Mwambalaswa naye pressure inapanda

Mkulima

JF-Expert Member
Feb 4, 2007
1,034
1,022
Mheshimiwa naona naye pressure imeanza kupanda na kushuka. Ukiona mbunge anakuja na madai mazito kama hayo bila kutaja majina jua ni yale yale ya kukalia kuti kavu, anataka kutumia neno ufisadi kudanganya wananchi ili kujiokoa. Kama ana ushahidi si aende polisi au mahakamani kuwataja hao wanaomwaga hizo pesa.

Mheshimiwa Mwambalaswa, kama una uhakika na madai yako, si wataje wanaosambaza pesa? Vinginevyo na wewe wapelekee wananchi zile pesa za posho mbili wakafaidi maana CCM wote mnafanana tu.

Mwanakatwe naye, hiyo ni hoja nzito au tuhuma (madai) nzito? Hawa waandishi wetu wa kwenye miembe balaa tupu.
Mbunge wa CCM: Mafisadi wamemwaga 60m/- jimboni
Na Thobias Mwanakatwe



28th December 2009




headline_bullet.jpg
Asema lengo ni kutaka kumng`oa 2010



Mwambalaswa.jpg

Mbunge wa Lupa CCM wilayani Chunya, Victor Mwambalaswa



Mbunge wa Lupa CCM wilayani Chunya, Victor Mwambalaswa, ameibuka na hoja nzito na kudai kuwa mtandao wa mafisadi umejipenyeza jimboni mwake kwa kusambaza fedha chafu zaidi ya Sh. milioni 60 kwa lengo la kutaka kumng'oa Uchaguzi Mkuu mwakani.

Mbunge huyo alitoa madai hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, kuelezea mambo aliyokutana nayo wakati yupo kwenye ziara ya kutembelea wapiga kura wake jimboni.
Mwambalaswa alisema katika ziara yake alibaini kuwa zaidi ya Sh. milioni 60 zimesambazwa katika vijiji vya jimbo la Lupa kwa lengo la kushawishi wananchi wasimchague mwakani.

Kwa mujibu wa Mwambalaswa, fedha hizo ambazo ana imani zimetolewa na mtandao wa mafisadi, zinasambazwa na mawakala wa mafisadi, wakiwemo watu wanaotaka kugombea ubunge jimboni humo mwakani.

Mwambalaswa alisema kutokana na fedha hizo kugawiwa ovyo vijijini, wananchi wameingiwa na hofu kubwa na kuhoji kama watu hao wanaozisambaza wana lengo zuri kwenye jimbo hilo kwani iwapo watakosa ubunge nini hatma kwa wananchi watakaokuwa wamepewa mamilioni hayo.

Mbunge huyo ambaye hakutaka kuweka wazi katika suala hilo, alisema fedha hizo chafu zimeletwa katika jimbo la Lupa kutoka kampuni moja ya ujenzi iliyopo mkoani Mwanza na kwamba uthibitisho wa kusambazwa kwa mamilioni hayo ameupata kutoka kwa wananchi ambao wamegawiwa.

Mwambalaswa alisema hata hivyo, anashangaa mafisadi kusambaza fedha hizo wakati yeye (Mwambalaswa) hajawahi kuwashambulia mafisadi hata siku moja.

''Mimi sijawahi kuwashambulia mafisadi lakini inashangaza nimekuta jimboni mwangu wamesambaza mamilioni,' 'alisema.
Alisema hata hivyo, hatishiki na mafisadi kumwaga fedha hizo na kuwataka wananchi kukaa mkao wa kula mamilioni hayo ila wajiulize wanaotoa fedha hizo wanania gani na je, wasipochaguliwa hatma yao itakuwaje.

''Kama umeikosea jamii kwa bahati mbaya kwa matendo yako nenda kwa padre au kwa sheikh ukatubu lakini si kumshughulikia mwenzako kwa fedha,'' alisema.
 
Mheshimiwa naona naye pressure imeanza kupanda na kushuka. Ukiona mbunge anakuja na madai mazito kama hayo bila kutaja majina jua ni yale yale ya kukalia kuti kavu, anataka kutumia neno ufisadi kudanganya wananchi ili kujiokoa. Kama ana ushahidi si aende polisi au mahakamani kuwataja hao wanaomwaga hizo pesa.

Mheshimiwa Mwambalaswa, kama una uhakika na madai yako, si wataje wanaosambaza pesa? Vinginevyo na wewe wapelekee wananchi zile pesa za posho mbili wakafaidi maana CCM wote mnafanana tu.

Mwanakatwe naye, hiyo ni hoja nzito au tuhuma (madai) nzito? Hawa waandishi wetu wa kwenye miembe balaa tupu.
Kwa mwenye uwezo wa kutumikia wananchi wake.. na kama kweli anapendwa....... tumieni chochote hatang'olewa. Lakini ukishaona mtu anaanza kuhaha kwa maneno........ ujuwe ni debe tupu haliachi kelele.
 
Kwa mwenye uwezo wa kutumikia wananchi wake.. na kama kweli anapendwa....... tumieni chochote hatang'olewa. Lakini ukishaona mtu anaanza kuhaha kwa maneno........ ujuwe ni debe tupu haliachi kelele.

Tutasikia mengi sana mwaka huu. Hata wale waliokuwa wanashinda Dar badala ya majimboni kwao, dakika ya mejeruhi ndio wanaamkia majimboni na kuja na kelele za mafisadi.

Ukiwa mchapa kazi, hata mafisadi waje na pesa kiasi gani, naamini wananchi hawatakutema. Utaratibu wa sasa wa wanachama wote CCM kupiga kura, una walinda wabunge wachapa kazi maana sio rahisi fisadi kuhonga wananchi wote.
 
Tutasikia mengi sana mwaka huu. Hata wale waliokuwa wanashinda Dar badala ya majimboni kwao, dakika ya mejeruhi ndio wanaamkia majimboni na kuja na kelele za mafisadi.

Ukiwa mchapa kazi, hata mafisadi waje na pesa kiasi gani, naamini wananchi hawatakutema. Utaratibu wa sasa wa wanachama wote CCM kupiga kura, una walinda wabunge wachapa kazi maana sio rahisi fisadi kuhonga wananchi wote.

Kwani yeye mwenyewe alipataje huo ubunge?? Si aligawa mapesaa!! Sasa ashangaa nini fisadi wa chini chini
 
Hivi huyu Mbunge ana maana ganai anaposema yeye hajawahi kuwashambulia mafisadi lakini anashangaa wanaliwinda jimbo lake??

Huyu hakika kastahili kuwa mbunge, sijui aliupataje.

Nafikiri TZ corruption na ufisadi usha kuwa part of our culture!! Kama ni kweli anafikiri wananchi hawapendi wamwaga pesa sasa yeye anaogopa nini?? Na kwa yeye mwenyewe hayuko mstari wa mbele kuwapiga vita mafisadi na ameamua kusema hadahrani na kutuonyesha kuwa anawafahamu!! Hakika hafai huyu!!
 
Kulingana na sifa za mafisadi, hata siku moja hawawezi kuaminiana na pia mara nyingi ni waoga sana kuona mngwana fulani anatoa misaada kwa wapiga kura hata kama hawajatangaza kugombea. Sababu kubwa ni tabia ya wabunge wengi hasa mafisadi kuupata ubunge huo kwa kugawa takirima kwa wananchi. Hivyo presha itapanda sana na kushuka kwa watu wa namna hiyo kadri tunapoelekea uchaguzi mkuu.
 
Huyo nae fisadi tuu,aache kubabaisha watu.Halafu aliyemwambia kiti cha pale ni cha kwake nani?Kwani kalithishwa!Nami nitaenda hukohuko kugombea japo sina pesa za kifisadi lakini 80ml.zitanitosha kabisa kupata ubunge halafu nitawaalika wana jf wote mje kusherehekea ushindi wetu,te te teh
 
Wabunge wengine hawajui hata kilichowapeleka bungeni. Mwambalaswa anaposema yeye hajawahi kuwashambulia Mafisadi anamaanisha nini:
1. anataka mafisadi wamsamehe kwa vile hajawatendea kosa?
2. anataka wananchi wamwonee huruma?
3. kuwa yeye pia yuko upande wa mafisadi ndiyo maana bungeni hasemi kitu?
4. hata yeye alipata ubunge kwa njia hiyo hiyo ya kumwaga mamilioni?

Hajiamini kwa wapiga kula wake anawasiwasi kwa vile hajatekeleza ahadi alizotoa.Badala ya kutoa takwimu ya yale aliyoyafanya katika kipindi chake yeye anaanza kuomba huruma kwa wapiga kura wake, hii ni (weakness) dalili tosha kuwa hajafanya chochote.
Mbali na kulialia kwake wabunge wa aina hii hawafai kabisa kurudi bungeni.
 
Wana JF nawashauri muwe mnafanya research kabla ya kutoa comments zenu. Inaonyesha wengi mnachangia mada kwa kukurupuka. Majibu yenu hayajaniridhisha kabisa.
 
Wana JF nawashauri muwe mnafanya research kabla ya kutoa comments zenu. Inaonyesha wengi mnachangia mada kwa kukurupuka. Majibu yenu hayajaniridhisha kabisa.

JF haipo kuridhisha watu, kama unataka tuandike unachokipenda, utakuwa umekosea njia kuja JF.

Mwambalaswa hana lolote zaidi yua kuomba huruma ya wananchi. Naona hata kasalimu amri kwa mafisadi, akiombea apewe huruma.
 
Hawa watu wananitibua kweli; kama wameshindwa kufanya mambo ya maendeleo kwenye majimbo yao wanafikiri watachaguliwa kwa sababu wanalia lia na mafisadi? Nani aliwaambia kuwa wana hati miliki ya majimbo?
 
Hawa watu wananitibua kweli; kama wameshindwa kufanya mambo ya maendeleo kwenye majimbo yao wanafikiri watachaguliwa kwa sababu wanalia lia na mafisadi? Nani aliwaambia kuwa wana hati miliki ya majimbo?


Mwenyewe anasema yeye hajawahi "kuwashambulia" mafisadi sasa iweje wanamfuata fuata?. Kwa maneno mengine yeye hana tatizo watu kuliibia taifa muradi tu yeye abaki kuwa Mbunge!

Kazi kweli kweli...
 
Mwenyewe anasema yeye hajawahi "kuwashambulia" mafisadi sasa iweje wanamfuata fuata?. Kwa maneno mengine yeye hana tatizo watu kuliibia taifa muradi tu yeye abaki kuwa Mbunge!

Kazi kweli kweli...


nimeisoma hiyo kauli nimebakia kucheka ni sawa na mtoto anasema "miye sikumchokoza lakini yeye ndiye mchokozi"! Halafu kinachonitibua na hawa wote wanaojiita wapambanaji kuendelea kuwaambia watu "mafisadi wakileta hela kuleni, ila kura nipeni"!!
 
..Nsanzugwanko naye amekabwa koo na Dr.Gerald Mpango Askofu Mstaafu wa Anglican.
 
Kama sikosei huyo bwana alitumia all means...I mean all means....kumng'oa Mzee wa G55 Njelu Kasaka...sasa analialia nini?
 
Kama aliwawakilisha watu wake vizuri miaka mitano iliyopita sioni ni kwa nini awe na wasiwasi. Waache wamwage mahela na watu watamchagua yule anayewafaa kwa maendeleo yao. Kulalama maana yake anaujua udhaiu wake na wapinzani wake wakautumia mwanya wa udhaifu kumdondosha. Na ajisafishe kwa kuonyesha kwamba anawafaa na sio fisadi, akijipambanua na wenzake kwa vitendo na hoja. Vinginevyo hata yeye ni fisadi machoni mwa watu wake asipoeleweka.

Leka
 
Alitumia pesa kumblock CCM,babu akahamia CHADEMA akamblock na huko,akaenda CUF akaambiwa muda wa kurudisha form ukaisha na watu wa NEC....Mwambalaswa akawa mbunge bila kupigiwa kura...
 
sasa huyu analalamika nini ,wakati yeye muda wote yupo kinondoni as if ye ndio Idd Azan anabadili vikao tuu,mara Bamboo Bar mara Makuna,sasa kwa mwendo huu anataka kuwaambia nini wapiga kura wake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom