Uchaguzi 2020 Mwana wa kulitafuta Lijualikali kalipata, baada ya kuangukia pua Ubunge ajaribu udiwani na kuambulia kura 5. Adaiwa kutamani kurudi CHADEMA

Lijualikali ataishi kwa kutangatanga sana, laana ya kuwasaliti wananchi Wa kilombero haitamuacha salama

Huyo ndio basi tena atabaki na historia ya kujakuwasimulia wajukuu zake kuwa aliwahi kuwa Mbunge kimasihara masihara, siri kubwa unapoacha kazi point A na ukaenda fanyiwa usaili point B kamwe usijaribu kumsema vibaya mwajiri wa kwanza kwani ukifanya hivyo tu mara moja unakuwa umekosa credibility kwa mwajiri mpya na hawezi kukuajiri
 
images (2).jpeg
 
mene, mene, tekeli na peresi


“Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
27 Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
28 Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
 
Huyu mpumbavu nakumbuka alidondosha hadi chozi bungeni...

Aisee...!!
Ushamba na ulimbukeni kutoka kwenye ule ufukara ghafla anaona mil250 inakuja mbele yake kwa nn asiwehuke......
 
Ningekuwa mimi baada ya kula kura 2 za UDIWANI na 5 za UBUNGE.... ningerudi hapo mlimani CITY nikawapigia magoti wajumbe wa Balaza kuu...huku nikimwaga michozi kama yote...wangenisamehe tu.
 
achana na Ubunge mzee jiran yangu hapa miaka mi 5 tu ana nyumba 7 za MAANA nazozijua na alikua kapanga...... Sabufa akaona njia ni hiyo tu kuponesha kitumbua chake hahaha
Hatari sana mtu wa namna hiyo anatafuta uongozi kwajili manufaa yake binafsi tu.
 
Taarifa nilizo nazo ni kwamba aliyekuwa mbunge wa Kilombero mh Lijualikali ana mipango ya kurejea Chadema na ameonekana maeneo ya Mlimani city katika mgahawa akiongea na mjumbe mmoja wa kamati kuu.

Mnyetishaji amenijuza kuwa Lijualikali amesema yuko tayari kuwa meneja kampeni wa Prof Jay katika jimbo la mikumi kwa gharama zake kama ishara ya kuonyesha toba na utii kwa Chadema.

Taarifa kamili itakuja.

Maendeleo hayana vyama!
 
Mwambieni ajiajiri maana wakiwa bungeni huwa wanaona ambao wanatafuta kazi kama punguani na wasio na maarifa zamu yake saivi

Motivation speaker wako wapi hawamuoni wampe fulsa ya kulima matikiti maana mtaji amesha pata miaka 5
 
Hatari sana mtu wa namna hiyo anatafuta uongozi kwajili manufaa yake binafsi tu.
Ndo hivo hakuna mbunge anaepambania wananchi kiivo wapo kwa manufaa yao pande zote tu ukifuatilia wanavojiwekezea ndo utajua. maguest..mahoteli wanajijengea. Lakini cjui zahanati au darasa limejengwa na mbunge wachache sanaaa cjawai sikia...
 
Kina Lijualikali, Mtolea nk walishinda Ubunge kwa sababu ya kampeni za mafuriko. Lowasa aliwaomba wananchi wamchagulie wabunge. Hawa jamaa hawakushinda kwa sababu ya sera au kuwa popular. Hata wangebaki upinzani, this time wasingeshinda ng'oo. Bora wabaki CCM wanaweza wakakumbukwa kwenye teuzi nyingine.
Uko sahihi kabisa; watu wengi waliochaguliwa Chadema mwaka 2015 ilikuwa ni kutokana na nguvu ya Lowassa, ambaye alikuwa amefanya kazi kwa miaka 10 kujenga network na wenyeviti wa CCM mikoni na wilayani; kura hizo nyingi walizopata CHADEMA zilikuwa za wana CCM. Hiyo ilikuwa ni tofauti sana na zile kura za 1995 na 2010 ambapo watu walikuwa na hamasa kubwa ya mabadiliko.

Sasa hivi Lowassa kaamua kustaafu ndani ya CCM, chadema ina hali ngumu sana kupata kura kama zile za 2015; wenye nafuu hapa ni huenda ACT kwenye viti vya Pemba; lakini kwa upande wa kusini ambako pia wamewekeza sana wanaweza wasiambulie kitu na Kiongozi wao naye akakosa kiti chake.

Ushauri wako ni sahihi sana, atulie yu abaki ndni ya CCM kwani hata akirudi CHADEMA hatapata mapoikezi mazuri, ila akibaki CCM anaweza kuwa kama mwenzake Mtatiro huko mbeleni. Halafu iwapo CHADEMA itambeza sana inaweza kuharakisha kwake kupata nafasi za kuteuliwa; ni afadhali CHADEMA isiweke neno lolote dhidi ya waliojiondoa. Kuna sababu nyingi za kuamini kuwa CCM itashinda urais kwa kura nyingi sana na viti vingi sana vya ubunge kuliko 2015. Subiri October; ni takriban miezi miwili tu
 
Back
Top Bottom