Mwanakijiji aibuliwa jambo MICHUZI blog

Status
Not open for further replies.

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
fitna iko hapa:

issamichuzi.blogspot.com/

michuzi Blog said:
salamu toka bongocelebrity.com

wadau kunradhi,

leo nimepokea ujumbe maridhawa toka bongocelebrity.com ambao mhusika alisita kuutundika na badala yake kaamua kunitumia kwanza kuulizia kama autundike ama la. mie sio tu nimemruhusu autundike kama ulivyo bali pia nimeuweka hapa pia ili aliyeandika apate kuridhika na roho yake. Ila tatizo kaandika kama ni kwa niaba ya wadau wote na si yeye binafsi. Je ni kweli anawasemea enyi wadau wote wa globu hii ya jamii?

Hii ni hoja ambayo kama anavyosema mwandishi itabidi ijibiwe kwa hoja, hasa ukizingatia kwamba mtu kama yeye hata kama kaandika kwa nia ya kujeruhi watu anataka lazima hoja yake iwekwe hewani huku hashangai kuona wenzie ambao ni wastaarabu hawawekewi ribiti. Na je, kuna ubaya gani kuwa tarishi wa mdau kama mwanakijiji ambaye, kama wanvyofanya wadau wengine, hupenda kutumia globu hii kupitishia ujumbe wao kama mdau yeyote yule?

Namsihi mwandishi huyo kwamba endapom kama ana matatizo na wadau wa globu hii ya jamii asinishirikishe kwenye ugomvi wake kwa njia yoyote ile, maana ukisoma katikati ya mistari utaona dhahiri hana nia njema na mwanakijiji ambaye si mdau pekee anayepitishia ujumbe wake humu mara kwa mara. kwa kifupi wadau, nikiwa mtumishi wenu ama tarishi ambaye hauwawigi, mna maoni gani juu ya maoni ya huyu mdau ambaye hata jina kalificha wakati yeye mwenyewe ni hodari kutaja ya wenzie?
kwa upande wangu hii ni moja ya changamoto nyingi nilizokumbana nazo muda wote toka niende hewani na kwa taarifa yako mwandishi hivi ndivyo vitu vinavyonitia moyo na si kunivunja, kwani naelewa fika kwamba 'kizuri kwa bata mzinga, ni kibaya kwa kuku' na sio rahisi kumridhisha kila mtu hata uweje!

ujumbe wa huyo mdau ni kama ufuatavyo:

MICHUZI USITUMINYIE 2008 VINGINEVYO TUTAHAMA !

Kama kawa Issa Michuzi amechemsha huko kwenye blogu yake mpaka akatupiwa taulo eti alidhani Boxing Day inahusiana na masumbwi akakurupuka na kuandika habari za Japhet ambaye ubingwa wake wa Dunia haupo popote katika rekodi za dunia.

Tunamuelewa sana Michuzi anapotumia tungo kama mai hasband wako na majina kama ukerewe, A-town, n.k Lakini kwa hili si utani wala hasijifanye kuwa alikuwa anachekesha maana huwezi kuweka post nzima na picha ya watu kwa utani.

Michuzi Jr mtupie taulo huko ndugu yetu kwenye hii link:http://issamichuzi.blogspot.com/2007/12/boxing-dei.html#comments

La pili ni kuwa Michuzi (senior) ambaye ndiye huwa anamtumia taarifa zote Mzee Mwanakijiji wa USA (Mpelelezi) ana utofauti mkubwa sana na Michuzi (Junior) ndio maana wengine tumeamua kuhamia huku kuliko kwenye blogu yake ambayo ana amua bila sababu kuzuia comments za watu na wakati hujaandika matuzsi yeyote kama nilivyoandika sasa.
Michuzi (senior) inabidi ukue kiuandishi, hoja zijibiwe kwa hoja na siyo kumminyia mtu comments zake. Hapa sina haja ya kuomba eti haya niliyoyaandika yawekwe ni dhahiri yanawekwa maana ni kwa ajili ya kuboresha namna ya kuhabarisha watu na pia sijaandika tusi lolote.

Kama nimeongea vibaya naomba msamaha na nisahihishwe hapa hapa.N.B nendeni jambo forums muone jinsi ambavyo huyo mzee Mwanakijiji pamoja na mazuri yake mengi amejikweza kiasi mpaka anaonekana kuwa yeye ndiye chanzo cha habari zoooote na kwamba yeye hasahihishwi na pia kuwa anajua kila kitu cha fani zote ulimwenguni kuanzia uvuvi wa dagaa mwanza hadi ubunge hadi thesis defence hadi mapenzi ya mfano hadi hard science fiction! Hadi Leo yeye anajiita mpinzani wa kweli lakini utambulisho wake haujulikani na kuna mtu aliandika hapa mambo yake lakini yeye akatetewa kuwa hana haja ya kujibu wakati motto yake at KLH News ni kuwa kila kitu kinazungumzika na hoja hujibiwa kwa hoja. Mimi napenda kusoma na kujifunza mambo ambayo wengine huandika lakini sipendi mtu anapojinyanyua mpaka karibu kujivika uungu mdogo katika fani ya uandishi.

Samahani kwa kuwapotezea muda wakati wa siku ya kupeana zawadi.
 
Man...people should get a life!! Kila siku Mwanakijiji this Mwanakijiji that...why?
 
Man...people should get a life!! Kila siku Mwanakijiji this Mwanakijiji that...why?
sipendi kuingia katika mijadala ya personal life kama hii ,lakini kwa vile suali lako liko simple nimeona nilijibu.umejaribu kujiuliza kwanini watu hao hao hawajasema nyani ngabu is this nyani ngabu is that....why???
NB:hili ni suali tu kwa nyani ngabu na halihusiani kabisa na uoni wangu kwa mheshimiwa mwanakijiji.ahsanteni. am out of topic
 
Huyo mwandishi nadhani anachuki binafsi na Mkijiji, na kama anadhaoni kwa kuandika hivo ana mmaliza, ajue anajipiga bao la kisigino kwa kuzidi kumtangaza na kumnyanyua, kwani kwa jinsi habari yenyewe ilivo kaa tenge, kila atakaye isoma atapenda kutafuta kujua zaidi juu ya Mkiji, sasa hapo.....

Ndipo katika harakati hizo atakapo jikuta naye anaungana naye kumkoma nyani bila kupenda!
 
... because they 'love, fear and loathe' him but are nitwitted and scared!!

Umenikumbusha, Hunter Thompson, author wa fear and loathing in las vegas na fear and loathing in '76 campaign trail.......

hao wakina buguruni ni "ma-intateina!!!.
 
sipendi kuingia katika mijadala ya personal life kama hii ,lakini kwa vile suali lako liko simple nimeona nilijibu.umejaribu kujiuliza kwanini watu hao hao hawajasema nyani ngabu is this nyani ngabu is that....why???
NB:hili ni suali tu kwa nyani ngabu na halihusiani kabisa na uoni wangu kwa mheshimiwa mwanakijiji.ahsanteni. am out of topic

Nimeuliza hivyo kwa sababu sijaona chochote kilicho na substance kilichoandikwa. Nilichoweza kung'amua ni mashambulizi na upakwaji matope dhidi ya Mwanakijiji. Listen here youngin..I pick on him too...but I do it in the spirit of having fun...nothing more..nothing less. So why not Nyani Ngabu this Nyani Ngabu that...well...I dunno. But what I know is if you want to go after Mwanakijiji...go after his works (writings) or whatever he does. What is going after Mwanakijiji..(a fictional character/ figure) gonna do for you? What do you gain from it? How can you attack and mudsling a fictional figure? I'm sorry...but that's retarded.
 
Mtu yeyote anayeanza kwa kuomba msamaha in the timid fashion ya "Kama nimekosea naomba msamaha in advance" halafu "blah blah blah" haifai kupoteza muda kumsoma au kumsikiliza kwani yeye mwenyewe hana uhakika na asemacho, seuze sisi wasomaji?

Kama unajijua unakosea fanya marekebisho halafu njoo na nondo nzito, sio kuleta weak apologist's notions.Watu tunamkoma nyani hatuna muda na apologists speculations na smear campaign.

If this was an attempt at "eminent criticism" au disguised and fake "humility" the author should seek further enlightenment on the subjects before touching the keyboard.As Churchill had it, his fake modesty reveals much to be modest about.
 
Rebugiri,
maneno yako kweli maanake huko KLH naona watu ndio kwanza wanazidi kuingia tena wengine wameniuliza huyu Mwanakijiji ndio nani na blog yak inapatikana vipi?..
Kudos mwanakijiji bao hilo la kisigino umecheza kama Zitto vile!
 
Wabongo bana,kuna mambo kibao ya kujadili lakini naona kila wakati ni personal issues tu.Kuwa mpelelezi si kazi kama kubeba box,kachagua kuwa sasa inauma nini.Kwanza mie nashangaa sana eti usalama wa taifa.Inaonekana mtu akiwa usalama basi ndio kapata tiketi ya kufika mbinguni.

Masuala kama ya haya niya kipuuzi sana hayafai kujadiliwa huku taifa linanuka kwa rushwa,ufisadi,umasikini na magonjwa.

Yaani mtu mzima anakaa mbele ya PC yake na kubofya bofya keybord maandishi lukuki dhidi ya Mkjj.Shame on him.Mimi nafikiri watu sasa tubadilike,ndio maana hapa tunatumia nicks name la sivyo......inachosha
 
Bugurumu kaingia mitini, hamtamwona tena mpaka atakapozichanga na kupata kiburi cha kutinga kwenye internet cafe............kama alivyosema Nyani Ngabu, hata mie huwa na attack baadhi ya hoja za mkjj. Mara nyingi huwa ni tofauti za kimitazamo(mfano kambona na nyerere) au kumfanya aweze ku-refine na kuwa better zaidi.........yeye anajua kuwa hatuendi personal hapa JF. lakini ku-attack mkjj kama mkjj ni kichaa!!
 
Bugurumu kaingia mitini, hamtamwona tena mpaka atakapozichanga na kupata kiburi cha kutinga kwenye internet cafe............kama alivyosema Nyani Ngabu, hata mie huwa na attack baadhi ya hoja za mkjj. Mara nyingi huwa ni tofauti za kimitazamo(mfano kambona na nyerere) au kumfanya aweze ku-refine na kuwa better zaidi.........yeye anajua kuwa hatuendi personal hapa JF. lakini ku-attack mkjj kama mkjj ni kichaa!!

Ha ha haaaaaaaaa.................... usituchekeshe hapa unafikiri Bugurunikwamnyamani hayupo online, think twice yupo hapa amejaa kama pishi la udaga. Yeye ameweka hii message kama vile imetoka: salamu toka www.bongocelebrity.com lazima ufahamu calibre ya mtu mwenyewe kwanza. Wako hapa wanaoangalia hoja na wanaopiga debe kwa MAFISADI wao. Kwa hiyo ni jukumu lako kuchambua mchele.
 
Tatizo letu wabongo CCM imetufikisha mahala ambapo hatuamini kama mtu anaweza akafanya jambo kwa manufaa ya wengine. Kwa hiyo kila kitu kizuri ambacho tunachoona mtu anafanya tunafikiri anataka kitu fulani binafsi. Ndio maana akina mwanakijiji walioamua kufanya mambo kwa ajili ya jamii na sio lazima wao binafsi wafaidi, watatundikwa majina sana tu, lakini go ahead MKJJ, at the end of the day the truth will stand out tall, visibly and clearly.
 
Folks, remember even when Mandela was fighting against apartheid, he was labelled as ''terrorist Number one'' and a threat to the entire universe. Can Mwkjj be exceptional??
 
yaani mie huwa nachekaga saana badala ya kujadili mambo ya maana kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu na sie kwa ujumla twaanza chokonoana personal maisha yetu n then twaanza ongelea hayo kama wat we are doin right now!sijui ni lini tutafika!
anyways ndugu Mwanakijiji la msingi don care abt wat pipo say abt u songa mbele tu muzeee!!na nakupongeza kwa watu kukutangazia biashara yako ya ur points na blog yako as si mchuzi watu kibao now wanakuulizia angalau wakujue yaani bonge la ku boostiwa u famous wako halafu bureee bila hata ya kulipia
 
Hao wana yao na Mwanakijiji. Ukiona watu wanaanza kubwabwaya hivyo jua wameshindwa kupambana kwa hoja na sasa wanaanza kumpakazia Mwanakijiji bila sababu.

Mwanakijiji wewe endelea na mapambano na tunategemea mwaka 2008 uwe na mafanikio makubwa katika kuwagusa hawa waheshimiwa pale pasipogusika.

Wameona hapa JF propaganda zao zimeshindwa na sasa wanaanza kuhamia kwenye vijiwe mbalimbali ili kujaribu kumchafua Mwanakijiji.

Mwanakijiji ana mazuri yake mengi sana na yale mabaya machache tunakosoana hapa hapa kama vile ambavyo mabaya yetu sisi wengine pia yanakosolewa hapa JF.

Hongera Mwanakijiji, kwa mwaka 2007 umekuwa kinara wa JF na michango yako imesaidia kukuza hiki kijiwe chetu. Tuendelee kumkoma Nyani Giladi, hata akimbilie kwenye miti, sisi tumo tu na mwaka 2008 yatakuwa makubwa zaidi.
 
nilisema awe low profile hakusikia, mengine haya ya kujitakia. Punguza mwendo kidogo.

Atapunguza mwendo ili iweje? Ili akina Lowassa waendelee kufaidi kasungura kao?

Inabidi mwaka 2008 kuongeza mapambano, si unaona sasa mpaka Maaskofu wameamka na kuingia kwenye mapambano ya hawa mafisadi?
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom