Mwanakijiji na Uislamu wa TAA/TANU mpaka CCM

kinachonishangaza pia ni kuwa watu wameshindwa kusoma hiyo alama ya 'kuuliza' ambayo ilikuwepo kwenye makala tangu mwanzo na hawajajiuliza kwanini sikuiweka kama statement of fact. Mada nzima ni swali wala haitoji jibu lakini kwa anayelisoma hilo swali anapata jibu ndani yake. Lakini watu wamekuja juu na kufikiria nimesema CCM ni chama cha Waislamu na Chadema chama cha Wachagga. Wanasahau hata ufunguzi wa hoja yangu umewekwa kwenye misingi ipi: NImeanza hoja kwa kusema hivi:




Hivi ni gumu sana kujua maana ya kujenga hoja ya kimantiki na kuonesha ukweli kwa kutumia kuizungusha lugha?

Mzee Mwanakijiji,


Tatizo ni reading skills zetu sisi watanzania ziko chini sana, watu huwa hatusomi kwa weledi unaotakiwa na kujiridhisha kuwa mantiki ya hoja aliyo andika mwandishi ndo hiyo niliyoelewa?


Unajua tena watanzania hatujazoea kusoma makala zilizoandikwa kwa kumfikirisha msomaji na kuwa makini kuvumbua lengo la kimantiki la mwandishi, jamani tujaribu kuboresha our reading skills vile vile
 
simple question kwa mwanakijiji. kwanini usiseme ccm na waislam. cdm na wakiristo: umerukia jamii ndogo ya wachaga?

haijalishi ningetumia ulinganisho gani mwingine pointi yangu ingebakia vile vile: Hivi ningesema "Chadema cha Watu wa Kaskazini; CCM cha Watu wa Pwani"? na kuonesha jinsi gani watu wengi wa Kaskazini walivyoshiriki kuiunda Chadema na kuwataja kwa majina yao kuwa wanatokea kaskazini bila kutaja dini wala mabila yao halafu ningetumia mwelekeo huo huo kuelezea watu wa Pwani walioshiriki kuunda TANU na CCM na jinsi ambavyo wameshika udhibiti wa Chama unajua wangekuja na kusema "watu wa pwani" nilikuwa namaanisha nini?
 
umesema kweli mkuuuu,mi nadhani mohamed hakuelewa makala adhimu ya mwanakijiji ndo maana analeta utetezi usio eleweka kama ambavyo hakumuelewa mwanakijiji
 
There are currently 51 users browsing this thread. (15 members and 36 guests)

Peasant,VISIONEER,Tumaini Jipya,Ame,chetuntu,Mohammed Shossi,Ngekewa,Prof Kasambanda,Mzee wa Rula,GWeLa 2003,Mr.Mak,Masanga,


Jamaa kaona amechemsha kaamua kukaa kimya kwenye thread yake mwenyewe!!
 
Hivi mliona wapi punda akilazimishwa kupura pumba na kukubali? Kwa lugha nyepesi ni kwamba huwezi kumwelewesha mtu mzima kitu alichokwisha jiamulia (hii ni kama vile tulivyohojiana na Mzee Mohammed Said kuhusu historia ya Tanganyika mpaka thread ikafungwa). Hapa ni wazi kuwa Mohammed Shossi ameamua kutoelewa hoja ya Mwanakijiji sasa tutabishana hapa mpaka asubuhi lakini ngoma bado nzito.
 
Shossi kwa vile umechagua kutokuelewa nilichoandika itabidi nikusaidie tu kwa moyo mkunjufu :


  1. Nukuu kwenye andiko langu la awali ni wapi nimesema kuwa "TAA mpaka CCM iilijaa Waislamu watupu"?Mohammed Said katika kitabu chake cha Abdulwahid Sykes anasema "TANU kuanzia mwanzo kilikuwa ni chama cha Waislamu" unakubaliana naye? - si maneno yangu hayo.
  2. Kwa vile umeweza kuonesha kuwa walikuwepo Wakristu katika TANU kitu ambacho mwanahistoria yeyote wa Tanzania anajua vizuri sana na kutokana na uwepo wake ina maana Mohammed Said amepotosha kwenye kitabu chache. Kama hili ni kweli TANU ilianzishwa kwa ushirikiano sawa wa Wakristu na Waislamu na dini zao hazikuwa sababu ya kujiona kuwa wanamiliki chama kwanini kitabu cha Mohammed Said kinaaminiwa na wapo wanaoamini kuwa ni "Waislamu ndio walioanzisha TANU" wakati kulikuwepo na Wakristu ambao tunawajua "majina na hata idadi yao"?
  3. Kama kuwepo kwa Wakristu ndani ya TANU kunafuta dhana ya TANU kama chama cha Waislamu kitu ambacho nakubaliana nacho (ndio maana nilisema hoja ya kuwa TANU ni chama cha Waislamu haina nguvu pale utakapoingiza Wakristu wake ndani yake) inakuwaje kuwepo kwa Watu wasio Wachagga ndani ya Chadema isivunje hoja ya Chadema kuwa ni chama cha Wachagga?
  4. Sote tunajua vizuri tu kuwa hakuna chama nchini ambacho kimeundwa kikiwa na watu wa dini moja, sehemu moja au kabila moja tu. HAKUNA. Lakini wapo watu walioafanikiwa kuwashawishi watu kwamba kati ya vyama vyote nchini ni Chadema ndicho ni cha "Wachagga, Wakristu na watu wa Kaskazini". Hata hivyo tunajua wapo Waislamu, Wasukumua na Wakerewe, Wahehe na Wangoni n.k na wapo watu wa Kusini (hadi MBozi na Katavi) n.k lakini pamoja na yote hayo kujulikana lakini bado watu wanaamini kuwa Chadema ni chama cha kidini, kikabila na kikanda?
  5. Umehamaki kuona kuwa nimewashambulia Waislamu; hivi unafikiria Wachagga wanajisikiaje wanaponyoshewa kidole na viongozi na wananchi wenzao ? Au mnafikiri Wachagga nao hawana hisia? Mnataka Wachagga wasijiunge na Chadema kwa sababu wakifanya hivyo watakuwa wanaonesha kuwa ni chama chao? Mnataka Wachagga, Wakristu na watu wa Kaskazini wanaotaka kujiunga na Chadema wakataliwe, waliopo wahesabiwe, na wenye nafasi mbalimbali waziachie kama mtu mmoja alivyowahi kupendekeza humu ili kufanya chama kisionekane cha "kikabila, Kikristu na Kikanda?

MMK hoja yako niliielewa vizuri sana na hata ufafanuzi wako umeendelea kupanua hoja. Kwa mtu makini asiyekurupuka, hatapata shida ya kujua nini haswa ulikusudia kuwasilisha. Ukweli ni kwamba hakuna propaganda zinazonikera kama hii ya kusema chadema ni chama cha wachaga na wakatoliki. Ebu fikiria mtandao wa chadema ulivyokuwa mpana baada ya uchaguzi wa 2010! Kuanzia mashariki ya nchi hadi magharibi, kwenda kaskazini hadi kusini! Nape Nnauye alipoongea waziwazi suala la uchaga wa chadema ilinisikitisha sana. Kwa ufupi, mimi sasa naamini kwamba hoja za udini na ukabila zinakuzwa na chama cha magamba baada ya kuzidiwa majukwaani. Nyerere alitabiri kuhusu tabia hii na sasa imejidhihirisha ndani ya chama alichoasisi mwenyewe.
 
MMK hoja yako niliielewa vizuri sana na hata ufafanuzi wako umeendelea kupanua hoja. Kwa mtu makini asiyekurupuka, hatapata shida ya kujua nini haswa ulikusudia kuwasilisha. Ukweli ni kwamba hakuna propaganda zinazonikera kama hii ya kusema chadema ni chama cha wachaga na wakatoliki. Ebu fikiria mtandao wa chadema ulivyokuwa mpana baada ya uchaguzi wa 2010! Kuanzia mashariki ya nchi hadi magharibi, kwenda kaskazini hadi kusini! Nape Nnauye alipoongea waziwazi suala la uchaga wa chadema ilinisikitisha sana. Kwa ufupi, mimi sasa naamini kwamba hoja za udini na ukabila zinakuzwa na chama cha magamba baada ya kuzidiwa majukwaani. Nyerere alitabiri kuhusu tabia hii na sasa imejidhihirisha ndani ya chama alichoasisi mwenyewe.


Wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka jana niliandika makala hii kwenye Tanzania Daima NI NANI ALIYEINGIZA UDINI KWENYE UCHAGUZI HUU?

Nilianza kwa kusema hivi:

SIJUI kama mwenzangu umegundua kuwa siku za karibuni wanasiasa wetu na watawala wetu walioshindwa wameanza kulalamika kuwa kuna udini unaingizwa katika kampeni hizi huku baadhi yao wakidai kuwa kuna watu wanawashawishi watu kupiga kura kwa misingi ya dini. Ukiwasikiliza vile unaweza kuamini kabisa kuwa hawajui jinsi gani suala la udini limeingia kwenye kampeni na sasa wameshtuka kuwa linaweza kuwagharimu uchaguzi, kuzaa vurugu na hata kusababisha machafuko nchini. Lakini mtu mwenye hekima hana budi kujiuliza tulifikaje mahali ambapo dini inaonekana kuwa sehemu ya kampeni hii?


Nilianisha kwenye makala ile kuwa ni watawala ndio wamekuwa wakiwachezea Watanzania akili zao. Sasa hii hoja tumeamua kuivunja mara moja na daima.
 
check: Nadhani utagundua maana ya neno "fallacy".
Kwanini awatoe hao kwenye nyekundu tu na asiwataje wengine waliobakia ilhali tunawajua wa majina na idadi yao? hebu jiulize halafu utajua alichokikusudia ili makala yake inoge!

Hapo mwanakijiji alijaribu kuthibitishia umma ya kuwa CCM sio cha kidini wala CHADEMA sio cha kikabila basi. Katika techniques za uandishi kuna kitu wanaita FALLACY
defn from wikipedia : In informal logic and rhetoric, a fallacy is usually incorrect reasoning in argumentation resulting in a misconception. By accident or design, fallacies may exploit emotional triggers in the listener or interlocutor (e.g. appeal to emotion), or take advantage of social relationships between people (e.g. argument from authority). Fallacious arguments are often structured using rhetorical patterns that obscure the logical argument, making fallacies more difficult to diagnose. Also, the components of the fallacy may be spread out over separate arguments.

Nasikitika ya kuwa ww umekuwa victim mkubwa wa Hii makala kiuwelewa. Kwenye hoja yako umeijenga kwa misingi ya kudhania kuwa Mwanakijiji hawajui hao uliosema lakini MKJJ alikuwa wazi kabisa ili nyie msiojua fallacy msije mkapotea njia. LAKINI WW USHASHINDIKANA. YAELEKEA HATA KILE KITABU CHA KUSADIKIKA HUKUELEWA PIA WALA KILE CHA MFALME JUHA
 
Wakuu kupinga hoja ya Mwanakijiji kwa mtizamo wa thread hii (waanzilishi wa chadema) it's just simple just come with the names like wanzishaji Chadema ni hawa Freeman Mbowe, Edwin Mtei, John Shayo, William Kimaro, George Mrema, Antony Mmmari, Elisikia Ngowi, Elibariki Lyaruu. Yes!!! ya kwamba si mnawaona waanzilishi wa Chadema lakini angalia diversity ya walioanzisha CCM. Otherwise mtazunguka wee huku mnaongea kitu kile kile. kifupi ni kwamba hakuna chama kilichosajiliwa Tanzania ambacho ni cha wachaga, au cha waislamu au cha wakristo period!
 
Mzee Mwanakijiji,


Tatizo ni reading skills zetu sisi watanzania ziko chini sana, watu huwa hatusomi kwa weledi unaotakiwa na kujiridhisha kuwa mantiki ya hoja aliyo andika mwandishi ndo hiyo niliyoelewa?


Unajua tena watanzania hatujazoea kusoma makala zilizoandikwa kwa kumfikirisha msomaji na kuwa makini kuvumbua lengo la kimantiki la mwandishi, jamani tujaribu kuboresha our reading skills vile vile

Mkuu jingine kubwa na hatari ni pale mtu anapoamua kutumia hisia na mihemko kujenga hoja, maana kuna wasomi humu ati!!. We always mix facts and opinions. Mara nyingi unakuta tunaegemea kulazimisha opinions kuwa facts, na tukiambiwa the real facts tunakuwa wazito kukubali au kuwa convinced.
 
check: Nadhani utagundua maana ya neno "fallacy".


Hapo mwanakijiji alijaribu kuthibitishia umma ya kuwa CCM sio cha kidini wala CHADEMA sio cha kikabila basi. Katika techniques za uandishi kuna kitu wanaita FALLACY
defn from wikipedia : In informal logic and rhetoric, a fallacy is usually incorrect reasoning in argumentation resulting in a misconception. By accident or design, fallacies may exploit emotional triggers in the listener or interlocutor (e.g. appeal to emotion), or take advantage of social relationships between people (e.g. argument from authority). Fallacious arguments are often structured using rhetorical patterns that obscure the logical argument, making fallacies more difficult to diagnose. Also, the components of the fallacy may be spread out over separate arguments.

Nasikitika ya kuwa ww umekuwa victim mkubwa wa Hii makala kiuwelewa. Kwenye hoja yako umeijenga kwa misingi ya kudhania kuwa Mwanakijiji hawajui hao uliosema lakini MKJJ alikuwa wazi kabisa ili nyie msiojua fallacy msije mkapotea njia. LAKINI WW USHASHINDIKANA. YAELEKEA HATA KILE KITABU CHA KUSADIKIKA HUKUELEWA PIA WALA KILE CHA MFALME JUHA

Kama wewe si mwalimu basi una moyo kweli wa kufundisha.
 
Wakuu kupinga hoja ya Mwanakijiji kwa mtizamo wa thread hii (waanzilishi wa chadema) it's just simple just come with the names like wanzishaji Chadema ni hawa Freeman Mbowe, Edwin Mtei, John Shayo, William Kimaro, George Mrema, Antony Mmmari, Elisikia Ngowi, Elibariki Lyaruu. Yes!!! ya kwamba si mnawaona waanzilishi wa Chadema lakini angalia diversity ya walioanzisha CCM. Otherwise mtazunguka wee huku mnaongea kitu kile kile. kifupi ni kwamba hakuna chama kilichosajiliwa Tanzania ambacho ni cha wachaga, au cha waislamu au cha wakristo period!

Unajua Nyambala, wanaweza kabisa kufanya hivi na imekuwa ikifanywwa kwa muda mrefu sana. Tatizo ukifuata hiyo "logic" ya kuangalia majina na mahali ukiihamishia CCM tu wanaona "haiwezekani"!
 
Shossi kwa vile umechagua kutokuelewa nilichoandika itabidi nikusaidie tu kwa moyo mkunjufu :


  1. Nukuu kwenye andiko langu la awali ni wapi nimesema kuwa "TAA mpaka CCM iilijaa Waislamu watupu"?Mohammed Said katika kitabu chake cha Abdulwahid Sykes anasema "TANU kuanzia mwanzo kilikuwa ni chama cha Waislamu" unakubaliana naye? - si maneno yangu hayo.
  2. Kwa vile umeweza kuonesha kuwa walikuwepo Wakristu katika TANU kitu ambacho mwanahistoria yeyote wa Tanzania anajua vizuri sana na kutokana na uwepo wake ina maana Mohammed Said amepotosha kwenye kitabu chache. Kama hili ni kweli TANU ilianzishwa kwa ushirikiano sawa wa Wakristu na Waislamu na dini zao hazikuwa sababu ya kujiona kuwa wanamiliki chama kwanini kitabu cha Mohammed Said kinaaminiwa na wapo wanaoamini kuwa ni "Waislamu ndio walioanzisha TANU" wakati kulikuwepo na Wakristu ambao tunawajua "majina na hata idadi yao"?
  3. Kama kuwepo kwa Wakristu ndani ya TANU kunafuta dhana ya TANU kama chama cha Waislamu kitu ambacho nakubaliana nacho (ndio maana nilisema hoja ya kuwa TANU ni chama cha Waislamu haina nguvu pale utakapoingiza Wakristu wake ndani yake) inakuwaje kuwepo kwa Watu wasio Wachagga ndani ya Chadema isivunje hoja ya Chadema kuwa ni chama cha Wachagga?
  4. Sote tunajua vizuri tu kuwa hakuna chama nchini ambacho kimeundwa kikiwa na watu wa dini moja, sehemu moja au kabila moja tu. HAKUNA. Lakini wapo watu walioafanikiwa kuwashawishi watu kwamba kati ya vyama vyote nchini ni Chadema ndicho ni cha "Wachagga, Wakristu na watu wa Kaskazini". Hata hivyo tunajua wapo Waislamu, Wasukumua na Wakerewe, Wahehe na Wangoni n.k na wapo watu wa Kusini (hadi MBozi na Katavi) n.k lakini pamoja na yote hayo kujulikana lakini bado watu wanaamini kuwa Chadema ni chama cha kidini, kikabila na kikanda?
  5. Umehamaki kuona kuwa nimewashambulia Waislamu; hivi unafikiria Wachagga wanajisikiaje wanaponyoshewa kidole na viongozi na wananchi wenzao ? Au mnafikiri Wachagga nao hawana hisia? Mnataka Wachagga wasijiunge na Chadema kwa sababu wakifanya hivyo watakuwa wanaonesha kuwa ni chama chao? Mnataka Wachagga, Wakristu na watu wa Kaskazini wanaotaka kujiunga na Chadema wakataliwe, waliopo wahesabiwe, na wenye nafasi mbalimbali waziachie kama mtu mmoja alivyowahi kupendekeza humu ili kufanya chama kisionekane cha "kikabila, Kikristu na Kikanda?

Kama bado anajilazimisha kutokuelewa akamatwe na ashtakiwe kwa uchochezi.
 
Joshua Arap Sang yupo in Ocampo six.Huyu ni mtangazaji kwa hiyo mwanahabari aliyechochea ghasia after uchaguzi Kenya.

M.M.Mwanakijiji ni mwandishi hivyo mwanahabari kama Joshua Arap Sang .Mwanakijiji mwandishi aliyeelimika na anayeheshimika kwa makala zake sasa anajisogeza kwenye list ya Ocampo (Tanzania 2015).

Nchi inanuka rushwa, CCM ikadhamiria kuwaondoa EL,RA,AC.Hili ni jambo la kheri ila ni M.M.Mwanakijiji aliyeandika makala ya OPERESHENI OKOA MAPACHA akizuia kusafishwa kwa ufisadi nchini.Kwa sasa kasi ya kuvua gamba imepooza au imekufa as Mwanakijiji backfires.

Mwanakijiji amevuka mipaka kwa sasa Mwanakijiji ameanza kuwaaminisha watanzania kuwa CCM ni chama cha Waislam.Akitumia kalamu yake na uhuru amezindua kampeni hii chafu kabisa itakayoliangamiza taifa.
Mwanakijiji ameanza kuwa na falsafa ya tubomoe taifa tutajenga kesho.Mwanakijiji unaushawishi mkubwa kwa makala zako kwa hiyo inakubidi uwe mwanaglifu zaidi unapoandika.
Mwanakiji unauwezo wa kukwepa Ocampo list ya Tz,Usituangamizie taifa tafadhali.

CDM haina udini
CCM haina udini
Mungu ibariki Tanzania
 
We unayejiita Jesuit, eti CCM inawakandamiza waislamu, sasa kama CCM inamilikiwa na waislamu halafu kinawakandamiza waislamu huo ni ushahidi tosha kuwa waislamu hampendani.Waislamu wana hati miliki ya CCM sasa inakuwaje wanawakandamiza waislamu??????????
 
aah
kweli mkuki mtamu kwa ngurume

au mchicha mzuriiiiiii ila umeota chooni (hoja ya udini imetumiwa na CCM kuidhoofisha CDM hoja hii inapotumiwa na Mwanakiji munaanza kuangaika)
 
Wakuu mi napingana na wote wanaosema kuwa Shosi hakuelewa hoja ya MMKJ. Ukweli ni kuwa jamaa kaielewa vizuri sana isipokuwa ameamua kwa makusudi kupotosha kwa sababu anazozijua yeye na pengine tunazoweza kuzihisi. Hakuna mtu asiyejua kuwa huyu ni mmoja wa wapotoshaji wakubwa sana hasa linapokuja suala la imani na pengine chadema.
 
Nitaomba radhi kwa kuanzisha thread mpya ili niweze kupata fursa ya kujibu hoja za ndugu yangu Mimi Mwanakijiji au kama anavyojiita sauti ya kijijini inayoelezea iliyoandikwa kwenye gazeti la Tanzania Daima: Kama CHADEMA ni Wachagga, CCM ya Waislamu? K

Napende niwaeleze wale wote walioshabikia historia ya TANU kuwa wamelishwa "tango pori" na mheshimiwa sana Mwanakijiji japo sijaelewa amefanya kwa makusudi au kwa kutokufahamu kwakuwa tunae humu jamvini ni imani yangu atatueleza na kututanabaisha mapenzi yake juu ya vyama alivyovizungumzia, ila ningependa kumshauri awe mzalendo zaidi na apendelee kuwaelimisha watu kwa historia ya ukweli japo kwa kiwango cha asilimia 80 kama si mia kwa mia.

Pengine ni vyema tuangalie mtiririko wa kupigania uhuru wa nchi hii ili tuone mchango wa Mwanakijiji juu ya hoja yake na tupate kumuenzi kwa kutupa elimu na historia adhimu tusioijua:

1929: TAA yaundwa ikiwa na wajumbe wafuatao:

1. Kleist Sykes, 2. Mzee bin Sudi, 3. Ibrahim Hamis, 4. Zibe Kidasi, 5. Ali Said Mpima, 6. Suleiman Majisu, 7. Raikes Kusi, 8. Rawson Watts, 9. Cecil Matola.

1950: TAA yawasiliana na KAU; Abdulwahid alikwenda Nairobi kukutana na Jomo Kenyatta ili kujenga mawasiliano na chama cha Kenya African Union (KAU).

1951: Kuundwa kwa tawi la siasa la TAA; likiwa na wajumbe wafuatao:

1. Abdulwahid Sykes (Secretary)
2. Sheikh Hassan bin Amir
3. Hamza Kibwana Mwapachu.
4. Said Chaurembo
5. Dk. Kyaruzi.
6. John Rupia.
7. Stephen Mhando

1951: Kenyatta akutana tena na viongozi wa TAA. Safari hii mkutano huo ulifanyika Arusha. Wajumbe wa TAA walikuwa Abdulwahid Kleist Sykes, Dossa Aziz na Stephen Mhando.

1952: Abdulwahid alichaguliwa kuwa Rais wa TAA.

1952: Mwalimu Nyerere atambulishwa kwa Abdulwahid na Bwana Kasela Bantu. Baada ya utambulisho huo ikawa kila Jumamosi Mwalimu Nyerere akawa anakutana na akina Dossa Azizi, Bw. Ally Sykes, Abdulwahid Sykes, Dustan Omar na Mhando kujadili mustakbali wa nchi ya Tanganyika.

Mikutano hiyo ama ilikuwa ikifanyika nyumbani kwa Dossa Azizi mtaa wa Congo au mtaa wa Stanley nyumbani kwa Abdulwahid.

Alikuwa ni Dossa Azizi ambaye mara nyingi alikuwa akimrudisha Mwalimu Nyerere kwa gari lake Pugu (St. Francis College) baada ya mkutano.

1953: Mwalimu achaguliwa kuwa Rais wa TAA. Wazee waliompa nguvu ya kisiasa Mwalimu mara baada ya kuingia katika TAA/TANU.

Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir, Mzee Mohammed Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate na Mwinjuma Mwinyikambi. Wengine walikuwa Rajab Diwani, Makisi Mbwana, Sheikh Haidar Mwinyimvua na Idd Faiz Mafongo. Aidha walikuwepo Idd Tosiri, Sheikh Mohamed Ramia na Mashado Ramadhani Plantan.

Oktoba 10, 1953 Mwalimu Nyerere, Abdulwahid Sykes, Ally Sykes, Dossa Aziz na John Rupia walikutana kujadili namna ya kuibadili TAA kuwa chama kamili cha siasa.

1954: TANU yaanzishwa. Wajumbe wa mkutano uliojadili kuibadili katiba ya TAA kuwa TANU walikuwa Abdulwahid Sykes, Julius Nyerere, Tewa Said Tewa, Dossa Aziz, Ally Sykes, Kasela Bantu, ,

Abubakar Ilanga na Saadan Abdu Kandoro. Wengine walikuwa S.M. Kitwana, C.O. Milinga, Patrick Kunambi, Gerimano Pacha, Japhet Kirilo na L.M. Makaranga. Walikuwa pia Joseph Kimalando na John Rupia.

Mkutano wa kuizindua rasmi TANU ulihudhuriwa na wajumbe wafuatao: Julius Nyerere, Abdulwahid Sykes, Ally Sykes, Dossa Aziz, John Rupia na Mshume Kiyate. Wengine walikuwa Makisi Mbwana, Jumbe Tambaza, Juma Waziri, Clement Mtamila, Rajab Diwani, Schneider Plantan na Marsha Bilali. Walikuwepo pia Rashid Ally Meli, Frederick Njiliwa, Idd Faiz Mafongo, Idd Tulio, Denis Phombeah na wengine.

Napenda kumfahamisha ndugu yangu Mwanakijiji kuwa pia ndani ya TAA na TANU kulikuwa na kina Dr Michael Lugazia, Dr Vedasto Kyaruzi, Dr Luciano Tsere, Dome Budohi, Zuberi Mtemvu, Ali Mwinyi Tambwe, Tatu bint Mzee, Mwinyijuma Mwinyikambi, Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo

Julius Nyerere alipewa kadi ya TANU Na. 1, kadi Na. 2 ikaenda kwa Ally Sykes na Abdulwahid akachukua kadi ya TANU Na. 3, Dossa Azizi alichukua kadi Na. 4, kadi Na. 5 ikaenda kwa Phombeah. Dome Okochi alipata kadi Na. 6, John Rupia Na. 7, Bibi Titi Mohamed kadi Na. 16 na Idd Tosiri kadi Na. 25.

Ndugu yangu Mwanakijiji,

Kwa watu makini makala yako ni moja ya utumiaji kalamu kupotosha jamii makala yako imebaka historia ya kweli ya TAA/TANU na sasa CCM kama nilivyoeleza mwanzo pengine mapenzi ya chama kimoja wapo ndio mapenzi hayo yamekusukuma kuinanga historia ya kweli.

Ni matumaini yangu ipo siku utaungana na Joseph Mihagwa utajitolea kuuvunjaa mwiko wa kuuzungumzia muungano inavyostahili.

Shukrani sana na nakutakia siku njema wewe na jamaa wote wa JF.

Mohammed Shossi.


Ndugu yangu Mohammed Shossi,
Nadhani hukuisoma vizuri ile makala ya MwanaKijiji ukaielewa.
MwnaKJJ aliomit kwa makusudi role ya wakristo katika utendaji wa TAA, TANU hadi CCM kwa minajiili ile ile CCM inavyo omit role za makabila mengine kwenye CHADEMA na ku generalize kwamba CHADEMA ni chama cha KICHAGA. Na ndiyo maana wakati anahalalisha hoja wana CCM kwamba CHADEMA ni cha kichaga MWANAKIJIJI hakuandika role za Makibal mengine mfano kina Bob Makani na wengine.

Kama unataka kurudisha role za wakristo katika harakati za TAA hadi CCM ni lazima na wewe urudishe role za makabila mengine ndani ya CHADEMA ili turudi kwenye line ya usawa na tuweze kujadili hii hoja ya Uchanga CHADEMA na Uislam CCM.

Na kwa msingi huo utakuwa umetusaidia sana kujipinga wewe (labda kama ni mwana CCM) na wana CCM wengine juu ya Propaganda wanazozieneza nchini kwamba CHADEMA cha Wachaga.
 
Ni vigumu kumuelewa Mwanakijiji kwakua ni mtu mwenye upeo mkubwa lakini ana chuki kubwa zaidi na uislam na waislam na uzuri wake hafichi hilo.
Kama vile ilivongumu ngamia kupita kwenye tundu la sindano ni ngumu sana waliojifungia ndani ya ngome ya dini kutoka nje ngome (out of the box) ili kuona ukweli wa mambo huko nje tofauti na uongo au upotoshaji kule ndani. Inategemea dini yako ina ukuta kiasi gani kukuzuia usione yaliyoko nje. Kuna dini zina kuta za mawe, zingine tofali na zingine zina wavu tu za chuma hivo kuona pande zote na kuweka mambo na ubongo wako sawa, ni rahisi.
Watu walioko kwenye kuta za mawe siku zote ni wabishi na hawajui hata pale wanapokosea wanadhani wao ndo wako sahihi. Huona watu wengine kuwa wanakosea na pale watu wanapowashangaa kwa huo msimamo usioendana na ukweli wowote hudhani kuwa watu wanachukia dini yao hiyo kumbe tatizo ni ukuta wa mawe usioruhusu ubongo kuona mambo zaidi ya yale yaliyomo ndani ya kuta za dini zao.
 
mimi sijaona udini wa Tanzania daima.
Hapa watu wanafura kisa Mwanakijiji kaonesha ni kivipi CCM ni ya waislamu WHERE AS cdm NI WACHAGGA

ccm wameudhuka sana na makala hii.
 
Back
Top Bottom