Mchambuzi nguli wa habari ya michezo maarufu kama mwalimu Kashasha amefariki dunia hivi punde alipokuwa amelazwa hospitali ya Kairuki.
Chanzo mimi mwenyewe niko eneo la tukio.
----
Mchambuzi nguli wa soka nchini Tanzania, Mwalimu Alex Kashasha amefariki dunia leo Agosti 19, 2021 akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Kairuki Jijini Dar es Salaam.
Mwalimu Kashasha alizaliwa mwaka 1957, mpaka umauti unamkuta alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC).
Mwalimu kashasha alikuwa mwalimu wa michezo katika vyuo mbalimbali na baadae akawa mchambuzi wa soka katika television ya taifa .
Mwalimu kashasha alikuwa anasikika katika kipindi cha michezo cha TBC FM.