Mwana JF aukwaa uongozi wa watanzania huko Uholanzi

Status
Not open for further replies.

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Napenda kuwataarifu kuwa mwana JF mwenzetu, Mzee Shughuli Bwana, amechaguliwa na watanzania wenzake wanaoishi nchini Uholanzi kuwa kiongozi wao. Mzee Shughuli Bwana alichaguliwa kwenye mkutano wa watanzania ulioitishwa na balozi wetu nchini Ubelgiji (unajumuisha pia nchi ya Uholanzi) uliofanyika Jumamosi 17 Mei 2007. Mzee Shughuli Bwana ataongoza kamati ya muda ya kuandaa katiba hadi uchaguzi kamili utakapofanyika ndani ya miezi mitatu.

Hii ni changamoto kwa Mzee Shughuli Bwana maana kapata nafasi nadra ya kutekeleza kwa vitendo yale ambayo amekuwa akiyahubiri sana hapa kuhusu uongozi na utawala bora, hasa kwa kuzingatia kuwa huyu bwana amekuwa yupo mbele sana katika kukivurumishia makombora chama tawala.

Hongera sana Mzee Shughuli Bwana; tunatarajia kuwa utakuwa mwakilishi mzuri wa principles za JF hasa katika kuukataa ubwenyenye na ufisadi!

Kila la heri.

PS: Hii sijui hapa ni mahala pake, kama sio basi MoDs mtanisamehe na kuipeleka panapohusika.
 
Napenda kuwataarifu kuwa mwana JF mwenzetu, Mzee Shughuli Bwana, amechaguliwa na watanzania wenzake wanaoishi nchini Uholanzi kuwa kiongozi wao.

Hii ni changamoto kwa Mzee Shughuli Bwana ... hasa kwa kuzingatia kuwa huyu bwana amekuwa yupo mbele sana katika kukivurumishia makombora chama tawala.

Hongera sana Mzee Shughuli Bwana;
Hongera Mzee Shughuli Bwana, aidha kwako kamanda Kitila ili kuwa kiongozi bora lazima uwe shujaa wa kurusha makombora kwa chama tawala?
 
Aidha kwako kamanda Kitila ili kuwa kiongozi bora lazima uwe shujaa wa kurusha makombora kwa chama tawala?

Ahaaaa haaa, mimi sijasema hivyo lakini, au nimesema? Nilichoeleza ni wasifu tu wa huyu bwana kwa jinsi ninavyomsoma hapa JF!
 
Napenda kuwataarifu kuwa mwana JF mwenzetu, Mzee Shughuli Bwana, amechaguliwa na watanzania wenzake wanaoishi nchini Uholanzi kuwa kiongozi wao. Mzee Shughuli Bwana alichaguliwa kwenye mkutano wa watanzania ulioitishwa na balozi wetu nchini Ubelgiji (unajumuisha pia nchi ya Uholanzi) uliofanyika Jumamosi 17 Mei 2007. Mzee Shughuli Bwana ataongoza kamati ya muda ya kuandaa katiba hadi uchaguzi kamili utakapofanyika ndani ya miezi mitatu.

Hii ni changamoto kwa Mzee Shughuli Bwana maana kapata nafasi nadra ya kutekeleza kwa vitendo yale ambayo amekuwa akiyahubiri sana hapa kuhusu uongozi na utawala bora, hasa kwa kuzingatia kuwa huyu bwana amekuwa yupo mbele sana katika kukivurumishia makombora chama tawala.

Hongera sana Mzee Shughuli Bwana; tunatarajia kuwa utakuwa mwakilishi mzuri wa principles za JF hasa katika kuukataa ubwenyenye na ufisadi!

Kila la heri.

PS: Hii sijui hapa ni mahala pake, kama sio basi MoDs mtanisamehe na kuipeleka panapohusika.

Napenda kumpongeza mwan JF mwenzetu. Ninaamini kabisa Uholanzi hakutakuwa na 'upuuzi' wa UK wa kufungua matawi ya vyama. Watanzania wanahitaji umoja zaidi kuliko kujigawa kivyama.

Nimefurahishwa sana na wenzetu wa US ambao mambo ya vyama hawana isipokuwa wanautana kama Watanzania.

Uholanzi tunatarajia makubwa sana kwenu kwani Uholanzi ni 'strategic country, kwa Tanzania. Watalii wameongezeka sana na biashara ya maua imekua sana.

Kila la kheri Watanzania wa Uholanzi
 
PS: Hii sijui hapa ni mahala pake, kama sio basi MoDs mtanisamehe na kuipeleka panapohusika.
Kitila, it's OK ikiwa hapa kwa muda lakini nadhani ulikokosea tu ni kuandika nick yake ya JF. Manake posts zake zaweza kufatiliwa na wengi na huenda wakapata mwanya wa kuhoja baadhi ya statements zake. Kama ungeandika jina lake halisi tu basi wengi wangebakia kujiuliza hutumia jina gani JF? Na hiyo ndiyo siri ya kuwa nyuma ya nickname. Kama hiyo nick atumiayo JF ndilo jina lake basi shukrani kwa kutupasha mpya hii.

BTW: Congrats Mzeeshughuli Bwana
 
JF ni kama chama cha upinzani machoni mwa chama tawala na serekali yake. Napata hisia kwamba Bw. Mlay atapata some few phone calls toka kwa 'wakubwa' na kupewa maelekezo fulani kuhusiana na uchaguzi huu, lets wait and see.
 
Napenda kumpongeza mwan JF mwenzetu. Ninaamini kabisa Uholanzi hakutakuwa na 'upuuzi' wa UK wa kufungua matawi ya vyama. Watanzania wanahitaji umoja zaidi kuliko kujigawa kivyama.

Nasikia balozi wa huko amekataa kabisa ujinga wa kujiingiza kwenye biashara ya kufungua matawi. Amesikika akisema kuwa wanaotaka kufungua matawi waende Tanzania nyumbani huko ndiko kuliko na wanachama. It looks like kwenye utawala huu bado kuna watu wanaoweza kufikiri beyond ukada!
 
Kitila, it's OK ikiwa hapa kwa muda lakini nadhani ulikokosea tu ni kuandika nick yake ya JF. Manake posts zake zaweza kufatiliwa na wengi na huenda wakapata mwanya wa kuhoja baadhi ya statements zake. Kama ungeandika jina lake halisi tu basi wengi wangebakia kujiuliza hutumia jina gani JF? Na hiyo ndiyo siri ya kuwa nyuma ya nickname. Kama hiyo nick atumiayo JF ndilo jina lake basi shukrani kwa kutupasha mpya hii.

You are right. Hata hivyo nilim-consult kabla akanipa go ahead nitumie jina lake la hapa. Thanks.
 
nami naungana na wengine kwa kumpongeza mkuu kiongozi mpya wa watz wa uholanzi. lakini tuzingatie angalizo la zitto. kuanzisha affiliation za vyama ni kuleta divisive tendencies zisizoleta msaada wakati sisi tunawategemea wajiunge pamoja waangalie namna bora zaidi ya kuremit their funds home kusaidia investments.
 
Mimi pia naomba nimpongeze.

Kwasababu ni wa muda tu hatuna shaka naye:) Sisi CCM hata mkitupinga vipi hamtuwezi!

Aisee Mzee Shughuli bwana tutaftane basi, kama huna simu tumia email.

Hongera sana.
 
Hongera Mzee Shug......., endeleza libeneke kwa maendeleo ya wenzetu huko majuu.... Kumbuka kuendelea kumkoma nyani Gila......
 
big up mzee shughuri bwana...
wahenga wanasema "mwanzo wa kumi ni moja" so tunaimani iko siku utapata cheo kikubwa zaidi ya hicho.
 
Mimi pia naomba nimpongeze.

Kwasababu ni wa muda tu hatuna shaka naye:) Sisi CCM hata mkitupinga vipi hamtuwezi!

Aisee Mzee Shughuli bwana tutaftane basi, kama huna simu tumia email.

Hongera sana.

Mkuu,

Unataka kumwajiri mara hii kwanini awasiliane na wewe.

Hongera mkuu, tunagitaji kuonyesha kuwa hatupigi kelele tu ila tukipata nafasi tunafanya kwa matendo yale tunayoyahubiri.
 
Hongera sana mkuu.Naona sasa mabadiliko yanaanza.Naamini kabisi hata chaguzi zijazo za huko nyumbani wanaJF wengi sana wataenda kuwakilisha fikra za hapa.

Keep it up mkuu,Cheo ni Dhamana
 
Hongera Mzee Shughuli Bwana. Huu ndio mwanzo, tuendeleza fikra za kuleta mapinduzi ya kimaendeleo kwa watanzania.
 
Mimi napenda kumpongeza Mzee huyu .Kweli huyu mtu siamini kama hatafanya yale ya aliyosema Zitto .Watanzania we need to come together for our Nation.Hakuna siasa kwenye vyama vyetu.

Nimepata Statement ya Balozi
Alikuwa Firm na Umoja wa Watanzania .He stayed focused on giving Tanzanians opportunities za ku explore Dunia.Balozi anasema hajali wewe ni Mzamiaji ama nani as long as wewe ni Mtanzania basi yeye yuko nyuma.Hawa ni baadhi ya watendaji wachache wa Serikali ambao huwa wanajua kwa nini sisi ni Tanzania na kujivuna kuitwa Watanzania .

Aliwapa moyo Watanzania wa kada zote kusimama imara na ku fight maisha lakini wakumbuke Tanzania kwa namna moja ama nyingine .

Mzeeshughuli hana mambo ya kisiasa .Wengi wanamjua amekuwa akisimamia haki nandiyo maana pamoja na Nabii kuja hapa akasema uongo juu ya huyu bwana lakini Nabii kaabika sasa kwa jinsi watanzania wenzake wanavyuo mwamini huyu mtu .

Siku za juzi kati maneno yalizuka hapa .Huyu mtu akashambuliwa sana kwamba anakula na konshula na Nabii akasema ukileta Uchaguiz hatapita .Kwa mshangao Watanzania hawa wanamwamini huyu mtu maana huwa hana unafiki wala vyama .Ana wajali Watanzania .Hata kama ni mwana JF hapa nimesoma mambo yake machache sana .

Hongera tena na wekeni misingi ya Kitanzania kwa Tanzania na watanzania wote .
 
Napenda kumpongeza mwan JF mwenzetu. Ninaamini kabisa Uholanzi hakutakuwa na 'upuuzi' wa UK wa kufungua matawi ya vyama. Watanzania wanahitaji umoja zaidi kuliko kujigawa kivyama.

Nimefurahishwa sana na wenzetu wa US ambao mambo ya vyama hawana isipokuwa wanautana kama Watanzania.

Uholanzi tunatarajia makubwa sana kwenu kwani Uholanzi ni 'strategic country, kwa Tanzania. Watalii wameongezeka sana na biashara ya maua imekua sana.

Kila la kheri Watanzania wa Uholanzi

Kweli kabisa Zitto,

Hapa US wamejaribu sana lakini wameshindwa. Hapa hakuna matawi ya vyama (ikiwemo CHADEMA) na hata wewe mwenyewe umeona kwenye mkutano wako na watanzania watu wakijadili mambo ya nchi na sio ya vyama.

CCM wanajaribu sana kuanzisha matawi yao hapa na wameshindwa. Labda wakianza kuanzisha matawi ya mtu mmoja na familia yake.
 
Nchi pekee yenye wapuuzi ni UK na huko Asia .Watu wenye uchungu na Nchi kwenye umoja wata angalia maslahi ya Nchi na si Vyama .Kila mmoja ana Chama chake na Umoja wa Watanzania ni wa wote .Above all nasikia Balozi Mlay si kama Mwanaidi .Mlya yeye Tanzania mbele na si Vyama .Pale Ubalozini kulikiuwa na mtu anaitwa Zoka na sasa karudi TZ yuko kweney Usalama ni mtu mkubwa sana kule Usalama ndiye alikuwa anU CCM hadi Ubalozini .Lakini mbali na hapo watu wanachapa kazi hakuna Vyama bali Nchi .
 
Asanteni sana Watanzania wenzangu.
Wenzangu wa hapa Hollamd wameniamini kwa sauti moja kubwa kabisa hata nikashangaa.Nikajiuliza niliwahi kuchaguliwa hapa hapa na ndugu Nabii kwamba sichaguliki nk .Lakini wanao jua jinsi nilivyo firm kwa Utanzania na kuwatetea Watanzania kuanzia kwa Mzungu hadi Ubalozini kwetu basi wamenipa heshima ya kuandaa kitu hiki kikubwa .Niliwaahidi wao na nyie wote kwamba sala na imani kwangu lazima niwalipe kwa kazi .Hakuna vyama hapa .Sisi ni Watanzania .Balozi Mlay alisema kwa kauli ambayo nakubaliana naye .Tuangalie maendeleo yetu na Tanzania na heshima yetu na Tanzania .

Kama nitakuwa Mwenyekiti rasmi nasema nitataka UK ni majirani wajue na wasikie na wajifunze .

Asanteni kwa sala na nia ni Kuibeba Tanzania na kuijenga Tanzania .

Mungu Ibariki Tanzania .
 
..hongera sana Mzee Shughuli Bwana.

NB:

..hii tabia ya kuwa na matawi ya vyama vya siasa ughaibuni imeanza na CUF.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom