Mwanafunzi Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) atengeneza mtandao wa kijamii

Sine r Winters

Senior Member
Jul 10, 2012
110
15
Kuiona cheki hapo social network udom. Hongera sana UDOM. Mungu ibariki UDOM, Mungu ibariki Tanzania.

Salamu wana Jamvi!

Jana katika tupiatupia macho kurasa za magazeti nikajikuta katika kurasa moja ya makala ya gazeti la "Mwananchi" ikiwa na kichwa cha habari kama nilivyokiandika katika "Title" yangu. Nilivyoshawishika kuisoma habari hiyo nikagundua kumbe vyuo vyetu vinaweza kuzalisha vijana ambao wana mawazo ya kujiajiri.

Huyu kijana ameanzisha "mtandao wa kijamii" kama ilivyo kwa "facebook" (Welcome to Mayocoo - Sign in, Sign up). Na kwa jinsi alivyoelezea, anadai inamambo mengi na salama hata zaidi ya hiyo "facebook".

Mimi nimefarijika (ingawa ni duplication ya idea).
Ombi langu kwa viwanda hivi (Vyuo), watazame zaidi mihula yao ili si tu hawa "mazalia" waweze kutengeneza vitu ambavyo tayari vipo, ila wawe na uwezo wa kufikiri na kuja na idea mpya. Na pia naamini vyuo vinaweza kuanzisha miradi ya kuwasaidia vijana ambao wanafungua njia za kujitemea. Ni rahisi kwa vyuo kutambua umuhimu wa mawazo ya wahitimu wao kuliko "taasisi" nyingine.

Mwisho: Kuzalisha wahitimu wenye mawazo ya kujiajiri inawezekana.
 
dat is good
but inabidi acheki security yake maana tanzania tumeingiliwa hivyo ahakikishe anafanya backup ya file zake zote pia kama ali host kwa free web host au ile ya bei rahisi awe makini
 
Toa details zake hapa tafadhali
Jina lake wasifu wake
Namba zake za simu
 
kama ni product ya UDOM nahisi kama namfahamu huyu mtu!!!!
ipo na muonekano mzuri
mbona hamna basic information za hii site sasa ntaaminije kama ni product toka TZ(udom)?
 
Samahani kama taonekana pessimistic..

Hio network yake ina watu wangapi ?

Sababu kutengeneza platform is one thing.., na ku-market, kupata watu kujiunga na kustick na forum yako is a totally different ball game.., ndio maana hata kina MySpace ingawa walikuja before Facebook lakini we know what happened..

Pia kuna forums nyingi zenye format na engine kama ya JF lakini nyingi zina visitors wawili baada ya miaka mitatu..

Kwahio kwenye Social Networks what really matters is the Network (people interactions) more than anything
 
samahani kama taonekana pessimistic..

Hio network yake ina watu wangapi ?

Sababu kutengeneza platform is one thing.., na ku-market, kupata watu kujiunga na kustick na forum yako is a totally different ball game.., ndio maana hata kina myspace ingawa walikuja before facebook lakini we know what happened..

Pia kuna forums nyingi zenye format na engine kama ya jf lakini nyingi zina visitors wawili baada ya miaka mitatu..

Kwahio kwenye social networks what really matters is the network (people interactions) more than anything
idea kwanza
 
nime-join ::::it loads very slowly,:::::ushauri wangu kwa Mayocoo team---watafute server kubwa kwa ajili ya kuhost website hii...pia kuna some spelling errors,mfano kwenye settings->deactivate->kuna sehemu inasema "underconstraction" ..... pia,kuna links kibao hazifanyi kazi(mfano,developers,privacy policy,na terms of service)..arekebishe...namtakia kila la kheri...ila ingekuwa vyema tukifahamu maana halisi ya neno "mayocoo"..its good to know the meaning,,,,,,,Kila la heri...Mungu abariki kazi yake.
 
idea kwanza

Indeed mkuu...

Lakini je idea ilianzia Udom, Facebook, MySpace, Bulletin Board System, Friendster, Linkedln n.k. ?

Pongezi natoa kwa IT literacy na coding efficiency lakini point za mafanikio ya social network yatatoka baada ya kujenga network na stick-ability ya said network (watu wakiingia wanakaa hawaondoki) and to do that marketing and promotion skills are needed even more than coding and IT skills
 
Back
Top Bottom