Mwanafunzi afariki katika ghasia Chuo Kikuu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Mwanafunzi afariki katika ghasia Chuo Kikuu
Mwandishi wetu
Daily News; Sunday,February 24, 2008 @00:02

FAMILIA ya Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, juzi usiku ilinusurika wakati wanafunzi wa chuo hicho, sehemu ya Mlimani, kuvamia nyumbani kwake wakishinikiza wapatiwe huduma ya maji.

Wanafunzi hao walifanya fujo katika maeneo mbalimbali ya chuo na mmoja kuzama katika bwawa la kuogelea chuoni hapo na kufariki dunia saa 4.30 usiku wakati akipata tiba katika hospitali ya chuo hicho.

Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, aliieleza HabariLeo Jumapili kuwa aliyefariki ni Deogratius Dominick aliyekuwa akisoma mwaka wa kwanza chuoni hapo.

Profesa Mukandala alisema jana jioni kuwa wanafunzi hao waliingia kuogelea baada ya kufanya vurugu katika maeneo mbalimbali ya chuo, ikiwa ni pamoja na kuvamia makazi yake, kuwashambulia wahadhiri na watu wengine katika eneo la UDASA.

Wakati makazi ya Profesa Mukandala yakishambuliwa alikuwa Zanzibar, hivyo endapo wanafunzi wangefanikiwa kuingia ndani ya nyumba anayoishi wangemkuta mkewe na watoto wake wawili.

Kwa mujibu wa Profesa Mukandala, kabla ya kuivamia familia yake na kuvunja geti la nyumba ya mlinzi, wanafunzi hao walikutana katika eneo la Hall 2 saa nne kasorobo usiku, baadaye walikwenda katika eneo la ofisi za utawala wakakubaliana kuwa wakamvamie.

Alieleza kusikitishwa pia na kitendo cha wanafunzi hao kuwavamia wahadhiri na watu wengine, wakiwamo wanafunzi wa kike Hall 3, kuharibu ofisi katika jengo la Hall 4, kuharibu milango 21 na mali nyingine.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Liberatus Barlow, jana aliwaeleza waandishi wa habari kuwa mwanafunzi aliyefariki dunia alijirusha katika bwawa, lakini haikufahamika endapo alikuwa na lengo la kuogelea au kufanya uharibifu wa miundombinu ya bwawa hilo.

Kwa mujibu wa Kamanda Barlow, wanafunzi hao walikwenda katika eneo hilo baada ya kufanya vurugu nyumbani kwa Profesa Mukandala, UDASA, nyumbani kwa Meneja makazi wa chuo hicho na katika makazi ya wanafunzi.

“Vurugu hizi chanzo chake ni kukatika huduma ya maji katika eneo la Chuo Kikuu. Uchunguzi umeonyesha kuwa maji hayo yalikatwa kutokana na ukarabati unaofanyika Lower Ruvu,” alisema.

Aliwaeleza waandishi wa habari kuwa, wanafunzi hao waliharibu magari mawili kwa kuyavunja vioo, likiwamo aina ya Corolla Limited lenye namba za usajili T 824 ABL lililovunjwa kioo cha nyuma.

Kwa mujibu wa Barlow, wanafunzi walifanya vurugu UDASA kwa takribani saa moja na nusu, baadaye walivamia nyumba ya Meneja Makazi wa Chuo wakavunja vioo vya madirisha 13.

Kwa mujibu wa polisi, walipotoka hapo walikwenda katika jengo liitwalo Hall 7 wakawalazimisha wenzao waungane nao kwenye vurugu hizo, milango 15 ikaharibiwa kidogo. “Pia vurugu hizo zilienea katika eneo la Hall 2 na 1.

Hata hivyo, maeneo hayo mawili hayakupata madhara,” alisema Barlow na kubainisha kuwa walipotoka hapo walikwenda katika bwawa la kuogelea wakavunja geti la kuingilia katika eneo hilo.

“Wanafunzi wanadai vurugu hizo zilichochewa na kukatwa huduma ya maji, hata hivyo ni mapema mno kutamka kwamba kilichopelekea kutokea kwa vurugu hizo ni tatizo hilo,” alisema. Alisema, uongozi wa Chu,o sehemu ya Mlimani, ulitoa huduma kwa kuweka maboza ya maji na kwamba haikuwa mara ya kwanza maji kukatika katika eneo hilo.
 
Wanafunzi UD sasa wanakosa hekima mbele ya Watz..sasa uharibifu wa mali na kupiga watu ndo watapata maji?

Mbona Dar pia kuna watu miaka mingi tuu hawana maji?

Wanaweza kuandamana..ila kuharibu mali ni aibu kwa wasomi!
 
The arrogance, such audacity!

Makes you wonder about the quality of education they are getting.A case of the chicken coming home to roost perhaps?
 
Ni jambo la kusikitisha kuona wasomi na viongozi wa kesho wa taifa letu wanafanya mambo kama haya.

Matatizo kama haya yameanza kujitokeza kwa wanafunzi wa ngazi mbali mbali pia. Nafikiri elimu na malezi yetu yamechangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka kwa maadili ya jamii.

Kuna mifano kama kule morogoro ambako wazazi waliwapiga walimu kwa kuwadhibu wanafunzi ambao walikuwa na makosa mbali mbali ikiwemo kutohudhuria zamu za wakati wa likizo.

katibu mkuu mama malale alitoa tamko mwalimu mkuu wa shule fulani achukuliwe hatua kwa makosa mbali mbali ikiwa ni pamoja na kushindwa kupanga wanafunzi zamu wakati wa likizo.

Tukaona pia kule morogoro wanafunzi wa sekondari walivyofanya vurugu ya kuharibu vitu vya shule kwa kutopikiwa WALI.

Na sasa hawa wa chuo.

Ni wazi serikali inatakiwa ichukue hatua ya haraka kwa kudhibiti vitendo vya namna hii.

Ni aina gani ya wasomi tunaowajenga? ni aina gani ya wafanyakazi wanaojengwa? Ni dhahiri kama tabia hii haitatafutiwa suluhisho mapema matendo kama haya yanaweza kuzoeleka na kuonekana ni jambo la kawaida.

AIBU kwenu wasomi wa chuo kikuu.
 
hayo ndio matunda yanayopatikana ktk nchi yeyote inayoendeshwa "kifisadi." Watoto hawana role models, kuanzia nyumbani mpaka viongozi wao wa serikali.
Kama jamii ya TZ haita kaa chini na kuji-evaluate from inside out, tena kuanzia ngazi ya familia na mtu mmoja mmoja binafsi.... basi matukio haya ni "trela" tu, makubwa yapo njiani yanakuja!!
Mungu inusuru Tanzania!!.
 
Hi jamani mbona hawa madogo wanatutia aibu??

Kweli mtu amefikia level ya UNIVERSITY anashindwa kutumia akili kweli kwa kuangalia tu na kutambua kuwa MAJI HAYAPATIKANI KWA MUKANDALA,, This guys are crazy, Mimi ningewaona wajanja sana kama wangeenda kufanya fujo kwenye ofisi za Dawasa na si kwenda kufanya fujo kwa Prof Rwekaza. Ninachokiona hapa ni ukosefu wa maadili na njaa ndo zinawasumbua kwa sababu wiki iliyopita kulitokea vurugu kama hizo Mabibo campus, walichokifanya ni aibu maana walivunja baa wakaiba bia na soda zote, sasa kweli hawa tunaowategemea ndo waje wawe viongozi wanaiba hata bia wakipewa madaraka si ndo wataturichmond kabisa? Shame on u all UD studensts.
 
Wanafunzi UD sasa wanakosa hekima mbele ya Watz..sasa uharibifu wa mali na kupiga watu ndo watapata maji?

Mbona Dar pia kuna watu miaka mingi tuu hawana maji?

Wanaweza kuandamana..ila kuharibu mali ni aibu kwa wasomi!

Hii ni taswira ya namna jamii yetu inavypotoka sana. jamii sasa haifahamu moral values...Hakuna tena anayejua maadili yetu, achilia mbali ukomavu wa akili unapoatikana mtu anapokwenda shule.

Hawa vijana wamefanya kitendo cha kihuni, ambacho kingefanywa hata na wahuni wa vituo vya mabasi huko Manzese...na hawajafanya tofauti yoyote ionekane baina yao na wale waliokosa shule. They have just put themselves in the same class as those crooks.

Ni kweli, tunahitaji mapinduzi makubwa kuanzia kwenye ngazi ya familia. watu tufahamu na tutekeleze wajibu wetu kama wazazi, kama walezi, kama viongozi, ili wanaofuata wapate mifano bora na halisi juu ya namna ya kupambana na changamoto za kila siku maishani.

Hawa kwa uvivu wao wa kufikiri, na walivyokuwa under heavy influence of culture imperialism... Nadhani kuna siku watapigana risasi kama wanavyofanya wenzao hao.
 
Halafu atakuja mtu aseme wasikilize wasomi toka Chuo Kikuu wamebobea nitamtoa mkuku ile mbaya .
 
Jamani huo si ukosefu wa maadili bali nidalili za uchovu! uchovu wa kuwaza na kufikiri, mambo yamezidi ukiona mtu mzima analia ujue yamemzidi ndio hayo, matatizo ni mengi na ndio watu wamechoshwa kinachouma wapo wanaofaidi hawana shida ya maji wala umeme!
Kukatika maji chuo kikuu sio suala la ajabu ni suala la kawaida, vyoo vinafungwa ukiwa madarasani unalazimika kuzunguka majengo 2 au 3 kutafuta choo chenye afadhali upate kujisitiri, kisa maji hakuna bado tunaambiwa kuchangia na halli ngumu ya maisha mtoto wa mlala hoi anatakiwa achangie asilimia kadhaa ili awepo CHUONI kujisomesha bado hakuna maji, vitabu nk unadhani nini kitakachotokea,hilo ni dogo usione vita ukadhani watu wanapenda ila ni watu wamechoshwa hii inabidi iangaliwe na kutathminiwa UONGOZI wa CHUO kikuu mlifikirie katika hali tofauti hili ili kuleta na maendeleza AMANI ya NCHI yetu Nzuri TUIPENDAYO!!

Ni mara nyingi vyoo hufungwa madarasani na hata kama vipo wazi haviingiliki hakuna maji vyoo si vya mashimo jamani au UONGOZI haufahamu hili,


Mungu IBARIKI TANZANIA!
 
Jamani huo si ukosefu wa maadili bali nidalili za uchovu! uchovu wa kuwaza na kufikiri, mambo yamezidi ukiona mtu mzima analia ujue yamemzidi ndio hayo, matatizo ni mengi na ndio watu wamechoshwa kinachouma wapo wanaofaidi hawana shida ya maji wala umeme!
Kukatika maji chuo kikuu sio suala la ajabu ni suala la kawaida, vyoo vinafungwa ukiwa madarasani unalazimika kuzunguka majengo 2 au 3 kutafuta choo chenye afadhali upate kujisitiri, kisa maji hakuna bado tunaambiwa kuchangia na halli ngumu ya maisha mtoto wa mlala hoi anatakiwa achangie asilimia kadhaa ili awepo CHUONI kujisomesha bado hakuna maji, vitabu nk unadhani nini kitakachotokea,hilo ni dogo usione vita ukadhani watu wanapenda ila ni watu wamechoshwa hii inabidi iangaliwe na kutathminiwa UONGOZI wa CHUO kikuu mlifikirie katika hali tofauti hili ili kuleta na maendeleza AMANI ya NCHI yetu Nzuri TUIPENDAYO!!

Ni mara nyingi vyoo hufungwa madarasani na hata kama vipo wazi haviingiliki hakuna maji vyoo si vya mashimo jamani au UONGOZI haufahamu hili,


Mungu IBARIKI TANZANIA!


Karibu sana Bibi Kizee .Umesha sema lawama sasa suggest Solution
 
Jamani huo si ukosefu wa maadili bali nidalili za uchovu! uchovu wa kuwaza na kufikiri, mambo yamezidi ukiona mtu mzima analia ujue yamemzidi ndio hayo, matatizo ni mengi na ndio watu wamechoshwa kinachouma wapo wanaofaidi hawana shida ya maji wala umeme!
Kukatika maji chuo kikuu sio suala la ajabu ni suala la kawaida, vyoo vinafungwa ukiwa madarasani unalazimika kuzunguka majengo 2 au 3 kutafuta choo chenye afadhali upate kujisitiri, kisa maji hakuna bado tunaambiwa kuchangia na halli ngumu ya maisha mtoto wa mlala hoi anatakiwa achangie asilimia kadhaa ili awepo CHUONI kujisomesha bado hakuna maji, vitabu nk unadhani nini kitakachotokea,hilo ni dogo usione vita ukadhani watu wanapenda ila ni watu wamechoshwa hii inabidi iangaliwe na kutathminiwa UONGOZI wa CHUO kikuu mlifikirie katika hali tofauti hili ili kuleta na maendeleza AMANI ya NCHI yetu Nzuri TUIPENDAYO!!

Ni mara nyingi vyoo hufungwa madarasani na hata kama vipo wazi haviingiliki hakuna maji vyoo si vya mashimo jamani au UONGOZI haufahamu hili,


Mungu IBARIKI TANZANIA!

Mkuu Bi Kizee,

Shukrani!

Wengi wetu tunafahamu taabu waipatayo wanafunzi wa chuo kikuu, hatubishi. Lakini kwa wasomi wanaojifunza na kuchambua mbinu mbali mbali za mwanadamu kukabiliana na mazingira yake, hatutegemei wavamie makazi ya watu, waharibu mali na kutishia maisha ya watu wengine. Hizo ni fujo, na kwa sheria za nchi, ni kosa la jinai. Kwa kufanya fujo hivyo, ni wazi kuwa maji yasingetoka pia. Zaidi zaidi, wangeishia lupango kwa uharibifu au kujeruhi.

Wangeonyesha ujenzi wa hoja madhubuti juu ya matatizo yao, pengine wangefanikiwa hata kumfukuzisha kazi Mukandala...inategemea wangekuwa na hoja nzito kiasi gani. Wangepata public sypmathy, na pengine yule mwenzao angekuwa anasoma JF sasa hivi kwa raha zake.

Frustrations and anger can not be best reasons for breaking of the law. Silaha ya msomi ni hoja, na si kuvunja vunja vitu na kutaka kusikilizwa. Unadhani wangefanikiwa kuipata familia ya yeyote pale ambayo ngeleta nao zogo si wangeishia kubaka wale? Mob psychology ni kitu kibaya sana.

Tatizo la maji bongo si la chuo tu, na wengine hawajakimbilia kufanya fujo hata DAWASA ili kushinikiza kupatikana kwa maji hayo.

Kama wasomi, wanategemewa kuonyesha njia mbadala za kutatua matatizo ya jamii kwa hoja na kufanya tafiti mbalimbali juu ya matatizo hayo. Kwa kufanya fujo eti kwa sababu maji ni tatizo, wasomi wetu wameonyesha udhaifu mkubwa wa bongo zao, kwamba their brains tend to overheat easily if subjected to too much thinking. What is the use of going to school then?

Wale wanaopendelea nguvu zaidi pia sehemu yao ipo, ila wawe tayari kwenda kwanza Military Academy Kunduchi. Wao hutumika where we use iron to cut iron.

Bi Kizee, hivi na yule mwanafunzi aliyeruka ghorofani kukwepa kukamatwa baadaya kufumwa akiiba kompyuta za chuo ilikuwa ni frustrations?
 
Halafu atakuja mtu aseme wasikilize wasomi toka Chuo Kikuu wamebobea nitamtoa mkuku ile mbaya .

teh teh teh teh hii kali sana
mtembelee pia kwenye ukumbi wa elimu maana wengi wanaishia hapa tkt ukumbi wa siasa.
 
Jamani huo si ukosefu wa maadili bali nidalili za uchovu! uchovu wa kuwaza na kufikiri, mambo yamezidi ukiona mtu mzima analia ujue yamemzidi ndio hayo, matatizo ni mengi na ndio watu wamechoshwa kinachouma wapo wanaofaidi hawana shida ya maji wala umeme!
Kukatika maji chuo kikuu sio suala la ajabu ni suala la kawaida, vyoo vinafungwa ukiwa madarasani unalazimika kuzunguka majengo 2 au 3 kutafuta choo chenye afadhali upate kujisitiri, kisa maji hakuna bado tunaambiwa kuchangia na halli ngumu ya maisha mtoto wa mlala hoi anatakiwa achangie asilimia kadhaa ili awepo CHUONI kujisomesha bado hakuna maji, vitabu nk unadhani nini kitakachotokea,hilo ni dogo usione vita ukadhani watu wanapenda ila ni watu wamechoshwa hii inabidi iangaliwe na kutathminiwa UONGOZI wa CHUO kikuu mlifikirie katika hali tofauti hili ili kuleta na maendeleza AMANI ya NCHI yetu Nzuri TUIPENDAYO!!

Ni mara nyingi vyoo hufungwa madarasani na hata kama vipo wazi haviingiliki hakuna maji vyoo si vya mashimo jamani au UONGOZI haufahamu hili,


Mungu IBARIKI TANZANIA!

kwa hiyo hakina hadhi ya kua chuo kikuu
 
Mwanafunzi afariki katika ghasia Chuo Kikuu
Mwandishi wetu
Daily News; Sunday,February 24, 2008 @00:02

....

Wanafunzi hao walifanya fujo katika maeneo mbalimbali ya chuo na mmoja kuzama katika bwawa la kuogelea chuoni hapo na kufariki dunia saa 4.30 usiku wakati akipata tiba katika hospitali ya chuo hicho.


Pamoja na pole ya msiba; huyu jamaa aliyezama swimming pool inawezekana alikuwa amelewa? au labda mfupi sana? au wenzie walimkandamiza kwenye maji? maswali ni mengi na hakuna maelezo yanayotosheleza mazingira ya kifo hiki. Nafakiri wazazi wa kijana huyu watahitaji kujua zaidi ya hii taarifa ya ki-polisi
 
Ndiyo yale yale ya Mwalimu (RIP) ya kugoma kushare vyumba wakati watu huko makwao wanapotoka wanabanana chumba kimoja pamoja na kuku na mbuzi. Hapo ukichunguza utakuta vinara wa mgomo wanatokea maeneo ambayo maji kwao ni kama dhahabu!
Anyway, labda wameamua ku copy style ya wanajeshi!
 
Karibu sana Bibi Kizee .Umesha sema lawama sasa suggest Solution
Majengo ya kisasa (kizungu) yanahitaji huduma za maji/umeme ili maisha yawe kama kwetu ambapo maji ni ya kisima na vyoo vya shimo. Hivyo uongozi wa chuo waige kile kilichofanywa na Wajapani katika wodi za watoto (A na B) pale Muhimbili hospital kwa kuchimba kisima kirefu ambacho kiliondoa adha ya ukosefu wa maji kwenye wodi hizo. Hii ni local solution wala haihitaji wataalam toka nje, FOE si wapo. Gharama ya deepwell pump na uchimbaji wa kisima kimoja hauzidi $ 3000. Vinginevyo wafanyie ukarabati mfumo wa mabomba, mmoja kwa maji ya kunywa na mwingine kwa maji yasio salama kunywa(industrial water)ambao utatumia maji ya kutoka bwawa karibu ya S/Msingi ikiwa ni long term solution.
 
The arrogance, such audacity!

Makes you wonder about the quality of education they are getting.A case of the chicken coming home to roost perhaps?

Sijui wewe binafsi kama ulipitia mlimani..lakini kwa akina sisi tuliopitia hapo twajua hali halisi kwa jinsi gani shule ilivyo mchakamchaka usiohitaji hata lag of 1 second...

Ktk hali kama hiyo haiwezekani hata kidogo kubalance btn shule na biashara kichaa ya kutafuta maji au sehemu ya kujisitiri kwa ajili ya call of nature..Quality of education has got nothing to do with the choice of few students who acted beyond limits..

Jamani tupende na kusaidia kuboresha vyuo vyetu kwa hali, mali na hata kauli zetu..uovu ukemewe lakini bila kupropose solution ni kuplay blame game which everyone of us is a pro.
 
Role models wao ni wale wanajeshi waliovamia DAWASCO juzi!

kwikwikwi....kweli kabisa, maana matukio yamefuatana, sijui hata wakina nani walioanza!!. seriously ni nani aloanza, ni hao wanajeshi wasokuwa na la maana la kufanya au ni hiyo mianafunzi vilaza???

mgogoro wa maji darisalama ni mkongwe, pengine kushinda umri za baadhi ya hao "njuka" toka swekeni huko ambako walikuwa hawana hata maji ya bomba!!! soln ni kuishinikiza serikali kwa hoja za why and how na sio kwenda kufanya ghasia zisokuwa na kichwa wala miguu.
Pole kwa familia ya marehemu!! lakini kuna swali najiuliza.......je, marhumu alikuwa anajua kuogelea!!?? kama jibu ni NO, basi itabidi nisiendelee na mjadala huu!! wallahi, kaaaazi kwelikweli.
 
Hii habari imenisikitisha sana kwasababu maisha ya mtu yamekatika ghafla kwa jambo ambalo wala halikuwa muhimu. Ndugu na marafiki waliokuwa wanamtegemea, wamepoteza mtoto, kaka, rafiki kwasababu ya umwamba ambao hauna maana yoyote.

Inaonyesha mlimani hata first aid ni tatizo. Hivi jamani sisi tuna matatizo gani? Wala hatuhitaji pesa za ziada kuwaandaa vijana wetu kwa majanga mbalimbali. Badala ya kumkimbiza hospitali, angehudumiwa vizuri pale pale, huenda angesalimika.

Hii dunia kadri tunavyokuwa mbele kudai haki zetu lazima pia tuwe mbele kulinda haki za watu wengine. Kuvamia nyumba za watu, kuiba, kupiga wafanyakazi kwa makusudi hata siku moja haiwezi kuwa jawabu ya matatizo yetu.

Vijana wa mlimani lazima wajue wao inatakiwa wawe kioo cha taifa kwa kujua kudai haki zao lakini pia kioo cha taifa kwa kulinda na kutetea haki za wengine pia. Kinyume cha hayo tunarudi kule kule, kwamba unalalamika kwasababu yanakuhusu wewe, yakimhusu Mtanzania mwingine, you don't care!
 
Back
Top Bottom