Mwalimu Nyerere na vigezo vya uongozi kwa Mwanamke

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
"Tunaweza kumpatia uongozi na madaraka mwanaume mlevi, lakini hatuwezi kumpa madaraka kama hayo mwanamke akiwa mlevi" Mwl. J.K Nyerere

Mwalimu alimaanisha tunapotaka kutoa madaraka kwa wanawake lazima vigezo viwe tofauti na wanaume! Kwa wanawake vigezo vinakua vingi zaidi

Lakini mimi sijaona tofauti ya mwanamke mlevi na mwanaume mlevi. Kwanini iwe kosa na dhambi kubwa kuiamini jinsia moja na kuitweza nyingine ilhali kilevi na kulewa ni kukekule?

Kwani kinachohofiwa kitafanywa na kiongozi mlevi mwenye jinsia ya kike si ndio hichohicho anaweza kufanya kiongozi mlevi mwenye jinsia ya kiume?
 
He was a unique character nakushauri uachane naye ukimchimba sana utaumia, siyo rahisi kumuelewa, inalazimu usome au umsikilize zaidi ya mara tatu kwa maneno yaleyale na usiishie kumsikiliza tu, umtafakari kwa kina.
 
Nyerere hajaongea kwa bahati mbaya, ndo uhalisia wenyewe. Huwezi kulinganisha kichwa cha mwanaume na mwanamke hata siku moja, mambo ya gender yabaki huko huko beijing.
 
Nyerere hajaongea kwa bahati mbaya, ndo uhalisia wenyewe. Huwezi kulinganisha kichwa cha mwanaume na mwanamke hata siku moja, mambo ya gender yabaki huko huko beijing..
Kuna falsafa kubwa sana ndani yake. Mwanaume "anapoangusha gari" baada ya kukata network kwa pombe ni tofauti sana kashfa hiyo ikiwa kwa mwanamke
 
Back
Top Bottom