Mwanafunzi Afia kwenye Daladala ya Kawe -Karikaoo wakati mjada wa Budget wizara ya Afya Unaendelea

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
May 24, 2008
10,942
428
Leo Majira ya saa moja na dakika 45 Asubuhi nikiwa nimepanda daladala pale kituo cha moroco kwenda kawe kwa bahati mbaya sikupata siti mpaka kwa Mwalimu, lakini tangu napanda kulikuwa na mwanafunzi wa kike ameketi katika siti amefunga hijabu lakini alikuwa anaonekana amesinzia ikafika njia panda ya coca colla konda akawa anakusanya nauli kufika kwa yule mwanafunzi akamuamsha lakini Binti alikuwa harespond chochote konda akajua ni usanii labda hataki kulipa nauli akamtikisa wapi!!... Ndipo watu wakaanza kumsaidia Kumuamsha, Lakini kumuangalia mapigo alikuwa kimya ,ndipo watu wazima walipomcheki na kugundua ameshafariki Imenisikitisha sana maana kabinti kamefia usingizini wakat mjada wa Budget wizara ya Afya ukiwa unaendelea dodoma
 
Leo Majira ya saa moja na dakika 45 Asubuhi nikiwa nimepanda daladala pale kituo cha moroco kwenda kawe kwa bahati mbaya sikupata siti mpaka kwa Mwalimu, lakini tangu napanda kulikuwa na mwanafunzi wa kike ameketi katika siti amefunga hijabu lakini alikuwa anaonekana amesinzia ikafika njia panda ya coca colla konda akawa anakusanya nauli kufika kwa yule mwanafunzi akamuamsha lakini Binti alikuwa harespond chochote konda akajua ni usanii labda hataki kulipa nauli akamtikisa wapi!!... Ndipo watu wakaanza kumsaidia Kumuamsha, Lakini kumuangalia mapigo alikuwa kimya ,ndipo watu wazima walipomcheki na kugundua ameshafariki Imenisikitisha sana maana kabinti kamefia usingizini wakat mjada wa Budget wizara ya Afya ukiwa unaendelea dodoma

maskini!!! inasikitisha sana!!!!!!!
 
Leo Majira ya saa moja na dakika 45 Asubuhi nikiwa nimepanda daladala pale kituo cha moroco kwenda kawe kwa bahati mbaya sikupata siti mpaka kwa Mwalimu, lakini tangu napanda kulikuwa na mwanafunzi wa kike ameketi katika siti amefunga hijabu lakini alikuwa anaonekana amesinzia ikafika njia panda ya coca colla konda akawa anakusanya nauli kufika kwa yule mwanafunzi akamuamsha lakini Binti alikuwa harespond chochote konda akajua ni usanii labda hataki kulipa nauli akamtikisa wapi!!... Ndipo watu wakaanza kumsaidia Kumuamsha, Lakini kumuangalia mapigo alikuwa kimya ,ndipo watu wazima walipomcheki na kugundua ameshafariki Imenisikitisha sana maana kabinti kamefia usingizini wakat mjada wa Budget wizara ya Afya ukiwa unaendelea dodoma

Sijaona link kati ya kifo hicho na mjadala wa budget.
 
Duhu!! Inauma sana ,the only solution ni kuondoa huu utawala dhalimu kwa maandamano,If posible tujipange weekend hii tuweke kambi Mnazi mmoja hope ndio sehemu nzuri ya kuanzia maandamano tukielekea Ikulu
 
Je binti huyo aliweza kujulikan ni wa shule gani? na abiria waliotoka na gari kariakoo au konda wanasema kapandia wapi huyo binti? Inna Lillah wa inna Ilay rajiuna.
 
RIP student!!

Ni njia ambayo kila mmoja wetu lazima apitie. Cha kusikitisha ni namna ambavyo mtu huwa anatutoka.
 
Sijaona link kati ya kifo hicho na mjadala wa budget.

Ningekuwa mhuni ningekutukana,pia avatar yako inaonyesha uwezo wako wa kufikilia very poor.Mtu mzima ovyoo!!!!!!!!!!!!!

Yani usichoona link ya tukio na KIFO CHA BINTI HUYU MDOGO [RIP] nini? Unajua kama mfumo wetu wa afya ungekuwa ni wa haki binti huyu familia yake ingekuwa inajua status ya binti yao hata kama si mgonjwa kwa kuwa mfumo ungekuwa unaruhusu Medical check up.
 
Ningekuwa mhuni ningekutukana,pia avatar yako inaonyesha uwezo wako wa kufikilia very poor.Mtu mzima ovyoo!!!!!!!!!!!!!

Yani usichoona link ya tukio na KIFO CHA BINTI HUYU MDOGO [RIP] nini? Unajua kama mfumo wetu wa afya ungekuwa ni wa haki binti huyu familia yake ingekuwa inajua status ya binti yao hata kama si mgonjwa kwa kuwa mfumo ungekuwa unaruhusu Medical check up.

Unajua kilichomuua??.
 
Unajua kilichomuua??.

Jamii ya watu waliostaarabika haswa tunaoishi mijini,tunajua kuwa tuna mazingira ya ustaarabu yaliyotuzunguka,zikiwemo hospitali na mengineyo.Kifoc ha ghafla si kuwa havitokei vinatokea.

Kwa akili ya kawaida ya kibinadamu afya zetu sisi Watanzania katika mazingira ya mfumo wetu wa kiafya,uwa tunazifanyia ukaguzi [Medical Check up] bila ya kusubilia ugonjwa.Hakika jibu lako litakua hakuna,. Na assumption zako mtoto huyo tujue amekufa na nini kwanza kisha tukishajua kilichomua ndio tuangushe lawama kwa wizara ya Afya ambayo leo ilikuwa inasoma budget yake.

Kwanini kwa assumption zako hizo hizo tusiassume kuwa mtoto huyu ajapewa sumu,au kunywa sumu ambayo imeondoa uai wake,bali tuassume mtoto huyu alikuwa mgonjwa kwa namna ambayo mazingira yamemfanya victim wa situation iliyotokea leo.

Mazingira circumstance ya situation kwangu mimi,kama mtu mzima binti huyu nampa 20% uenda kifo chake kuwa kama ningekuwa ni kuassume kuwa binti huyu ni victim wa case hiyo ambayo wewe unataka tuone kama yaweza kuwa ni sababu ya kifo chake. Lakini assumption zangu kwa umri wake kupata matatizo hayo yaliyotokea leo yametokana na ugonjwa ingekuwa 80%.

Na unajua kama ni ugonjwa ni dhahili alieanzisha thread hii ilikuwa kusudio lake la kutuambia kuwa katika taarifa zote ulizoziskia leo kupitia budget ya wizara ya Afya kwa siku ya leo,lakini kw upande wa Afya bado tuko nyuma mpaka Taifa linampoteza binti huyu mdogo ambae hatujui Mungu angempa nafasi gani kulitumia Taifa hili.Uenda angekuwa Anna makinda ajae,au Roze Asha Migiro wa miaka hiyo ijayo au hata Rais wa Jamhuri ya Muuungano,lakini kwa kuwa mikakati yetu ya wizara husika bado ni tatizo kwa jamii yetu.

Unajua kuna Mataifa ya wenzetu yana mipango bora ya uzazi, kati ya watoto mia [100] wanaozaliwa ni watoto watatu tu [3] wanatopoteza, maisha wakati wanazaliwa.Je unajua nchini kwako ni watoto wangapi wanapoteza maisha yao wakati wanazaliwa, kati ya watoto mia [100] wanaozaliwa?

Kinchopigiwa kelele ni jukumu la wizara na mikakati yake katika kumkwamua mtanzania dhidi ya magonjwa yanayomsumbua,na huduma za Afya kwa ujumla wake ili awe salama na kumudu maisha yake na kuendleza ujenzi wa Taifa lake.

Bro acha mchezo na afya.Unajua sasa hivi imeibuka Malaria inayomfikisha mgonjwa ICU toka ilimposhika yuko barabarani,au yuko ofisini kwake. Au wewe mwenzetu unaishi UK,au USA,inawezekana ujui kwanini watu wanaumia na hali hii.
 
Sijaona link kati ya kifo hicho na mjadala wa budget.
link ipo, afya ya mtoto haikua salama lakini ndo hivyo tena wengi tu tunatembea siajabu bila kujua kwamba miili imeshakwisha kazi

Apumzike kwa amani mtoto mzuri, ametangulia tu, na sie tupo mbioni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom