MwanaJF mwenzetu aliyefariki kwenye ajali ya Ndege, Nelson Olotu apumzike kwa amani

Habari zenu nyote...! Rest In Peace Nelson Olotu.


Napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole familia ya Mzee Olotu iliyopoteza kijana wao mpendwa kwenye ajali ya ndege iliyotokea hivi majuzi hapa. Poleni sana wafiwa kwa kumpoteza ndugu yetu Nelson.


Lakini pia Nelson alikuwa ni mmoja kati ya mwanajamii mwenzetu hapa JamiiForums tangu mwaka 2013, hivyo basi wanajamii tunasikitika kumpoteza member mwenzetu akiwa bado anahitajika kwa kiasi kikubwa kabisa katika jamii yetu hii.


Nikiwa kama member mwenzake nachukua nafasi hii kwa niaba ya Uongozi mzima wa JamiiForums na kwa niaba ya members wote wa JF kutoa pole kwa familia ya wafiwa na tunawaombea MUNGU awatie nguvu sana katika kipindi hiki kigumu cha msiba. AMEN.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA. JINA LA BWANA LIHIMIDIWE. MUNGU AKULAZE MAHALI PEMA NDUGU YETU NELSON OLOTU. AMEN.

Pia soma


olotu huyu ndio yule mwenye maduka hapa uhuru road
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom