Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Umebakia mwezi kama mmoja tu kabla ya kikao cha Bajeti hakijaanza ambapo viongozi wa kitaifa wengi watakuwa wamebanwa Dodoma; je nini kitaendelea wakati huo? Najiuliza mwamko huu yaweza kuwa umetangulia mwendo wa viongozi wa kitaifa - yaani wananchi wameamka na wanatangulia wao kuleta mabadiliko?
Swali la msingi ambalo linahitaji fikara zaidi ni ninihutokea baada ya maandamano na watu kurudisha kadi na shangwe na nyimbo za kufurahia? Nini hutokea baada ya viongozi wa kitaifa kuja na kuondoka; wakifanya mikutano yenye hamasa kubwa? Nini kimetokea Kiteto, Biharamulo, Buchosa, Tarime, Mwanza, Arusha, Songea, Mbeya, Iringa, Mbozi, Magu, Kirumba, Kiwira na kwingine huko kote? Baada ya kurudisha kadi na baada ya viongozi wa kitaifa kuondoka nani anaangalia hawa ambao 'wamekata shauri' kuikataa CCM na kukubali CDM kuwa tumaini leo?
Je CDM inayo miundo mbinu ya kutosha na ya kisasa ya kudumisha (sustain) mwamko huu kabla ya CCM hawajaanza counter attack - na kweli inakuja? Ikumbukwe kuwa baraza la mawaziri lilivyobadilishwa kimsingi limeweka makada mahiri wa chama kwenye nafasi nyeti. Ukiangalia wizara wote ambazo watu wake wamebadilishwa zote zimewekwa makada wa chama cha Mapinduzi kwa kile ambacho nakiita ni 'strategic preparation before war". Ni sawasawa na vikosi vya majeshi vinavyo amass kwenye eneo kabla ya kuleta mashambulizi.
Ninachoweza kukiona kutoka mbali ni kujipanga huku kwa vikosi vya CCM chini ya makamanda wapya na watakapoanza kurudisha majibu kuna watakutwa off guard. Mabadiliko ya Sektretariati ya CCM yanayotarajiwa kuja wiki ijayo utakuwa ni mwendelezo ya kujipanga huku na CDM kama wasipoangalia watajikuta wanajibu (react) na kulazimishwa kwenda kwenye kujitetea (defensive positions).
CCM watakapoanza kujibu mashambulizi hakutakuwa na huruma; hata mtandao wetu huu wa JF na mfumo wake wa kufanya kazi utakiona cha moto kwani watawala hawatoacha waende kwenye uchaguzi mwingine mkuu mitandao kama hii ikiwa kama ilivyokuwa kabla ya 2010. Hili nina UHAKIKA nalo wa kutosha. CDM ikitegemea nguvu ya wananchi tu kuisukuma inaweza - isipoangalia - kujikuta ikiwa imebanwa katika kuzunguka 'mlima huu'.
CDM ifanye nini basi? au isubiri liwalo na liwe kwa sababu 'wananchi wanaipenda'?