Ndugu wana jamii, katika sakata la mwanaharakati msemakweli kumlipua Manji dhidi ya wizi wa fedha za umma, manji amejibu mapigo kwa kufungua kesi dhidi ya mwanaharakati msemakweli, akimwunganisha Mengi kwenye kesi hiyo.
Nimebahatika kupata nakara ambayo nime attach lengo wote tupate habari.
Baada ya kufanikiwa kupata uamuzi wa mahakama ya Temeke kuzuia Mwanahalisi lisimuandike na kubenea kukabidhi nyaraka zote kumhusu, Manji sasa amepata uamuzi wa mahakama ya kinondoni kuzuia raia mwema lisimuandike na kuzuia raia mwema na marafiki zake kutoandika wala kutoweka ktk mitandao habari zozote kuhusu Kagoda na Manji. Pia imefahamika kwamba ameshafanikiwa toka Julai 2001 kupata hukumu Mahakama ya kinondoni kuzuia magazeti yanayotolewa na Mwananchi Communication ya Mwananchi na Citizen kumuandika kuhusu jambo lolote bila kibali chake. Pia kesho anataka mahakama ya kinondoni izuie Tanzania Daima lisimuandike. Tayari Manji amekwama kumzuia Mengi, Msemakweli na wengine kumuandika ama kumsema. Manji amefungua kesi mbili tofauti zinazofanana mahakama kuu na zote anataka kuzuia uhuru wa habari kwa kutaka mitandao yote (Ikiwamo JF) izuiwe kumuandika na itoe habari zake zote haraka iwezekanavyo na wote wenye uhusiano na aliowashitaki kisiasa, kijamii na kibiashara kuzuiwa nao kumsema kwa njia yoyote.
Zaidi, angalia attached images chini
Nimebahatika kupata nakara ambayo nime attach lengo wote tupate habari.
.Mfanyabiashara Yusuf Manji, anachotaka ni kuwafunga midomo watu wanane na mitandao yote kuzungumzia kuhusika kwake na wizi wa kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, baada ya Jaji Kiongozi Fakihi Jundu kusita hata kupangia tarehe maombi ya mfanyabiashara huyo mtata ya kutaka asikilizwe pekee mahakamani.
Katika maombi yake mahakamani aliyowasilisha mahakamani Alhamisi Septemba 8, 2011, Manji alitaka kufungwa midomo kwa watu wanane wakiwamo Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, Mwanaharakati, Kainerugaba Msemakweli, waandishi wa habari Saed Kubenea na Islam Mbarak.
Hata hivyo, jalada la kesi hiyo namba 135 ya 2011, lilipofika kwa Jaji Jundu, halikupangiwa tarehe ya kusikilizwa, jambo ambalo lilikwamisha mpango wa Manji kuzima kabisa kuzungumzwa kwa Kagoda hadharani na mtu yeyote.
Wengine ambao Manji alitaka mahakama iwazuie kuzungumza lolote kumhusu hata bila upande wa pili kusikilizwa (Ex-Parte) ni Sabas Kiwango, Silvanus Chingota na Zuberi Kiponda.
Manji katika maombi yake hayo ambayo pia anaishitaki Kagoda, anaiomba mahakama bila kusikiliza upande wowote kuamuru maandiko yote yaliyopo katika mitandao ya intaneti, blogs na tovuti kuondolewa mara moja na kuzuiwa mitandao yote kuzungumzia lolote kumhusu bila ya yeye kutoa kibali cha maandishi.
Pamoja na kuzuia na kutaka mahakama iamuru taarifa zote katika mitandao zinazomhusu ziondolewe na mtu yeyote asiweke katika mtandao taarifa zake, Manji pia ametaka mahakama iamuru watu wote wanane aliowalalamikia na washirika wao kukabidhi nyaraka zote walizonazo zinazomhusu, makabidhiano ambayo anataka yaambatane na kiapo.
Manji pia anataka pia mahakama iwazuie watu aliowalalamikia wazuiwe kufanya mawasiliano na watu wote ambao wanahusiana kibiashara, kisiasa na hata kijamii, kwa jambo lolote linalomhusu yeye, kampuni zake ama washirika wake kwa namna yoyote ile.
Manji katika kesi hiyo anawakilishwa na wakili Nasir Hussein Rattansi, katika nyaraka zilizoandaliwa na kampuni ya Law Associates, zenye ofisi zake jengo la CRDB, mtaa wa Azikiwe, Dar es Salaam.
Malalamiko ya Manji yanatokana na mkutano wa waandishi wa habari uliofanywa na Msemakweli na kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwamo televisheni ya ITV ambayo mfanyabiashara huyo pia anaitaja katika hati yake ya kiapo aliyoiwasilisha mahakamani.
Katika mkutano huo, Msemakweli alitaja wahusika wa Kagoda akiwamo Manji na watu wengine kadhaa pamoja na kuwasilisha nyaraka kadhaa, ambazo awali aliziwasilisha kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
Tayari serikali imekwishachukua hatua kwa kuunda kikosi kazi cha kuchunguza sakata hilo huku Msemakweli akiitwa kutoa ushirikiano kwa kuandika maelezo.
Mawakili, Ratansi na Law Associates wanahusika na Kagoda, na majina yao yamo katika nyaraka alizowasilisha Msemakwali kwa DPP na DCI. Ratansi ndiye aliyasaini nyaraka za mkataba kati ya Manji na Kagoda wakati Law Associates walihusika katika kampuni ya Afritainer iliyohusika pia katika EPA ya mwaka 2000 na ina uhusiano na Kagoda. (Docs zote zimo humu JF)
Baada ya kufanikiwa kupata uamuzi wa mahakama ya Temeke kuzuia Mwanahalisi lisimuandike na kubenea kukabidhi nyaraka zote kumhusu, Manji sasa amepata uamuzi wa mahakama ya kinondoni kuzuia raia mwema lisimuandike na kuzuia raia mwema na marafiki zake kutoandika wala kutoweka ktk mitandao habari zozote kuhusu Kagoda na Manji. Pia imefahamika kwamba ameshafanikiwa toka Julai 2001 kupata hukumu Mahakama ya kinondoni kuzuia magazeti yanayotolewa na Mwananchi Communication ya Mwananchi na Citizen kumuandika kuhusu jambo lolote bila kibali chake. Pia kesho anataka mahakama ya kinondoni izuie Tanzania Daima lisimuandike. Tayari Manji amekwama kumzuia Mengi, Msemakweli na wengine kumuandika ama kumsema. Manji amefungua kesi mbili tofauti zinazofanana mahakama kuu na zote anataka kuzuia uhuru wa habari kwa kutaka mitandao yote (Ikiwamo JF) izuiwe kumuandika na itoe habari zake zote haraka iwezekanavyo na wote wenye uhusiano na aliowashitaki kisiasa, kijamii na kibiashara kuzuiwa nao kumsema kwa njia yoyote.
Zaidi, angalia attached images chini
Attachments
-
111017.jpg24.5 KB · Views: 133
-
Manji 1.jpg46 KB · Views: 64
-
Manji 2.jpg17.3 KB · Views: 50
-
Manji 3.jpg27.1 KB · Views: 45
-
Manji 4.jpg46.3 KB · Views: 884
-
Manji 5.jpg39.3 KB · Views: 874
-
Manji 6.jpg41.5 KB · Views: 43
-
Manji 7.jpg38.4 KB · Views: 43
-
Manji 8.jpg36.7 KB · Views: 40
-
Manji 9.jpg32.5 KB · Views: 42
-
Manji 10.jpg37.7 KB · Views: 899
-
Manji 11.jpg22.1 KB · Views: 38
-
Manji 12.jpg3.4 KB · Views: 50
-
Manji 13.jpg3.1 KB · Views: 53