Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,779
- 18,746
kwanza kabisa nianze kwa kusema hakuna siasa zinazoua nchi kimaendeleo kama siasa za kujaribu kunufaisha wanyonge na kulazimisha usawa wa kiuchumi. Ila bahati mbaya kwa Africa, 'marais wa waonyonge' ndio wanaonekana ndio sahihi
Mfano akitokea Rais akaanza ku deal na matajiri, akachukua mfano viwanda vya Bakresa, Mo, azania n.k na kuvifanya vya serikali ambavyo vitakuwa vinazalisha na vinagawa maziwa, unga na bidhaa nyingine bure kwa wananchi, huyu Rais atashangiliwa na nchi nzima na Waafrica wengi watamuona mkombozi
Lakini bila kujua njia yake hii ya kuwapa dezo na vya bure wanyonge sio sustainable na baada ya miaka kadhaa viwanda vitafilisika
Na hii ndio mistake aliyofanya Nyerere na Magufuli
Wakati wa Nyerere utasikia baadhi ya watu wakisifu tulikuwa tunakunywa sijui maziwa, nyama za bure, tunasoma bure n.k
Lakini huu ubure huu ulitokana na serikali kutaifisha viwanda na ranchi za wawekezaji na kuua uchumi, na pia kuwajengea wananchi utamaduni mbaya wa kudhani serikali ndio baba wa kuwafanyia kila kitu na wao ni kuisujudu
Matokeo yake ni tabaka la watu wanaofikiri, wanaojenga uchumi kwa kuzalisha linafutwa na kujenga taifa la watu wasiofikiri sana, waoga na wanaotegemea kupewa vya bure serikali
Hili ndio taifa aliliacha Nyerere, kwa kujua ama makusudi. Tiafa kama hili haliwezi kupata maendeleo endelevu, bali kila kitu kitategemea serikali
Magufuli nae alikuwa akielekea huku huku, taifa ambalo Serikali ina nguvu kubwa kwenye uchumi, na wananchi wanaoisujudu, serikali inayopiga vita tabaka la kati na la juu ambao ndio wanaoendeleza nchi
Mfano akitokea Rais akaanza ku deal na matajiri, akachukua mfano viwanda vya Bakresa, Mo, azania n.k na kuvifanya vya serikali ambavyo vitakuwa vinazalisha na vinagawa maziwa, unga na bidhaa nyingine bure kwa wananchi, huyu Rais atashangiliwa na nchi nzima na Waafrica wengi watamuona mkombozi
Lakini bila kujua njia yake hii ya kuwapa dezo na vya bure wanyonge sio sustainable na baada ya miaka kadhaa viwanda vitafilisika
Na hii ndio mistake aliyofanya Nyerere na Magufuli
Wakati wa Nyerere utasikia baadhi ya watu wakisifu tulikuwa tunakunywa sijui maziwa, nyama za bure, tunasoma bure n.k
Lakini huu ubure huu ulitokana na serikali kutaifisha viwanda na ranchi za wawekezaji na kuua uchumi, na pia kuwajengea wananchi utamaduni mbaya wa kudhani serikali ndio baba wa kuwafanyia kila kitu na wao ni kuisujudu
Matokeo yake ni tabaka la watu wanaofikiri, wanaojenga uchumi kwa kuzalisha linafutwa na kujenga taifa la watu wasiofikiri sana, waoga na wanaotegemea kupewa vya bure serikali
Hili ndio taifa aliliacha Nyerere, kwa kujua ama makusudi. Tiafa kama hili haliwezi kupata maendeleo endelevu, bali kila kitu kitategemea serikali
Magufuli nae alikuwa akielekea huku huku, taifa ambalo Serikali ina nguvu kubwa kwenye uchumi, na wananchi wanaoisujudu, serikali inayopiga vita tabaka la kati na la juu ambao ndio wanaoendeleza nchi