Mwambieni Shaka A Shaka atulie, kazi yake siyo kumtetea na kumsemea Rais Samia

G4N

JF-Expert Member
Apr 6, 2014
1,386
3,387
Shaka A. Shaka tangu amepewa nafasi hiyo amekuwa bize kujibu kila mashambulizi yanayoelekezwa ama kwa rais SSH moja kwa moja au kwa serikali yake.

Jana baada ya BBC swahili kurusha maoni ya J. J . Mnyika kuhusu kauli ya rais SSH wakati akihojiwa na chombo hicho hicho mara tukaona Shaka A. Shaka akijibu mashambulizi.

Siku chache zilozopita tuliona Shaka akimuonya askofu Gwajima baada ya kutoa msimamo wake kuwa chanjo ya korona haifai.

Kwa kufanya hivi, wajuvi na wachambuzi wa Mambo wanasema Shaka A. Shaka anaibagaza na kupwaya ktk kazi yake.

Ikumbukwe kuwa kazi ya kuisemea serikali iko mikononi mwa Msigwa.

Shaka A. Shaka aache mihemko, atulize boli maana kiwanja ni kidogo.
 
Shaka nafasi inayomfaa ni kusimamia usafi wa vyoo vya stend ili afiti kutoa matamko walio kunya pembeni.
 
Huyu mashaka mpuuzeni wala msimjibu kitu na ndio dawa yake ,akiropoka mnamnyamazia kimyah mnapiga sunsumia yeye mnamwacha anacheza tu maana hawezi kucheza koboka.
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Back
Top Bottom