni halali?
kuna wale ambao hujiuza kwa wanawake hao nao tuwaiteje?

Akina dada ndio mnaotazamiwa kujenga utetezi wa haki zenu, onyesheni yanayowasibu kutokana na sisi akina kaka kutojali haki za msingi za mwanamke.
 
demand inasababisha supply iwepo.

Mfano, zamani tanzania tulizoea kuona utafiti wa dhahabu na chuma.

Ila baada ya komputa kuja, sasa watafiti wa rare earth minerals si wameongezeka sana

demand inadetermina supply sana.

naona leo akili yangu haiwazi vyema ila hebu nikuulize jambo Kongosho hivi wanaume wanalazimishwa kununua hizi bidhaa? je wasingekuwepo wakanunua unajua kwamba zisingefanyika? je wasingekuwa wanunuzi wafkiri wanawake wangekosa kitu chza kufanya ili wamudu maisha yao?

hivi umewah kuwaza kama mm kwamba yawezekana kabisa kwamba kuna kitu ambacho kiko unexploited simply kwasababu matumizi yake kwa sasa hayajulikan lkn ikatokea kitu kimoja kikatolewa kwenye system kitu hiki ambacho kiko dormant kigetake place???? sijui kama umenielewa .............
 
Last edited by a moderator:
demand inasababisha supply iwepo.

Mfano, zamani tanzania tulizoea kuona utafiti wa dhahabu na chuma.

Ila baada ya komputa kuja, sasa watafiti wa rare earth minerals si wameongezeka sana

demand inadetermina supply sana.
Lakini kitakwimu (statistics) supply ni kubwa kuliko demand. Hata hivyo bado supply inaonekana kuwa so cheap kiasi cha kuwa bidhaa za kutangaza kutafuta wateja kwa kujianika kwenye viambaza na kwenye mitaa mbalimbali na vibutio vya mikusanyko ya watu.
 
Jiulize why inaitwa 'the oldest profession in the world..
I know, but kinachonishangaza hata pale wale ambao ningetazamia wameelimika na hata kiuchumi hawako katika hali mbaya lakini kuwakuta katika mazingira ya kujigeuza bidhaa, inatia huruma sana kujidhalilisha kwa kiwango hicho.
 
I know, but kinachonishangaza hata pale wale ambao ningetazamia wameelimika na hata kiuchumi hawako katika hali mbaya lakini kuwakuta katika mazingira ya kujigeuza bidhaa, inatia huruma sana kujidhalilisha kwa kiwango hicho.


Wewe unawatazama wanawake kwa macho ya kiume
ndo maana unaona wanajidhalilisha

wenzio kitendo cha mwanaume kuwalipa kwa mwili wao sio kudhalilisha
deep down wanajua sio kila mwanamke akijiuza atapata soko...
anaejiuza anauzika......which to women sio kitu kidoogo sana

Ndo maana hata mwanamke awe vipi,akitazamwa na wanaume akipita anafurahi
hata kama kaolewa na Rais...
 
Ni suala la kimtazamo tu.

Wewe unaweza kuona kabisa kuwa vitendo anavyofanya mwanamke fulani ni dhalili.

Yeye akawa anaona kuwa si dhalili, na madhali ndivyo vinavyompa riziki yake halali basi yeye haoni ubaya.

Ndiyo maana kuna baadhi ya sehemu hapa duniani ukahaba ni ajira halali kabisa.
 
Wewe unawatazama wanawake kwa macho ya kiume
ndo maana unaona wanajidhalilisha

wenzio kitendo cha mwanaume kuwalipa kwa mwili wao sio kudhalilisha
deep down wanajua sio kila mwanamke akijiuza atapata soko...
anaejiuza anauzika......which to women sio kitu kidoogo sana

Ndo maana hata mwanamke awe vipi,akitazamwa na wanaume akipita anafurahi
hata kama kaolewa na Rais...


Kwangu mimi maana kamili ya upendo wa kweli ni pale ninapoona wote kwa pamoja wanafurahia matunda ya upendo wao bila mmoja kujigeuza kuwa chombo cha kulipiwa na mwenzake wakati wote wanafurahia na kupata raha ile ile.

Kwa wenye upendo wa kweli wanajisikia haki sawa na kusaidiana iwe mdada au mkaka vyo vyote wanahitaji kwa pamoja kuwekana sawa iwe kimapenzi hali kadhalika kiuchumi. Mdada yuko tayari kumsaidia mkaka katika hali na mali na mkaka hali kadhalika. Ipo siku mdada anam-take out mkaka na siku nyingine mkaka anam-take out mdada, hao ndio wanajua maana ya mapenzi ya kweli na uwajibikaji wa kila mmoja kwa mwenzake.

Nilichokuwa na fikiri wale wasio na ajira na hali ngumu ya maisha mazingira hayo huwasukuma kufanya hayo. Lakini kibaya ambacho kimenisukuma kuandika makala haya ndogo ni kile ambacho sikuamini kwa macho yangu niliposhuhudia mdada ninayemkuta mara nyingi kwenye ofisi fulani mwenye siha na kazi nzuri akiwa katika ziara sehemu isiyo rasmi kujifanya urimbo kupata mteja. Ilinishtua amini usiamni. kujidhalilisha kwa kiwango hicho.
 
Ni suala la kimtazamo tu.

Wewe unaweza kuona kabisa kuwa vitendo anavyofanya mwanamke fulani ni dhalili.

Yeye akawa anaona kuwa si dhalili, na madhali ndivyo vinavyompa riziki yake halali basi yeye haoni ubaya.

Ndiyo maana kuna baadhi ya sehemu hapa duniani ukahaba ni ajira halali kabisa.

Uhalaliswaji wa shughuli hiyo ya kukodisha mwili utumiwe na mtu kwa kujiliwaza kwa muda ungekuwa na utaratibu maalum. Hata hizo nchi unazosema zimehalalisha jambo hilo, kuna utaratibu ambao unakubalika, kinyume chake ni kudakwa na corps na kuswekwa ndani iwe mwanaume au mwanamke.

Bahati mbaya kwa Tanzania inaelekea jambo hilo ni wanaotazamwa ni wanawake tu, lakini nchi zilizoendelea kama ulizosema mtego ni kwa wanaume pia wanaotafuta hao wanajitegesha sehemu kudaka wateja. Mchezo ni kuwaweka askari kanzu au wasichana wa kukodiwa na polisi waliojilegeza huku wakiwa na vitendea kazi vyao kufumba na kufumbua jamaa ananaswa live, hapo mchezo wa wanawake unapotea kwa vile hakuna mteja aliyetayari kujiweka kwenye risk kwani huwezi jua aliyejitegesha ni malaya au polisi kama picha hapo chini inavyoonysha huyu mdada ni mpolisi anayenasa watafutaji.

images
 
kupanga ni kuchagua

'kalia uchumi wako ufe maskini'

ila siku hizi hata wanamme wanajiuza, mashoga na walio straight.

Aka mwenzangu! Duniani tupo wengi, wakati wapo wengi wanaoshabikia mfumo wa kibidhaa kwa wateja zao lakini wapo pia wachache wanaojali maana, heshima na ustaadhi wa maisha yao katika jamii kuwa na hali halisi ya maisha na mapenzi ya kweli yenye kubebwa na wapenzi wote wawili kwa ushirikiano wa kweli katika taabu na raha. Kwa hili sifi na njaa kwa vile wenyewe wasio biashara na wasio bidhaa kwa wateja wanatafuta na kupata wa aina yao, hapo njaa nitapataje nafasi?

Bidhaa hutembezwa na hutangazwa ili wateja wazione, wazikague na wafanye makubaliano ya bei yake, kwa mwendo huo tegemea kupata bidhaa si mwenzi mwenye penzi lenye kuridhia maisha ya ushirikiano hata kiuchumi. Wa aina yangu sitegemei kupata maeneo walikojitandaza kibidhaa kama machinga wafanyavyo Kariakoo, bali kama wahenga wetu nilivyoona walivyofanya huko nikutulia aliyetulia yule pale, familia ile wanalea vizuri, oh rafiki yako fulani aliniambia yule kijana poa sana, wajua dada yule tabia yake ina mvuto wa aina. Wajua tuliposafiri siku ile dada fulani anavyoshirikisha alicho nacho ni hazina ukimwoa. Mwenzako nguo zangu hizi gf wangu huninunulia mara kwa mara kunipa zawadi. Wajua mke wangu ndiye mwenye kuhakikisha nguo nzuri ndiye anayezijua maduka bora ya kununua anachonidai ni saizi nitumiayo kwani anasema gharama kama hizi ni jukumu lake anaposhughulikia nguo za watoto ndo kazi yetu akina mama ati. Kuna mengi lakini wenzangu mwajua zaidi.

Waso na tabia ya ridhio la radhi ya mapenzi ndio wanaolizwa na njaa, kwani mshiko usipokubali hakuna penzi ndio dhana ya mfumo wa kibidhaa kwa mteja lete dau upate penzi, la sivyo no love, lakini wenye kujawa na ridhio la mapenzi yasiyo na uchoyo wa kutoa na kupokea kwa mpenzie ambaye pia si haba kwa kumridhia mwinzie kwa kupokea na kutoa maisha yao huwasitiri na mangi. Tulia duniani hutakosa wa kiwango chako kama uko mkweli na mstahimilivu.
 
Wewe unawatazama wanawake kwa macho ya kiume
ndo maana unaona wanajidhalilisha

wenzio kitendo cha mwanaume kuwalipa kwa mwili wao sio kudhalilisha
deep down wanajua sio kila mwanamke akijiuza atapata soko...
anaejiuza anauzika......which to women sio kitu kidoogo sana

Ndo maana hata mwanamke awe vipi,akitazamwa na wanaume akipita anafurahi
hata kama kaolewa na Rais...

Aksante The Boss umeielewa vema pyschology ya wanawake waliopo katika hii profession. Haijalishi mtu ameelimika kiasi gani, ana pesa kiasi gani kile anachokipata pyschologically kutokana na maamuzi yake anayoamini ni sahihi ni kikubwa zaidi kuliko tunavyoweza kufikiria. Hata wale wanaofikiria kuwa ni ukosefu wa kujitambua thamani zao wanakosea kwani wengi tunajitambua na thamani yetu tunaielewa tofauti inakuja ni aina ya thamani na kiwango tunachokiweka katika thamani hizo. Kuna wale ambao wanaamini katika thamani ya kuwa na mume mmoja na wale wanaoamini wameumbwa wakaumbika kama wanawake na hivyo kuweka price tags katika miili yao. Kwa mtu wa aina hii, ukimweleza kuwa mwili wako una thamani kubwa kuliko millioni 2/3 anazozipata kwa mwezi na kwa bahati mbaya hiyo thamani unayojaribu kumshaishi haipimiki quantitatively utakuwa unatwanga maji kwenye kinu.
 
Last edited by a moderator:
Refer to this thread https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/349080-raha-ya-tendo-la-ndoa-kwa-m-mke.html

Nilitoa jibu ndefu, lakini ntarudia point nilizoandika:

Kwenye uchangudoa, this is a matter of supply and demand. Let me explain. Men have more of a sexual appetite than women. There are different things that can get in the way of women's ability to have sex e.g. period, pregnancy, stress or just not being happy in general. Since sex is something men want/need to have they resort to paying for it so that it is readily available whenever they need it. This is when the changudoa comes in. Uchangudoa usingekuwepo kama demand ya sex isingekuwepo.


Inaelekea unajua breakdown ya cost ya machangudoa. Ninachojua kuwa unalipia kwa ajili ya muda wake. Whether or not the sex is good or how long/how many times you climax does not matter. You still have to pay. The reason prostitution is illegal is because it is not taxable. I believe prostitutes can enjoy sex as well, but that shouldn't mean you get a discount. The best sex is when both participants are having fun, so consider that a bonus.




Kuhusu kutumia mwili kama asset, turudi kwenye idea ya demand and supply. Typically, we live in a male-dominated society. We have men that are employers, teachers, professors, police men; and essentially bread winners. Women can use their bodies for sexual favours in exchange of cash, employment, and passing examinations from men. Again, if men were more in control of their urges, none of this would be an issue. Wanaume wanaotembea na wanawake ili kujipatia mali au promotion (gigolos, serengeti boys) pia wapo, lakini si wengi kama wanawake sababu si wanawake wengi ambao ni willing kuhonga au kulipia kwa ajili ya mapenzi. Another issue of demand and supply. Ni rahisi zaidi kwa mwanamke kupata mtu wa kutembea nae bila malipo kuliko mwanamme kupata mwanamke wa kutembea nae bila malipo. Fact.




images
images
images
images
Eneo moja wapo ambalo vigumu kwa wanawake wengi
kupata ukombozi kamili
Mwanamke anapojiruhusu kudhalilishwa na kujidhalilisha ni pale anapoamua kuwa chombo cha kutumiwa kwa malipo mojawapi ikiwa ni kufanya ngono kwa kubadilishana na pesa au vitu, na mtu uamuapo kutumika kwa malipo pasipo ridhaa ya moyo wa kuridhiana dhana kamili na halisi ya mapenzi yenye kuwaburudisha wote ni kujigeuza bidhaa. Hata wawili mnaporidhiana kimapenzi na kupendana lakini mmoja kuhitaji ziada ya raha wanazopata wote pamoja akirimiwe malipo kwa kustarehe wote ni dhana ya kutumia maungo ya mwili wake kwa minajili ya kufanya ngono kwa malengo ya kibiashara.

Bila malipo hayuko radhi kufanya ngono hata kama wamependana, hivyo dhana ya mapenzi kwa msichana wa aina hiyo ni biashara ya mapenzi /ngono aina ambayo kwa tafsiri nyepesi ni uasherati. Uasherati ni msamiati usioleta maana nzuri katika jamii lakini ni wengi tu wanaofanya uasherati kwa maana lete pesa tufanye ngono maana hakuna mwasherati anayeweza kufanya ngono bila malipo kwa vile ameshajiruhusu kuwa ni bidhaa ya kunadi mwili wake kwa ngono ili alipwe. Hali kadhalika mwenye kutumia chambo cha pesa kama njia ya kukodi mwili wa mwezie kufanya mapenzi ni uasherati pia. Hawa wanaokodi mtu kwa minajili ya kutumia maungo yao kwa kujiridhisha kingono ndio wanaofanya wenye kufanya biashara hii iimarike.

Mwanaume mwenye kuridhia mahusiana na mfanya biashara huyo wa kukodisha maungo yake kwa ngono pengine huishia kufanya hata yasiyotegemewa ili mradi pesa yake itumike kwa namna anavyoona imemtosheleza hata kama ni kuharibu afya yake.

Kwa wenye upendo wa kweli wanajisikia haki sawa na kusaidiana iwe mdada au mkaka vyo vyote wanahitaji kwa pamoja kuwekana sawa iwe kimapenzi hali kadhalika kiuchumi. Mdada yuko tayari kumsaidia mkaka katika hali na mali na mkaka hali kadhalika.
Ipo siku mdada anam-take out mkaka na siku nyingine mkaka anam-take out mdada, hao ndio wanajua maana ya mapenzi ya kweli na uwajibikaji wa kila mmoja kwa mwenzake.

Ukishaona mdada anatanguliza dalili za deal ya mapenzi kibiashara ujue moja tu maisha yote hata mkioana utabaki kununua huba kwa sababu utaratibu wake kufanya mapenzi ni kukodisha mwili wake kwa malipo, na pengine ukawa na ziada peke yako financial kwa familia na yeye asijisikie kama ni sehemu ya jukumu lake.
  • Nini maana ya bf/gf au mume na mke?
  • Inajenga dhaba gani katika mapenzi ya kweli kuwa kukodishana kwa malipo?
  • Kwa nini wasichana wakiwa na shida ya kutimiziwa hamu ya ngono hawawakodi wanaume kwa malipo?

Kati ya wawili wanaojamihiana nani anayenufaika au kufurahia? Wote pamoja wanajisikia raha na kufarijika na kujisikia faraja toka kwa mwenzie. Iweje wakati wote mmeonja raha sawa halafu mwingine akamuliwe? Hii ndiyo hali ya mwanamke kujiruhusu kuwa chombo cha kutumiwa kibiashara kwa kukodisha mwili wake kwa muda utumiwe na mwanaume kuwa source ya mapato ya mwanamke kwa njia ya zinaa/ngono. Nakumbuka kuli ya mzee ruksa alipowaasa watanzania: "tuache ngono jamani, ukimwi utatumaliza, nawasihi tuache ngono jamani."

Kuna dalili wazi nyingine mojawapo ya msichana kuomba hili mara lile hata kama hamjafahamiana kutosha, maana yake amejitosheleza kwa kila anachohitaji hata kuhusu mwenza anaye, ila ni njia tu ya kukukatalia. Mwanaume kuendelea kubembeleza basi dau linapanda na kujikuta mwanaume laini na mwepesi kujiruhusu nusu ya mshara wake amalizie kwa starehe ya mahaba ya dakika chache. Pengine wengine licha ya kuwa na mwenza hugeuza nje ya mwenza kuwa kitegea uchumi, rejea paragraph ya kwanza niliyosema kujidhalilisha na kujiruhusu kudhalilika kwa kutumia maungo ya mwili wake kukodisha kama chambo cha kuwatega wanaume wammuminie michuzi ya kuishia.
:cheer2::cheer2::cheer2:​

Ukombozi wa wanawake walio wengi bado

Inamfikisha mfanya biashara kulegeza ugo kwa wateja kadhaa,
au Mwanaume kupitia wateja kadhaa

kwa sababu tu kukubali uteja, au kujiruhusu kuwa bidhaa.

:cheer2::cheer2::cheer2:
 
kupanga ni kuchagua

'kalia uchumi wako ufe maskini'

ila siku hizi hata wanamme wanajiuza, mashoga na walio straight.



thats right
wale wajamaa wanaoitwa kwa jina la mjini kama "mari o"

wanatoa huduma kwa mashuga mami ili wapate kuendesha maisha yao

mjin shule hapa
 
Cheap ni relative term

As long as demand ipo, supplier wameongezeka kama ilivyo kwenye biashara zingine
Kumbuka wakati M-Pesa inaanza ilivyokuwa deal ama kuuza gesi za kupikia majumbani
Sasa hivi kila mahali M-pesa zimejaa, wauza gesi ni wengi na wananyang'anyana wateja, haina tofauti na wanaouza miili

Nachoweza kusema ni kuwa, katika Tanzania mostly tuna SMEs, hali kadhalika machangu wana-operate kama small scale sex workers kutokana na ujuzi labda mdogo, mitaji midogo na kukosa market network ya ku-export miili yao nje.

Hebu tizama, baadhi ya sex workers waliopatafursa na kuzitumia vema, wapo wanaoenda kujiuza nchi za nje (refer malalamiko ya Ubalozi wa China nchini hadi kuongeza mchakato wa utoaji wa visa)

Biashara ya kuuza miili nchini ina matatizo yanayoshabihiana na matatizo ya wafanyabiashara wengine kama kawaida, kwa hiyo si kwamba ni cheap but the business environment iko hivyo ilivyo.

Lakini kitakwimu (statistics) supply ni kubwa kuliko demand. Hata hivyo bado supply inaonekana kuwa so cheap kiasi cha kuwa bidhaa za kutangaza kutafuta wateja kwa kujianika kwenye viambaza na kwenye mitaa mbalimbali na vibutio vya mikusanyko ya watu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom