Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwaselela iliyopo katika Kata ya Iwindi Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Alinani Mwakifuna (59) anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kwa tuhuma za kumbaka mjukuu wake mwenye umri wa miaka 15.
Kamanda Ulrich Matei
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei amesema mwalimu huyo alimbaka mjukuu wake ambaye jina limehifadhiwa Februari 16 mwaka huu akiwa naye shambani.
Akitoa taarifa hiyo, Kamanda Mtei amepinga kuhusisha tukio hilo na masuala ya kishirikina.
Katika tukio lingine Kamanda Matei amesema kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Samwel Msukila (22) mkazi wa Mbeya, anashikiliwa na Jeshi hilo kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka tisa.
Kamanda Matei alisisitiza kuwa matukio yote mawili na mengine ambayo yamekuwa yakitokea mkoani humo hayahusiani na imani za kishirikina na badala yake ni tamaa za kimwili za wahusika.
Itv
Kamanda Ulrich Matei
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei amesema mwalimu huyo alimbaka mjukuu wake ambaye jina limehifadhiwa Februari 16 mwaka huu akiwa naye shambani.
Akitoa taarifa hiyo, Kamanda Mtei amepinga kuhusisha tukio hilo na masuala ya kishirikina.
Katika tukio lingine Kamanda Matei amesema kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Samwel Msukila (22) mkazi wa Mbeya, anashikiliwa na Jeshi hilo kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka tisa.
Kamanda Matei alisisitiza kuwa matukio yote mawili na mengine ambayo yamekuwa yakitokea mkoani humo hayahusiani na imani za kishirikina na badala yake ni tamaa za kimwili za wahusika.
Itv