Mwalimu Nyerere College Inahujumiwa!

Mizizi

JF-Expert Member
Mar 8, 2008
1,275
391
Kwa taarifa nilizozipata leo hii kutoka kwa wadau wa Mwalimu nyerere Memorial Academy ni za kusikitisha sana. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba, mambo haya yanafanywa na vijana, ambao tulitegemea wangeleta mabadiliko na kusahau ile kasumba iliyokuwa ikishusha hadhi ya baadhi ya vyuo mbali mbali hapa nchini! Kinachotokea Mwalimu Nyerere ni kwamba kuna baadhi ya walimu wamesahau wajibu wao wa kuwasimamia wanafunzi wao ili kufikia malengo yao ya kitaaluma na badala yake wamejigeuza miungu watu.

Haya yametokea hivi karibuni pale wanafunzi wa kada mbalimbali walipohitajika kuandika ripoti zao za tafiti mbalimbali kama utaratibu unavyoeleza. Kinyume na matarajio, baadhi ya wanafunzi hasa wa kike ambao wasimamizi wao ni wanaume vijana kukutana na vikwazo mbalimbali. Wengine walitakiwa kupeleka ripoti hizo nyumbani kwa walimu nyakati za usiku. Waliokataa kufanya hivyo wamefikia hatua mbaya, hata kukataliwa kupokelewa ripoti zao na hivyo kuwepo uwezekano wa kurudia mwaka! Cha kushangaza, ni kwamba, hawa wanaofanya haya wengine wamesoma ndani na nje ya nchi, na wameona ni jinsi gani huko walimu walivyo committed na helpful kwa wanafunzi wao kama wao walivyosaidiwa kwa hali ya juu. Cha ajabu ni kwanini wanaamua kuwafanyia ushenzi kama huu watanzania wenzao.

Kuna mwalimu mmoja baada ya kufanya upumbavu kwa mwanafunzi mke wa mtu, mumewe akaamua kutia timu chuoni, mwalimu alipolazimishwa kuipokea ripoti ya mwanafunzi na mkuu wake akamwambia yule mwanafunzi amwite mumewe wasaishe wote,mwanafunzi alipoambiwa vile akaamua kufikisha malalamiko kwa mkuu wa yule mwalimu, ndipo akabadilishiwa msimamizi, ndipo yule mwalimu wa awali akamfuata huyu mwalimu na kumpa maelekezo kwamba, ahakikishe yule mwanafunzi anarudia mwaka ama yeye anaunja urafiki nae.
Majina ya hawa walimu wote ninayo, na kuna mengi yaliyofanywa hapo chuoni, ikihitajika tutayaweka hapa.

Sasa najiuliza, haya mambo mbona hayafanani na falsafa ya Mwalimu kama chuo kilivyobeba jina lake? Ama ndio hujuma za makusudi kukihujumu chuo hiki kwa malengo maalumu?
 
Hao walimu kweli au ndo waliobebwa wakati wa taaluma zao vyuoni? hao wana tabia za kinyama kabisa hawafai ktk maendeleo ya taifa letu, hebu ifikie kipindi vyuo viwe katka hali ya upekee kama ngazi ya juu ya elimu kwa kutoa elimu bora bila ya unyanyasaji wa wale wanaosoma sasa, kweli hao walimu ni educated au schooled people?
Kwa taarifa nilizozipata leo hii kutoka kwa wadau wa Mwalimu nyerere Memorial Academy ni za kusikitisha sana. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba, mambo haya yanafanywa na vijana, ambao tulitegemea wangeleta mabadiliko na kusahau ile kasumba iliyokuwa ikishusha hadhi ya baadhi ya vyuo mbali mbali hapa nchini! Kinachotokea Mwalimu Nyerere ni kwamba kuna baadhi ya walimu wamesahau wajibu wao wa kuwasimamia wanafunzi wao ili kufikia malengo yao ya kitaaluma na badala yake wamejigeuza miungu watu.
Haya yametokea hivi karibuni pale wanafunzi wa kada mbalimbali walipohitajika kuandika ripoti zao za tafiti mbalimbali kama utaratibu unavyoeleza. Kinyume na matarajio, baadhi ya wanafunzi hasa wa kike ambao wasimamizi wao ni wanaume vijana kukutana na vikwazo mbalimbali. Wengine walitakiwa kupeleka ripoti hizo nyumbani kwa walimu nyakati za usiku. Waliokataa kufanya hivyo wamefikia hatua mbaya, hata kukataliwa kupokelewa ripoti zao na hivyo kuwepo uwezekano wa kurudia mwaka! Cha kushangaza, ni kwamba, hawa wanaofanya haya wengine wamesoma ndani na nje ya nchi, na wameona ni jinsi gani huko walimu walivyo committed na helpful kwa wanafunzi wao kama wao walivyosaidiwa kwa hali ya juu. Cha ajabu ni kwanini wanaamua kuwafanyia ushenzi kama huu watanzania wenzao.
Kuna mwalimu mmoja baada ya kufanya upumbavu kwa mwanafunzi mke wa mtu, mumewe akaamua kutia timu chuoni, mwalimu alipolazimishwa kuipokea ripoti ya mwanafunzi na mkuu wake akamwambia yule mwanafunzi amwite mumewe wasaishe wote,mwanafunzi alipoambiwa vile akaamua kufikisha malalamiko kwa mkuu wa yule mwalimu, ndipo akabadilishiwa msimamizi, ndipo yule mwalimu wa awali akamfuata huyu mwalimu na kumpa maelekezo kwamba, ahakikishe yule mwanafunzi anarudia mwaka ama yeye anaunja urafiki nae.
Majina ya hawa walimu wote ninayo, na kuna mengi yaliyofanywa hapo chuoni, ikihitajika tutayaweka hapa.
Sasa najiuliza, haya mambo mbona hayafanani na falsafa ya Mwalimu kama chuo kilivyobeba jina lake? Ama ndio hujuma za makusudi kukihujumu chuo hiki kwa malengo maalumu?
 
Cha kushangaza wanapoomba kazi, ukisoma barua zao na CV zao wanavyojieleza kwa ethics utapenda! Wanapopewa ofisi za umma wanafanya "uswahili" wao wa kijinga!
 
hayo malalamiko mtumie rais kwenye account yake facebook watashughulikiwa haraka iwezekanavyo.
 
Kweli inashangaza sana. Halafu 2nasema 2nataka kuwafikia Westeners. Kwa mtindo huu wa kukabidhiana degree za kitandani tutafika?
 
Kwa taarifa nilizozipata leo hii kutoka kwa wadau wa Mwalimu nyerere Memorial Academy ni za kusikitisha sana. Cha kusikitisha zaidi ni kwamba, mambo haya yanafanywa na vijana, ambao tulitegemea wangeleta mabadiliko na kusahau ile kasumba iliyokuwa ikishusha hadhi ya baadhi ya vyuo mbali mbali hapa nchini! Kinachotokea Mwalimu Nyerere ni kwamba kuna baadhi ya walimu wamesahau wajibu wao wa kuwasimamia wanafunzi wao ili kufikia malengo yao ya kitaaluma na badala yake wamejigeuza miungu watu.
Haya yametokea hivi karibuni pale wanafunzi wa kada mbalimbali walipohitajika kuandika ripoti zao za tafiti mbalimbali kama utaratibu unavyoeleza. Kinyume na matarajio, baadhi ya wanafunzi hasa wa kike ambao wasimamizi wao ni wanaume vijana kukutana na vikwazo mbalimbali. Wengine walitakiwa kupeleka ripoti hizo nyumbani kwa walimu nyakati za usiku. Waliokataa kufanya hivyo wamefikia hatua mbaya, hata kukataliwa kupokelewa ripoti zao na hivyo kuwepo uwezekano wa kurudia mwaka! Cha kushangaza, ni kwamba, hawa wanaofanya haya wengine wamesoma ndani na nje ya nchi, na wameona ni jinsi gani huko walimu walivyo committed na helpful kwa wanafunzi wao kama wao walivyosaidiwa kwa hali ya juu. Cha ajabu ni kwanini wanaamua kuwafanyia ushenzi kama huu watanzania wenzao.
Kuna mwalimu mmoja baada ya kufanya upumbavu kwa mwanafunzi mke wa mtu, mumewe akaamua kutia timu chuoni, mwalimu alipolazimishwa kuipokea ripoti ya mwanafunzi na mkuu wake akamwambia yule mwanafunzi amwite mumewe wasaishe wote,mwanafunzi alipoambiwa vile akaamua kufikisha malalamiko kwa mkuu wa yule mwalimu, ndipo akabadilishiwa msimamizi, ndipo yule mwalimu wa awali akamfuata huyu mwalimu na kumpa maelekezo kwamba, ahakikishe yule mwanafunzi anarudia mwaka ama yeye anaunja urafiki nae.
Majina ya hawa walimu wote ninayo, na kuna mengi yaliyofanywa hapo chuoni, ikihitajika tutayaweka hapa.
Sasa najiuliza, haya mambo mbona hayafanani na falsafa ya Mwalimu kama chuo kilivyobeba jina lake? Ama ndio hujuma za makusudi kukihujumu chuo hiki kwa malengo maalumu?


Mie nadhani inahitajika!! hebu mwaga hapa hayo majina mkuu! u r a great thinker mkuu,ain't u?
 
Mtoa mada uliyosema ni kweli. Yupo mwalimu mmoja anapenda kuwakomalia sana wake za watu, haswa wanaotoka mikoani. Na yeyote hata kama hajaolewa. Anawabana sana ktk research work, jina limenitoka, nilikuonyeshwa akiwa ndani ya gari ya jamaa yake maeneo ya Posta.

Wanatumia Mkendo Motel, halafu kuna mmoja anatajwa kuwapeleka kwenye Hotel moja ipo maeneo ya Kariakoo karibu na Mtaa wa Lumumba.
 
Inabidi muweke majina yao hadharani ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao. Kwanini watanzania mnapenda kuficha ficha mambo? Hao wataendelea kudidimiza elimu pamoja na kuchafua sifa nzuri za chuo.
 
Hili ni tatizo kubwa.Walimu wa vyuo hawana ethics za ualimu.Wanapata kazi kwa sababu wana GPA kubwa.Hakuna kozi wanazopelekwa kusomea ualimu pamoja na ethics zake ndiyo maana mambo kama haya yanajitokeza.
 
Hivi hapo Chuoni hakuna Serikali ya Wanafunzi? Kwa nini watu wawakubalie hao mafisadi badala ya kutumia vyombo vya kutafuta haki? Hakuna regulations dhidi ya sexual harassment? Kuwataja hapa JF yatakuwa kama majungu tu. Kama wahusika ni serious wafanye mipango ili hao watu wakamatwe ready-handed in action. Hili linawezekana. Lakini vile vile kuna wanawake wavivu au wasiojiweza (darasani) wakifeli wanasingizia eti walimu waliwataka kimapenzi wakawakatalia. Chunguzeni pande zote mbili.
 
Mhusiika atoe data ambazo zitasaidia kulifanyia jambo hili. Kuongea kwa mafumbo hakusaidii
 
ainisha majina yao jamvin humu, hawafai kwa lolote hata jina la kuwapa sina.Majina tu
 
Hivi hapo Chuoni hakuna Serikali ya Wanafunzi? Kwa nini watu wawakubalie hao mafisadi badala ya kutumia vyombo vya kutafuta haki? Hakuna regulations dhidi ya sexual harassment? Kuwataja hapa JF yatakuwa kama majungu tu. Kama wahusika ni serious wafanye mipango ili hao watu wakamatwe ready-handed in action. Hili linawezekana. Lakini vile vile kuna wanawake wavivu au wasiojiweza (darasani) wakifeli wanasingizia eti walimu waliwataka kimapenzi wakawakatalia. Chunguzeni pande zote mbili.

Mkuu ingekuwa hivyo ulivyofikiria endapo matokeo yangekuwa yametoka na wahusika wamefeli mitihani yao!
Nilichokielezea hapa, hata matokeo hayajatoka, kwa hiyo sidhani kama inaweza kuwa ni uvivu wa akina dada kutokamilisha repoti ndio wamesingizia hivyo kwa hili, japokuwa siwezi pingana moja kwa moja kwamba baadhi ya wanawake wanatumia njia za kujirahisisha kupata wepesi kwenye mambo ya elimu. Ila haimaanishi pia kwamba hakuna walimu wenye tabia chafu kama hizi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom