tz au somaliaHata hivyo; taifa lililolaaniwa chini ya utawala dhalimu haya ni kawaida!
hao ni wafuasi wa chadema. pole yako mdada
hukumu wabakaji na wao wabakwe tu kilazima..MWANAFUNZI wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 13 wa shule ya msingi ya Themi iliyopo jijini Arusha mkoani Arusha hali yake siyo nzuri baada ya kunajisiwa na watu sita.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 1 usiku Oktoba 7 mwaka huu katika kata ya Daraja Mbili jijini hapa. Imeelezwa kuwa sehemu yake ya kizazi imeharibika kutokana na unyama huo.
Akizungumza na gazeti hili jana nyumbani kwake Daraja Mbili mara baada ya kuruhusiwa kutoka katika Hospitali ya Kanisa Katoliki ya Father Babu ya jijini na kuendelea na matibabu Hospitali ya Serikali ya Mount Meru Arusha mwanafunzi huyo alisema pamoja na kuruhusiwa kutoka hospitali lakini hawezi kutembea kutokana na maumivu makali yanayomsumbua.
Alisema siku hiyo kulitokea ugomvi nyumbani na mama yake Zukhura Said (40) na aliamua kukimbilia kwa mjomba wake ndipo njiani alipokutwa na dhahama hiyo ambayo katika maisha yake hataisahau.
Mwanafunzi huyo alisema alifanyiwa unyama huo karibu sana na nyumbani kwao na watu waliomfanyia unyama huo anawafahamu kwa majina na sura na watatu wameshakamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Arusha na watatu bado hawajakamatwa.
Mwanafunzi huyo akizungumza alisema wakati akifanyiwa unyama huo alipoteza fahamu na alijikuta asubuhi akiwa nje ya chumba cha mmoja wa watuhumiwa hao.
Nimefanyiwa unyama mkubwa sana nilipoteza fahamu kutokana na unyama huo na kwa mujibu wa daktari kizazi changu kimetoboka shangazi yangu ndio aliyepiga simu nyumbani kujulisha hali hiyo kwani alinikuta hapo nje asubuhi majira ya saa 2 asubuhi, alisema mwanafunzi huyo.
Akizungumzia tukio hilo mama mzazi wa mtoto huyo, Zukhura Said (40) alisema anasikitishwa na jinsi upelelezi wa tukio hilo unavyoendeshwa kwani mpelelezi wa tukio hilo {jina tunalo} amekuwa mstari wa mbele kutaka wazazi wa pande zote wamalizane kwa kukaa mezani.
Mama huyo alisema wahalifu waliosalia wako mtaani na wazazi wao kwa kushirikiana na kiongozi wa mtaa {jina tunalo} wanafanya kila njama na fitina kutaka kesi hiyo iondolewe Polisi na kurudishwa nyumbani.
Chanzo: Habarileo
Hata hivyo; taifa lililolaaniwa chini ya utawala dhalimu haya ni kawaida!
Hivi hawa waendesha mashtaka na wanasheria huwa hawatafuti lopholes za kisheria kuwaunganisha wanaowasaidia wahalifu na kuwaunganisha na washtakiwa? Kwanini hawawasaidii wanaonyimwa haki? Au mpaka uwe na pesa? Hebu watenge nafasi za kuwasaidia wengine bila gharama kama sadaka yao kwa muumba wa wote. Wakumbuke ipo siku watauhitaji msaada wa jamii inayowazunguka.
Kamata huyo afande njaa na wazazi wa wahalifu kwa kuwasaidia wahalifu kisha tuone matokeo. Hebu wajiweke kwenye maumivu ya huyo binti japo kwa sekunde tu!