stigajemwa
JF-Expert Member
- Nov 12, 2016
- 449
- 430
Salaam,
Kwa waliosahau; Lowasa amekuwa akitajwa sana na wapinzani wake kuwa ni fisadi namba moja nchini.
Mwanzo kabisa alitajwa na kambi ya chadema kuwa ni fisadi kwa kigezo chake cha kujiuzulu kutokana na kashifa ya richimond. Hivyo chadema na kundi lake wakazunguka nchi nzima wakitangaza kuwa Lowasa ni fisadi namba moja nchini na wakamworodhesha kwenye orodha waliyoiita list of shame.
Ufisadi wa Lowasa kwa chadema na kundi lake uliishia pale Lowasa alipojiunga nao na kisha kumteua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA.Kilichofuata ni chadema hao hao kuzunguka nchi nzima wakisema kuwa Lowasa si fisadi na wanaosema ni fisadi waende mahakamani au walete ushahidi. Kiufupi single ya ufisadi wa Lowasa kwa chadema iliishia hapo.
Wimbo wa ufisadi wa Lowasa ukahamia kwa ccm na kundi lake. Wao walimpachika ufisadi mara tu baada ya kuihama ccm na kujiunga chadema kisha kuteuliwa kuwa mgombea urais kupitia mwanvulj wa UKAWA.Toka hapo ccm nao wakaanza kumnanga Lowasa kama fisadi.
Wimbo huu kwa upande wa ccm umekuwa ukichagizwa na Dk Mwakyembe kama mwenyekiti wa kamati ya richmond ambaye amekuwa akijinasibu kuwa ana ushahidi wa kutosha ambao ulikuwa bado kutolewa na kamati yake.
Lakini single ya ufisadi wa Lowasa kwa ccm nayo imeishia mikononi kwa mwenyekiti wa ccm Taifa. Aambaye msimamo wake ndani ya chama huwa ndio msimamo wa chama. Na ktk msimamo huo mwenyekiti wa ccm, rais Magufuli alisema kuwa Lowasa ni MTU safi yaani hana makandokando.
Hivyo kwa msimamo huo wa mwenyekiti wa ccm Taifa, maana yake ccm na kundi lake nao kwa sasa wanakiri kuwa Lowasa si fisadi. Kwa mantiki hiyo single ya Lowasa ni fisadi imekufa rasmi kwa pande zote mbili, yaani kambi ya upinzani na chama tawala.
Mwisho kabisa, baada ya single ya ufisadi wa Lowasa Kwisha sasa tuangalie single mpya ambayo imeasisiwa na Makonda.
Yenyewe inahusu ukatili wa Lowasa wa kutelekeza mtoto na mama yake. Tutarajie wapinzani wake kuanza kumtangaza Lowasa kuwa si mwadilifu kwa kutelekeza mama na mtoto.
Aksante.
Kwa waliosahau; Lowasa amekuwa akitajwa sana na wapinzani wake kuwa ni fisadi namba moja nchini.
Mwanzo kabisa alitajwa na kambi ya chadema kuwa ni fisadi kwa kigezo chake cha kujiuzulu kutokana na kashifa ya richimond. Hivyo chadema na kundi lake wakazunguka nchi nzima wakitangaza kuwa Lowasa ni fisadi namba moja nchini na wakamworodhesha kwenye orodha waliyoiita list of shame.
Ufisadi wa Lowasa kwa chadema na kundi lake uliishia pale Lowasa alipojiunga nao na kisha kumteua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA.Kilichofuata ni chadema hao hao kuzunguka nchi nzima wakisema kuwa Lowasa si fisadi na wanaosema ni fisadi waende mahakamani au walete ushahidi. Kiufupi single ya ufisadi wa Lowasa kwa chadema iliishia hapo.
Wimbo wa ufisadi wa Lowasa ukahamia kwa ccm na kundi lake. Wao walimpachika ufisadi mara tu baada ya kuihama ccm na kujiunga chadema kisha kuteuliwa kuwa mgombea urais kupitia mwanvulj wa UKAWA.Toka hapo ccm nao wakaanza kumnanga Lowasa kama fisadi.
Wimbo huu kwa upande wa ccm umekuwa ukichagizwa na Dk Mwakyembe kama mwenyekiti wa kamati ya richmond ambaye amekuwa akijinasibu kuwa ana ushahidi wa kutosha ambao ulikuwa bado kutolewa na kamati yake.
Lakini single ya ufisadi wa Lowasa kwa ccm nayo imeishia mikononi kwa mwenyekiti wa ccm Taifa. Aambaye msimamo wake ndani ya chama huwa ndio msimamo wa chama. Na ktk msimamo huo mwenyekiti wa ccm, rais Magufuli alisema kuwa Lowasa ni MTU safi yaani hana makandokando.
Hivyo kwa msimamo huo wa mwenyekiti wa ccm Taifa, maana yake ccm na kundi lake nao kwa sasa wanakiri kuwa Lowasa si fisadi. Kwa mantiki hiyo single ya Lowasa ni fisadi imekufa rasmi kwa pande zote mbili, yaani kambi ya upinzani na chama tawala.
Mwisho kabisa, baada ya single ya ufisadi wa Lowasa Kwisha sasa tuangalie single mpya ambayo imeasisiwa na Makonda.
Yenyewe inahusu ukatili wa Lowasa wa kutelekeza mtoto na mama yake. Tutarajie wapinzani wake kuanza kumtangaza Lowasa kuwa si mwadilifu kwa kutelekeza mama na mtoto.
Aksante.