Mwakyembe,peleka muswada bungeni kufuta mfumo wa vyama vingi vya siasa!!

iparamasa

JF-Expert Member
Nov 14, 2013
13,438
14,916
Historia iko wazi na haijawahi kukanushwa,Ccm waliukataa mfumo wa vyama Vingi na waliukubali kwa shinikizo la baba wa taifa...Mwalimu nyerere....ila nafsini mwao hawakuwa tayari!

Na hii imeendelea kujidhihiri kila rais anayekaa madarakani.
Kimsingi, hata nyerere aliwahi kulalamika kwamba kila kitu alichokipangilia na kukitolea hoja nchi hii,baada ya nyerere kutoka madarakani,Ccm walikitupa,sembuse vyama vingi!!
Baada ya uchaguzi vyama hufanya Kazi ya kujijenga kwa wananchi na kuwasiliana na wanachama na kutengeneza wanachama wapya.

Sasa vyama vya siasa vimezuiwa kutafuta wanachama wapya wala kutembelea waliopo na hata kufafanua kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara madhumuni ya kuanzishwa kwake.
Sasa vinataka kugeuzwa vyama vya kutafuta kura na si wanachama na wafuasi....kimsingi wanacham na wafuasi hutafutwa kabla ya uchaguzi kupitia mikutano ya hadhara na huwa nguzo ya chama wakati wa kampeni kwa kusimamia maslahi yake

Kwa kuwa vyama hivi vimekuwa kero kwao japo sheria ya kuvianzisha ilitungwa na bunge lililokuwa na wabunge 100% Ccm,basi namshauri mwakyembe waziri wa sheria kwamba,apeleke muswada(kama ana ubavu)akavifute kwa kuwa bunge hili asilimia mia wanaokaa ni Ccm baada ya ukawa kuwaachia ukumbi
 
Historia iko wazi na haijawahi kukanushwa,Ccm waliukataa mfumo wa vyama Vingi na waliukubali kwa shinikizo la baba wa taifa...Mwalimu nyerere....ila nafsini mwao hawakuwa tayari!

Na hii imeendelea kujidhihiri kila rais anayekaa madarakani.
Kimsingi, hata nyerere aliwahi kulalamika kwamba kila kitu alichokipangilia na kukitolea hoja nchi hii,baada ya nyerere kutoka madarakani,Ccm walikitupa,sembuse vyama vingi!!

Kwa kuwa vyama hivi vimekuwa kero kwao japo sheria ya kuvianzisha ilitungwa na bunge lililokuwa na wabunge 100% Ccm,basi namshauri mwakyembe waziri wa sheria kwamba,apeleke muswada(kama ana ubavu)akavifute kwa kuwa bunge hili asilimia mia wanaokaa ni Ccm baada ya ukawa kuwaachia ukumbi
kweli maana hapa kuna shida, lakini .................
 
Intelijensia ya itumiwe kulinda shughuli halali na sio kuzizuia....
 
Neno chama haliwezi kuwepo bila kuwepo wanachama,ndio maana lazima,kabla ya kusajili chama uwe na wanachama 200 kwa kila mikoa bara na visiwani, sasa kwa hiyo hata usajiliwa wa vyama umesitishwa? Utawapataje hao wanachama 200 bila mikutano ya hadhara
 
Kaona wamezubaa na wengine wanaomba ushirikiano na serikal.....may be out of this tutapata upinzani halisi,sio ule unaotaka nipe nikupe,wananchi wanaweza kuvuna faida as well as siasa za mageuzi,akina mbatia walikula rungu,wa sasa hivi mkwara kidogo wanajificha,
Zamani unakaa,unawasubiri waje Jangwani,siku hizi hata Meseji za watsap zinawakimbiza
 
Kama kweli ukombozi unatakika kupitia upinzani bsi cha msingi ni vyama vyote vya upinzani kutoshiriki uchaguzi mkuu 2020 bali namna nyingine itafutwe kuliko ya kupiga kura au kushiriki uchaguzi huo !!
 
Hana ubavu vyama vingi viko kisheria MKUU uwe unasoma katiba kwanza sio unakurupuka Iparamasa
 
Hana ubavu vyama vingi viko kisheria MKUU uwe unasoma katiba kwanza sio unakurupuka Iparamasa
Umekurupuka bila kusoma....nakusamehe kwa kuwa bado ni asubuhi labda mama watoto mnakurupushana akujali asubuhi
 
Kwa kweli huu uzi umegusa penyewe "HAKUNA MAENDELEO BILA UPINZANI"Tuangalie mf Marekani wanakinzana kwenye uchaguzi ukishapita kila chama na raia ana haki ya kutoa maoni yake
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom