Mwalimu wa shule ya msingi Tunduru mkoani Ruvuma afikishwa Mahakamani kwa kumpa mimba Mwanafunzi wake.

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Mwalimu wa shule ya msingi katika kata ya Ligunga tarafa ya Matemanga wilaya Tunduru mkoani Ruvuma Rajabu Morisi amefikishwa katika Mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake na kumsababishia ujauzito.

Akisoma shauri hilo no 148/2017, mbele ya mlinzi wa amani hakimu wa Mahakama ya mwanzo itika Korosho mwendesha mashtaka wa Mahakama ya wilaya Inspekta Bosco Kilumbe amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo kati ya mwezi January na Mei mwaka huu katika muda usiojulikana baada ya kumrubuni mwanafunzi huyo.

Amesema kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria namba 130(1) na (2e) na namba 131 (1) na (2) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo amekana kosa hilo upelelezi bado unaendelea , mtuhumiwa yupo nje kwa dhamana, kesi hiyo itatajwa tena Mahakamani Agosti 28 mwaka huu.

Wakizungumzia tukio hilo nje ya Mahakama baadhi ya wananchi walikuwa na ujumbe huu kwa serikali. Kwa upande wake Mwenyekiti wa ulinzi na usalawa wa wilaya ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homela aliyetembelea shule hiyo amewahakikishia haya wananchi wake.


ITV
 
Mwalimu wa shule ya msingi katika kata ya Ligunga tarafa ya Matemanga wilaya Tunduru mkoani Ruvuma Rajabu Morisi amefikishwa katika Mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake na kumsababishia ujauzito.

Akisoma shauri hilo no 148/2017, mbele ya mlinzi wa amani hakimu wa Mahakama ya mwanzo itika Korosho mwendesha mashtaka wa Mahakama ya wilaya Inspekta Bosco Kilumbe amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo kati ya mwezi January na Mei mwaka huu katika muda usiojulikana baada ya kumrubuni mwanafunzi huyo.

Amesema kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria namba 130(1) na (2e) na namba 131 (1) na (2) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo amekana kosa hilo upelelezi bado unaendelea , mtuhumiwa yupo nje kwa dhamana, kesi hiyo itatajwa tena Mahakamani Agosti 28 mwaka huu.

Wakizungumzia tukio hilo nje ya Mahakama baadhi ya wananchi walikuwa na ujumbe huu kwa serikali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa ulinzi na usalawa wa wilaya ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homela aliyetembelea shule hiyo amewahakikishia haya wananchi wake.

Chanzo: ITV
 
Back
Top Bottom