Mwakyembe: Mwisho wa Waandishi wa Habari wasio na elimu kuanzia stashahada Desemba 2021

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe amesisitiza kuwa itakapofika Desemba mwaka 2021 ndio mwisho wa waandishi wa habari wasiokua na elimu kuanzia ngazi ya stashahada kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma ya habari ya Mwaka 2016.

Waziri Mwakyembe ametoa kauli hiyo jana Mkoani Singida alipokuwa anazungumza na wadau wa tasnia ya habari ambapo amewataka waandishi hao kutambua kuwa kuanzia mwaka 2022 wale ambao hawatakua na vigezo kulingana na Sheria ya Huduma za Habari hawatakua na nafasi wala sifa ya kuitwa Waandishi wa Habari.

“Uandishi wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine na sio kimbilio la wale ambao wamefeli katika masomo au waliokosa kazi ya kufanya,hivyo naomba mtambue kuwa mwaka 2021 ndio mwisho wa waandishi wasiokua na elimu ya uandishi wa habari kuanzia ngazi ya stashahada”amesema Mwakyembe.

Aidha Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Ibara ya 18 d ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza kuwa kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa sahihi hivyo ni jukumu la wanahabari kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa ambazo ni sahihi kutoka kwa watu sahihi na kuzifikisha kwa walengwa kwa usahihi.
 
Sema hata hivyo vyeti vya sasa hivi (diploma na digrii) vinatia shaka sana; wengi walio navyo hawana uwezo unaolingana na vyeti vyao. Wachunguze na hivyo vyuo na pia walimu. Education ya nchi hii sasa hivi ni majanga matupu.

Sahihi kabisa pia kuhusu wabunge, wasio na vyeti vinavyoeleweka, na huku ndiyo wanaotutungia sheria wasiruhusiwe kuwa wabunge. Mbunge lazima awe na kiwango cha elimu kinachoeleweka.
 
huyu nae .....

alipokuwa waziri wa sheria alitaka mahakimu wawe na degree....

leo huku upande wa habari na vichekesho napo wawe na stashahada.....


kwa nn mzee huyu ana amini sana katika shule shule ?


ubunifu kiduchu ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu nae...

badala ya kuwa creative kuexplore na ku create job opportunities katika wizara yake...ndio kwanza anataka kupoteza ajira za wengine...nini faida ya huu upuuzi?
 
Ametabiri au ni tamko?
Je ana uhakika wa kuwepo kwenye wadhifa!?

Sent using Jamii Forums mobile app

Aidha Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Ibara ya 18 d ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza kuwa kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa sahihi hivyo ni jukumu la wanahabari kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa ambazo ni sahihi kutoka kwa watu sahihi na kuzifikisha kwa walengwa kwa usahihi.

umesoma hii section?
 
Kwa Sasa pia elimu hailipi sana kilingana na uwekezaji wake, education costs! Sasa bado tunaendelea kuweka unemployment zone
 
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe amesisitiza kuwa itakapofika Desemba mwaka 2021 ndio mwisho wa waandishi wa habari wasiokua na elimu kuanzia ngazi ya stashahada kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma ya habari ya Mwaka 2016.

Waziri Mwakyembe ametoa kauli hiyo jana Mkoani Singida alipokuwa anazungumza na wadau wa tasnia ya habari ambapo amewataka waandishi hao kutambua kuwa kuanzia mwaka 2022 wale ambao hawatakua na vigezo kulingana na Sheria ya Huduma za Habari hawatakua na nafasi wala sifa ya kuitwa Waandishi wa Habari.

“Uandishi wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine na sio kimbilio la wale ambao wamefeli katika masomo au waliokosa kazi ya kufanya,hivyo naomba mtambue kuwa mwaka 2021 ndio mwisho wa waandishi wasiokua na elimu ya uandishi wa habari kuanzia ngazi ya stashahada”amesema Mwakyembe.

Aidha Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Ibara ya 18 d ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza kuwa kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa sahihi hivyo ni jukumu la wanahabari kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa ambazo ni sahihi kutoka kwa watu sahihi na kuzifikisha kwa walengwa kwa usahihi.
Journalism is a 'cosmopolitan profession'.
 
Mwakyembe aanze na hao watunga sheria, baadhi hata std VII ni kwa shida tu wamepenya!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo Ni katiba sio Sheria .Katiba inasema kila mpiga kura Ana haki ya kupiga kura na kupigiwa kura.hapo ndipo penye maneno .Sema wasiosoma wasipjua kusoma Wala kuandika wakiamua waweza kuchachamaa waweza shtaki kuwa wao wameachwa kinyume Cha katiba kugombea udiwani,ubunge na uraisib wakati Ni wapiga kura.Kuwa Kama wapiga kura wanaruhusiwa na katiba pia kuwa wapigiwa kura.Tuvumiliane tu kwa hili la vyeo vya kisiasa
 
Creativity na Education ni vitu viwili tofauti na vipo mbali mbali.

Unakuta mwandishi msomi hawezi kufanya ubunifu na ana degree mbili ukimpeleka field ni shida.

Upande wa Ubunifu tuna mfano kwa kijana wa jf Max yeye hakuwa jounalist lakini kwa sababu ya ubunifu umemfanya aingie kwenye tasnia.

Waandishi wote wapo darasani kwa sasa na watakuja na hivyo vyeti wanavyotaka na si kufanya mambo makubwa kutokana na elimu bali ni vyeti tu.
 
Back
Top Bottom