kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MWALIMU wa shule ya Msingi Mtwivilla mjini Iringa, Alexander Kapolesya, anadaiwa kumuua mwalimu mwenzake, Ernest Komba (48), wa shule hiyo hiyo wakati wakimgombea mhudumu wa baa (Bar Maid).
Walimu hao walikuwa wakigombea penzi la mwanamke huyo aliyekuwa akiwahudumia kwenye moja ya sehemu zinazouza vinywaji katika eneo hilo la Mtwivilla.
Inadaiwa kwamba, mwalimu Komba alikufa baada ya Kapolesya kumpiga na kitu kizito kichwani.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa na jirani na eneo la tukio, walimu hao waligombana jana saa 2.30 usiku katika baa hiyo.
Habari kutoka katika eneo la tukio zinadai kuwa, wakati walimu hao wakinywa pombe kila mmoja kwa wakati wake alikuwa akiongea na mwanamke huyo ili aondoke naye kwa ajili ya kwenda kufanya ngono.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, amemtaja mwalimu Komba kuwa ndiye aliyempiga mwenzake hadi kufa.
Mangalla amesema, baada ya tukio hilo, Mwalimu Kapolesya alijaribu kukimbilia mafichoni lakini polisi walibaini alipokuwa wakamkamata.
Alidhani angeweza kutoroka, lakini hakufanikiwa kwani alikamatwa muda mfupi baadaye katika maficho yake aliyoyafanya huko huko Mtwivilla, amesema Kamanda Mangalla.
Amesema, wakati uchunguzi unaendelea, mwalimu huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya mauaji.
Kamanda Mangalla amesema,jina la mwanamke aliyesababisha walimu hao wagombane halijapatikana, hajulikani alipo, polisi wanamtafuta.
Walimu hao walikuwa wakigombea penzi la mwanamke huyo aliyekuwa akiwahudumia kwenye moja ya sehemu zinazouza vinywaji katika eneo hilo la Mtwivilla.
Inadaiwa kwamba, mwalimu Komba alikufa baada ya Kapolesya kumpiga na kitu kizito kichwani.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa na jirani na eneo la tukio, walimu hao waligombana jana saa 2.30 usiku katika baa hiyo.
Habari kutoka katika eneo la tukio zinadai kuwa, wakati walimu hao wakinywa pombe kila mmoja kwa wakati wake alikuwa akiongea na mwanamke huyo ili aondoke naye kwa ajili ya kwenda kufanya ngono.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, amemtaja mwalimu Komba kuwa ndiye aliyempiga mwenzake hadi kufa.
Mangalla amesema, baada ya tukio hilo, Mwalimu Kapolesya alijaribu kukimbilia mafichoni lakini polisi walibaini alipokuwa wakamkamata.
Alidhani angeweza kutoroka, lakini hakufanikiwa kwani alikamatwa muda mfupi baadaye katika maficho yake aliyoyafanya huko huko Mtwivilla, amesema Kamanda Mangalla.
Amesema, wakati uchunguzi unaendelea, mwalimu huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya mauaji.
Kamanda Mangalla amesema,jina la mwanamke aliyesababisha walimu hao wagombane halijapatikana, hajulikani alipo, polisi wanamtafuta.