Mwanajeshi wa Israel afukuzwa kazi baada ya kukataa kumuua mtoto wa kipalestina

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,991
17,888
Jeshi la utawala wa Kizayuni limemfukuza mwanajeshi mmoja aliyekataa kumpiga risasi binti wa Kipalestina aliye na umri wa miaka 16 kwa jina la Nauf Infiat.
Katika tukio hilo ambalo lilijiri mwanzoni mwa mwezi huu katika lango la kuingilia katika kitongoji cha Wazayuni kwa jina la Mevou Dotan huko katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, mwanajeshi huyo wa Kizayuni aliyefukuzwa jeshini hakuwa tayari kummiminia risasi binti huyo wa Kipalestina, ambapo mwanajeshi mwingine alimpiga risasi binti huyo na kumjeruhi vikali na hatimaye binti huyo kuaga dunia siku moja baadaye.
Baada ya kumchunguza mwanajeshi huyo aliyekataa kumpiga risasi binti wa Kipalestina, jeshi la Israel lilisema kuwa mwanajeshi huyo hakuonyesha radiamali inayofaa mkabala na binti huyo wa Kipalestina. Jeshi hilo limedai kuwa, binti huyo wa Kipalestina alikuwa na lengo la kumshambulia mwanajeshi Mzayuni katika lango la kuingilia katika kitongoji cha walowezi wa Kiyahudi cha Mevo Dotan. Hadi kufikia sasa, Wapalestina zaidi ya 300 wameuawa shahidi na wengine wengi wametiwa mbaroni na wanajeshi wa Israel tangu kuanza Intifadha ya Quds mwezi Oktoba mwaka 2015.
Parstoday.com
 
Wewe Utakuwa Muislamu Tu
Ulitaka awe mkristo au mpagani israel ni taifa la kishetani kazi kuuwa watu wasio na hatia ingekuwa ISIS wamefanya hayo ungesikia kelele nyingi kana kwamba damu ya waislam ni haki kumwaga ya wengine ndio ugaidi hamna haki duniani ila ipo siku dunia yote mnayoringia itaangamizwa hakuna kitakachobaki sio trump wala netanyahu pale haki itakaposimama
 
Hawa jamaa ni wabanguzi halafu umoja wa mataifa upo tu kimya... Yaani Israel ina idadi ndogo ya raia lakini ndiyo wanao i control hii dunia... Yaani hamna nchi yoyote ile inayo weza kuwaambia kitu... Wapo juu ya sheria
 
Mimi naunga mkono Israel kuuwa wapalestina wanaojifanya wanavurugu, wapalestina wanapandishwa mizuka ya hasira na wachache alafu wanaishia kuuwawa.....mtu silaha huna alafu unataka kupigana ma mtu mwenye AK47
 
Ni sahihi kabisa; huyo mwanajeshi ni mjinga. Madhara ambayo huyo binti angesababisha ni makubwa kuliko kummalizia mbali huyo binti. Hamas (and other terrorist groups - Boko Haram and the like) wamekuwa na tabia ya kuwatumia vibinti kama hao kufanya mashambulizi ya kujilipua.
 
Mimi naunga mkono Israel kuuwa wapalestina wanaojifanya wanavurugu, wapalestina wanapandishwa mizuka ya hasira na wachache alafu wanaishia kuuwawa.....mtu silaha huna alafu unataka kupigana ma mtu mwenye AK47
Fikiria umenunua kiwanja, then jirani uliyepakana nae anaongeza mpaka wake ndani ya eneo lako, will you sit and do nothing?
 
Huwa nawashangaa sana waTz walokole wanaowashobokea waisrael wakat hata waisrael wenyw wanaupinga ukristo wako busy na dini yao. Get out of the box waisrael wasasa sio wale wahayudi wa Musa.
hahahah! utakuta kanisani kuna bendera ya zion/Israel wakifikiri Mwenyezi Mungu anashawika kwa bendera ya wayahudi kanisani, huo ni upotevu wa walokole wengi.
 
hahahah! utakuta kanisani kuna bendera ya zion/Israel wakifikiri Mwenyezi Mungu anashawika kwa bendera ya wayahudi kanisani, huo ni upotevu wa walokole wengi.
Misukule na uhaba wa elimu ya dini mtu kafeli form four hajaenda hata chuo cha kusomea bible hajui A wala z anajita nabii anaajifanya anaponya uwezo wake wa kufikiri ni zero anajaza mazombi anawaita kondoo wake kaz inaanza kama mtu unabishia angalia tu channel ten utaona jinsi watu wanavopiga pesa kizembe kwa misukule. Angalia waroma kwa kua mapadri wamesoma na wanawajua vzr wanaojiita wanaisrael wa kileo uone kama ataishobokea hyo nchi inayoongoza kwa kua na gays weng ulimwenguni afu unakuta mbongo kashika bendera ya Israel anaibusu et taifa teule cjui watu wa pepon nan kakwambia jews waliopo Israel ndo wale waliookolewa na Mussa hawa jamaa wameenda Palestine mwaka 1945 juz tuu kuanzisha nchi na mussa ni wa miaka maelfu ilopita ssa unakuaje na uhakika kama ndo ile specie ya kipind kile. Unatakiwa kwanza uwe zombi na mzito kufikiri ndo utakua m........
 
Back
Top Bottom