My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Tunamjua vizuri sana huyo ni agent wa TISS, na hatutamruhusu kutuharibia ChamaWanabodi,
Baada ya kutulia kwa tishio ugonjwa wa Corona, sasa watu hawana uoga tena, hivyo sasa Vuguvugu la kugombea urais wa JMT uchaguzi Mkuu wa October, limeanza kupanda joto, kwa moto wa urais kuwashwa na mwanadada, msomi wa Ph.D, Dr. Mayrose Majinge, amekuwa ndie mwanamke wa kwanza kujitokeza kutangaza nia ya kuwania kuteuliwa kugombea nafasi ya urais wa JMT kwa tiketi ya kupitia Chadema.
View attachment 1459773View attachment 1459775View attachment 1459776
Mimi nimetokea kumfahamu mwanamke huyu, kwanza ni msomi, pili ni mwanamke wa shoka, na anauwezo, yaani kama ni jembe, huyu mdada ni jembe kweli, na ni mwanaharakati wa ukweli ila kuna swali moja tuu najiuliza kumhusu huyu dada
Kama Chadema ina watu wazuri kama hawa tena wana CV nzito kama hii, walikuwa wapi siku zote hizi hadi mtu kama huyu asiteuliwe ubunge viti maalum Chadema, na badala yake Chadema ikatujazia baadhi ya yale makorokocho kule Bungeni?!.
Jibu langu ni moja tuu, kuna uwezekano ni kweli ubunge wa viti maalum Chadema unapatikana kwa namna fulani, ambayo kwa jinsi ninavyomfahamu huyu dada alivyo ni mtu wa msimamo, ni mcha Mungu, hivyo hizo namna za kumpatia ubunge wa viti maalum Chadema zilimshinda akaamua kutulia, sasa kama ubunge tuu wa viti maalum alishindwa kupewa Chadema, kutokana na misimamo ya kukataa mambo fulani, jee sasa kwenye urais ndio atapitishwa?!
Kwa vile mimi namfahamu vizuri huyu dada na niliwahi kumzungumza humu,
Uenyekiti wa UWT: Ni Vita Kati ya Ukweli na Ubatili! - JamiiForums
Huko nilichangia hivi
Haya niliyasema tarehe 3 Agust, 2012, leo nimeiona hii picha
Kiukweli Chadema imevuna Jembe!. Hata BAWACHA itafufuka na itasimama na kuipuku UWT!.
Hongera Mayrose kwa kuukubali ukweli. Nakukumbusha mane yangu haya
Hivyo naamini, mimi ni miongoni mwa waliomshawishi huyu dada kujiunga Chadema ya enzi ile, na kama amedumu Chadema muda wote huu, bila any recognition ya aina yoyote, then ile Chadema niliyomshauri kujiunga ni Chadema ile, ila kwa Chadema hii...
View attachment 1459777
Kwa wale mtakaopata nafasi, tumsikilize hapa asubuhi hii.
Ushauri wangu kwake ni saa hizi hajachelewa, ajirudie tuu nyumbani kumenoga, Chadema is a sinking ship, asipoamua mapema, ana zama nayo.
All the best Dada Dr. Mayrose Majinge.
Mimi ni Kaka yako Mkubwa
Paskali.