Is this what you guys mean by "Kubenea kanunuliwa? Tafakari! Rostam Aziz anacheza kama Pele | Gazeti la MwanaHalisi
We ndio humjui Said kweli kweli na kama anakutumia basi anakutumia vibaya, Kubenea unaweza kumtenganisha na Mengi wakati kila siku anashinda kwa Mengi na hata hizo safari za kwenda kutibu hilo jicho lake ni nani anaemfadhili amekwambia?Nimewasoma wote watatu - anayejiita Mtanzania Huru, Mojo na Ngao One. Nawafahamu. Ninachosikitika ni kwamba hamumfahamu Kubenea. Huyu jamaa ni chuma cha pua. Si kweli kwamba Kubenea analipiwa safari zake za India na serikali ya Rais Jakaya Kikwete. Hili naweza kulithibitisha . Muache kucahfaua watu kwa hisia.
Kuhusu Kubenea kufadhiriwa na Mengi na sasa urafiki wa Mengi na Kubenea umekufa, na kwamba wakati wowote anaweza kumuandika Mengi, nadhani ninyi hamumfahamu vizuri huyu kamanda. Kubenea hana rafiki na yeyote ambaye anatia ulimi puani. Nani asiyejua kwamba Mengi anamtetea Kikwete, kwamba hahusiki na ufisadi wakati huohuo anasema nchi imejaa mafisadi?
Inawezekana kweli kwamba Kubenea haheshimiki na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari hapa nchini. Lakini kwangui mimi kutoheshimika kwake kunatokana na husda waliyonayo baadhi ya watu kwa kumuona Kubenea amepiga hatua kubwa ya kumiliki gazeti lake yeye mwenyewe.
Kuhusu hili la kumwagiwa tindikari kwa kuwa alikuwa na mke wa mtu, hizo ni poropaganda za wale waliotumwa kumdhuru. Tunawajua hata kwa majina.
Is this what you guys mean by "Kubenea kanunuliwa? Tafakari! Rostam Aziz anacheza kama Pele | Gazeti la MwanaHalisi
Mkurupukaji mungine huyu,mzee unamjua huyo Nyaronyo Kicheere alieandika hiyo habari ya ROSTAM anacheza kama Pele???au umekurupuka tu!kwa taarifa yako huyo sio kubenea,huyo ni mwandishi wa habari nguli ambae kwa muda mrefu amekua kwenye vyombo vya habari vya mengi akiwahi pia kuwa mwanasheria wa mengi na katika uchaguzi uliopita aligombea ubunge wa tarime nadhani kwa tiketi ya nccr sikumbuki sawasawa kwa taarifa za nyongeza amewahi kujaribu kusomea upadri sitaki kuingia sana ndani hapa,ila tu hiyo story hajaandika kubenea na hawezi tena kuandika hivyo,kubenea katiwa mfukoni wadau sisi ni marafiki tunamjua anatujua na wala hatukukutana nae barabarani kama anavopenda kusema mkubwa mmoja hapa nchini,saidi awadanganye nyinyi msiomjua,mimi sitaki kuwaita misukule ila maamuma.Hata kama anapenda said hawezi na hana ubavu tena wa kuwaandika vibaya mabwana zake wapya Lowassa na Rostam,tatizo hapa jf watu wakimpenda mtu hata uwaeleze nini huwa hawaelewi mpaka yawakute mfano mzuri ni zitto kabwe alipoanza kutoka nje ya mstari,kuna watu tulikua wa mwanzo mwanzo kumshtukia tuliposema hapa tulizomewa ile mbaya lakini baadae alipokuja kutoa makucha ndio watu wakaanza kushtuka too late zitto harekebishiki tena tunaishia kumbembeleza tu cha kumfanya hatuna,ndio huyu kubenea wenu sasa mtamjua vizuri tu huko mbele
Nachelea kusema huna akili timamuSitta pamoja na matatizo yake chungu nzima, lakini pale anaposimama kutetea maslahi ya nchi kwa mfano kupinga malipo fisadi ya sh 113 billioni kwa Dowans basi Watanzania wote tunabidi tumuunge mkono pamoja na kujua kwamba Sitta si safi. Kumbukeni umoja ni nguvu ni utengano ni udhaifu. Sijamsikia hata siku moja Kikwete, Pinda, Pinda au Lowassa wakisimama hadharani na kumuita Sitta ni mnafiki maana hawana ubavu wa kufanya hivyo ila wameamua kuwatumia vibaraka vyao kumshambulia Sitta ambaye ameamua kusimama kidete katika kuipinga Dowans.
Hata kama aliyeandika stori ya Rostam anacheza kama pele, siyo Kubenea, lakini gazeti la MwanaHALISI ni la Kubenea. Anayepitisha hizo makala na sdtori, ni Kubenea. Anayelipa waandishi wanaoandika ni yeye. Sasa nami nimeitafuta stori hii imeandikwa na Kubenea mwenyewe, Juni mwaka huu. Soma kisha wewe na Sitta wakp mthibitishe kwamba huyu jamaa amenunuliwa. Tatizo lenu mnataka kila kukicha amuandike Lowassa hata kama hajafanya jambo lolote.
Endelea Kubenea kafanye kazi ya kukomboa taifa achana na makuwadi wa Sitta, Nape na Mwakyembe.
Hahahaaa... Nimeipenda hii..magamba ndani ya ccm yako ya aina mbili njano na kijani ila yote ni magamba tu, na sasa wantumia nyumdo kupigania vichwani na jembe kizikzna ardhini Sitta ni walewale ambao wameifikisha nchi hii hapa
Nimezipenda hizo data na jinsi ulivyozitumia kuwakilisha ujumbe wako.Nachelea kusema huna akili timamu
Ikiwa SITTA ndiye aliyeuzima mjadala wa Dowans BUNGENI leo tumwamini vipi anapopinga malipo ya Dowans???
Ni SITTA aliyeunga POSHO bungeni kwa kuwaita wanaozikaa ni wanafiki-Ikiwa SITTA ana huruma na wanainchi kwa nini asingeunga mkono hoja ya kukataliwa POSHO ili bili 900 ziingie kwenye kusaidia jamii???
SITTA ni mnafiki sana
Nimezipenda hizo data na jinsi ulivyozitumia kuwakilisha ujumbe wako.Nachelea kusema huna akili timamu
Ikiwa SITTA ndiye aliyeuzima mjadala wa Dowans BUNGENI leo tumwamini vipi anapopinga malipo ya Dowans???
Ni SITTA aliyeunga POSHO bungeni kwa kuwaita wanaozikaa ni wanafiki-Ikiwa SITTA ana huruma na wanainchi kwa nini asingeunga mkono hoja ya kukataliwa POSHO ili bili 900 ziingie kwenye kusaidia jamii???
SITTA ni mnafiki sana
Hahahaaa... Nimeipenda hii..magamba ndani ya ccm yako ya aina mbili njano na kijani ila yote ni magamba tu, na sasa wantumia nyumdo kupigania vichwani na jembe kizikzna ardhini Sitta ni walewale ambao wameifikisha nchi hii hapa