MwanaHalisi na Raia Mwema - silaha za kuangamiza mafisadi na watawala masultani!

DENYO

JF-Expert Member
Sep 14, 2010
698
57
NIMEKUWA NIKISOMA MAGAZETI YA MWANAHASILI NA RAIA MWEMA, kwa kweli sitaki kuwa mnafiki HAYA magazeti ni ukombozi wa MTANZANIA. NI SILAHA ZA MAANGAMIZI KWA MAFISADI NA WATAWALA MASULTANI WANAOJILIMBIKIZIA MALI WANAOSUBIRI WAPELEKEWE MEZANI. NI MAGAZETI YA UKOMBOZI WA MTANZANIA, YANALIPUKA UKWELI BILA KUANGALIA SURA WALA CHEO, HAKUNA UNAFIKI WA KUJIPENDEKEZA KWA MASULTANI -WATAWALA WANAOSUBIRI KUAMBIWA NDIO WAWAJIBIKE. WATANZANIA TUWAUNGE MKONO WASEMAJI WETU -WA NGUVU YA UMMA. MWANAHALISI NA RAIA MWEMA HONGERA
MWANAHALISI KWA KUTUWAKILISHA WANYONGE. LIJE JUA IJE MVUA MWANAHALISI NA RAIA MWEMA YATADUMU KWA NIABA YA UMMA.
 
These two are atleast the few impartial neutral media houses we have in the country!
 
Habari leo ni sawa na tazama, dira, rai, uhuru, mzalendo, mtanzznia, hawa wanandika kile mafisadi wanachosema waandike ili walipwe mshahara, ni magazeti dhaifu, duni na yanayoangamiza umma. Huwatumikia masultani wakati wananchi wanateseka. Mfano mhariri mtendaji wa mtanzania manyerere katka wilya anayotoka msumo vijijini ndiyo ya mwisho kwa maendeleo -yaani maskini wa kutupwa (reference report world bank & imf 2010) lakini yeye badala ya kuanika uovu na wizi wa mali ya umma na kutowajibika kwa viongozi yeye habari zote anawalemba mafisadi na masultani huku musoma vijijini wanakula mapanki. Huo ni uandshi kweli-alitakiwa asimame kidete katika habari kama alivyosimama kuzuia uteuzi wa meghji kuwa waziri.
 
What happened to RAI? hivi hawa wana website?

Rai ni mali ya fisadi kwa sasa. No Room to attack fisadiz. nadhani hata waandishi wake ni tufisadi tudogotudogo. Maana naona wameishakuwa brainwashed!

But Mwananchi nayo inaandika vizuri, tusiisahau.
 
Mwanahalisi and raia mwema are the best newspapers -i can even pay 5000 to buy them.
 
Pamoja na pongezi zote hizo, zitakua hazina faida yeyote Kama wananchi watasoma tu habari na kufahamu bila wanaotuhumia kushugulikuwa. Tunafaham mengi sana kupitia media lakini laiti kuzungumzwa au kuandikwa kwa hayo mambo ingekua mambo yanafanyiwa kazi leo hii tusingekua na haja nayo... Ni Kama wimbo wanatuimbia kila siku kukicha. Twataka action kwa yaandikwayo.
 
What happened to RAI? hivi hawa wana website?

Magazetiyote aliondoka nayo Jenerali Ulimwengu akamuuzia Rostam Aziz KASHATUPU linalofanana na yaliyokua magazeti ya RAI, Mtanzania, The African, Dimba na nyinginezo.

Kwa biashara hii sasa sijui nani aliuziwa cheni bandia na yupi kala noti bandia vile vile humo?? Aziz pengine alidhani gazeti ni yale makaratasi na baadaye akashauriwa akaingize wahariri wenye mikofia, masikini, hata asijue kwamba uhalisia wa gazeti ni SERA ZAKE na jinsi gani hizo sera zinavyoendana na matakwa ya jamii.

Kwa mtaji huu, wala sitoshangaa Jumba lililowahi kuunguruma nchini mwetu la 'Habari Coperation likigeuka zizi la kufugia ngurue hapo baadaye kidogo kama si Godown kabisa pale Sinza.

Mmmhhh!!! Na kama makosa hayo hayajatufunza vyakutosha naye FISADI mwingine kwa Jina la Manji pia kaibuka na gazeti. Watu wengine bwana. Tena huyu angeenda akamtafute Mhe Adamje na gazeti lake la kila msimu wa uchaguzi na wiki mbili kupotea kabisa ndio akajisanyie mizania kama hela alizo nazo ziendelee kumiminwa tu baharini au hapana.

Kila siku najiuliza MAFISADI wanakusudia kutuhabarisha nini na vyombo hivi hasa??????
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom