Kichwa Kichafu
JF-Expert Member
- Apr 13, 2017
- 44,565
- 188,766
Habari za mihangaiko.
Mazingira yoyote yale unapokuwepo binadamu unaweza kupata kitu chochote chanya (Faida) au hasi (Hasara).
Hapa twende moja kwa moja mfano, hapa JamiiForums kuna watu wa tofauti tofauti sana na wana mitazamo mbalimbali.
Wewe unapoingia humu kuwa na lengo hata moja tu la kupata kitu kipya chenye mantiki. Unakuta mtu anasema "walahi Jf sihami" ukifuatilia nini kinamfanya aseme hivi? Unakuta kuona kumbe ni umbea /member aliyejitoa ufahamu kuandika upumbafu/ nk.
Ila kwa makini angetulia na kutafakari kuna majukwaa mangapi humu Jf angeweza kupata tip hata moja mpya mfano kama ni mfanyabiashara angepata mawazo mengine mengi mapya toka humu.
Kuna vijana kabla ya kuingia Jf labda alikuwa vizuri kwenye programming ila kaingia huku kasombwa na upepo wa MMU anasahau kujifunza kitu kipya wakati kuna mambo mazuri sana Jukwaa la Science & Tech.
Mara nyingi ukitumia muda mwingi kwenye mambo yasiyo ya msingi akili yako itawaza hayo hayo.
Mtu anabaki kushangaa kwanini huyu member yupo vizuri kwenye haya masuala? Jibu wakati alipokuwa kama wewe alijifunza. Wewe wakati huu unafanya nini?
Kuna majukwaa mengi sana jaribu kutumia hata dakika 15 kila siku kupata kitu kipya then endelea na huko unaposema una-refresh.
Humu ndani wakati huu unaweza kujifunza bure kabisa ila baadae maarifa hayo watu watakuja nunua kutoka kwako.
Nawasilisha.
Siku njema!
Cc. Kichwa kichafu
Mazingira yoyote yale unapokuwepo binadamu unaweza kupata kitu chochote chanya (Faida) au hasi (Hasara).
Hapa twende moja kwa moja mfano, hapa JamiiForums kuna watu wa tofauti tofauti sana na wana mitazamo mbalimbali.
Wewe unapoingia humu kuwa na lengo hata moja tu la kupata kitu kipya chenye mantiki. Unakuta mtu anasema "walahi Jf sihami" ukifuatilia nini kinamfanya aseme hivi? Unakuta kuona kumbe ni umbea /member aliyejitoa ufahamu kuandika upumbafu/ nk.
Ila kwa makini angetulia na kutafakari kuna majukwaa mangapi humu Jf angeweza kupata tip hata moja mpya mfano kama ni mfanyabiashara angepata mawazo mengine mengi mapya toka humu.
Kuna vijana kabla ya kuingia Jf labda alikuwa vizuri kwenye programming ila kaingia huku kasombwa na upepo wa MMU anasahau kujifunza kitu kipya wakati kuna mambo mazuri sana Jukwaa la Science & Tech.
Mara nyingi ukitumia muda mwingi kwenye mambo yasiyo ya msingi akili yako itawaza hayo hayo.
Mtu anabaki kushangaa kwanini huyu member yupo vizuri kwenye haya masuala? Jibu wakati alipokuwa kama wewe alijifunza. Wewe wakati huu unafanya nini?
Kuna majukwaa mengi sana jaribu kutumia hata dakika 15 kila siku kupata kitu kipya then endelea na huko unaposema una-refresh.
Humu ndani wakati huu unaweza kujifunza bure kabisa ila baadae maarifa hayo watu watakuja nunua kutoka kwako.
Nawasilisha.
Siku njema!
Cc. Kichwa kichafu