Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 51,985
- 69,372
Mwanamke aitwaye Mariam mkazi wa Sinza Lion Dar es Salaam, amejeruhiwa kwa kupigwa risasi maeneo ya begani katika harakati za Polisi kuwatuliza raia wenye hasira kali waliokuwa wanataka kumpiga mwizi aliyekwapua simu kwenye bodaboda majira ya saa 12:00 asubuhi ya leo Mei 20, 2022
Kwa maelezo ya mashuhuda wa tukio hilo, wanadai baada mwizi huyo kukwapua simu alikimbilia nyumba iliyokuwa jirani na baadaye kidogo walitokea maaskari waliomwokoa mwizi lakini katika harakati za kuwatuliza raia, inadaiwa walifyatua risasi iliyomjeruhi raia huyo ambaye amekimbizwa hospitali
Chanzo: EATV
SOMA PIA:
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 20, 2022, wakati akizungumza na East Africa TV & EA Radio Digital, ili kutoa ufafanuzi wa madai yaliyotolewa na mashuhuda wa tukio hilo kwa kusema kwamba mwanamke huyo aitwaye Mariam amejeruhiwa na polisi.
"Ni kweli tukio hilo limetokea na jeshi linaendelea kulifuatilia, lakini ni kwamba askari walifyatua risasi juu katika juhudi za kumuokoa mtuhumiwa na kwa bahati mbaya kuna mwanamke amejeruhiwa ingawa anaendelea vizuri," amesema Kamanda Muliro.
Aidha Kamanda Muliro akimzungumzia mwizi huyo amesema, "Huyo mtuhumiwa hatujamtambua kwa sababu hajaweza kuongea, alikuwa tayari amepigwa, hawezi kuongea, hivyo tunalichunguza tukio hilo".
Kwa maelezo ya mashuhuda wa tukio hilo, wanadai baada mwizi huyo kukwapua simu alikimbilia nyumba iliyokuwa jirani na baadaye kidogo walitokea maaskari waliomwokoa mwizi lakini katika harakati za kuwatuliza raia, inadaiwa walifyatua risasi iliyomjeruhi raia huyo ambaye amekimbizwa hospitali
Chanzo: EATV
SOMA PIA:
Muliro azungumzia raia aliyejeruhiwa kwa risasi
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha tukio la mwanamke kujeruhiwa kwa risasi leo maeneo ya Sinza Lion, na kusema imempata kwa bahati mbaya baada ya Askari kufyatua risasi juu kwa lengo la kuwatawanya wananchi waliokuwa wanampiga mwizi wa simu.Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 20, 2022, wakati akizungumza na East Africa TV & EA Radio Digital, ili kutoa ufafanuzi wa madai yaliyotolewa na mashuhuda wa tukio hilo kwa kusema kwamba mwanamke huyo aitwaye Mariam amejeruhiwa na polisi.
"Ni kweli tukio hilo limetokea na jeshi linaendelea kulifuatilia, lakini ni kwamba askari walifyatua risasi juu katika juhudi za kumuokoa mtuhumiwa na kwa bahati mbaya kuna mwanamke amejeruhiwa ingawa anaendelea vizuri," amesema Kamanda Muliro.
Aidha Kamanda Muliro akimzungumzia mwizi huyo amesema, "Huyo mtuhumiwa hatujamtambua kwa sababu hajaweza kuongea, alikuwa tayari amepigwa, hawezi kuongea, hivyo tunalichunguza tukio hilo".