Mwakyembe: Mahakimu walioshinda kesi za rushwa wasirudishwe kazini, wananchi hawana imani nao

nkanga chief

JF-Expert Member
May 31, 2016
2,084
1,620
mwakyembe2014.jpg


Waziri wa katiba na sheria, Dkt. Harrisson Mwakyembe ameitaka tume ya utumishi wa mahakama kutowarejesha kazini mahakimu 28 ambao wameshinda kesi za rushwa zilizokuwa zikiwakabili kwa lengo la kulinda imani ya mahakama kwa wananchi na badala yake mahakimu hao wakafanye kazi nyingine.

Waziri wa katiba na sheria, Dkt. Harrison George Mwakyembe amesema kumekuwepo na watumishi wa mahakama ambao walikuwa wakikabiliwa na tuhuma za rushwa mahakamani, ambapo kati yao watumishi 30 wamekutwa na hatia na kufukuzwa kazi huku mahakimu wengine 28 wakishinda kesi zao, lakini akasema kuwa hawastahili kurejeshwa kazini waendelee kutoa haki kwa madai kuwa tayari wananchi hawana imani nao.

Dkt. Harrison Mwakyembe ambaye ameanza ziara ya kiserikali ya siku tatu katika mikoa ya Mbeya na Songwe, ametembelea ofisi ya msajili wa vizazi na vifo katika halmashauri ya jiji la Mbeya ambako ameitaka ofisi hiyo na nyingine nchini kuongeza kasi ya usajili wa vizazi kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ili kuiondolea Tanzania aibu ya kuwa miongoni mwa nchi tano za mwisho barani Afrika kwa kusajili vizazi vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano.

Mratibu wa zoezi la usajili wa vizazi vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano wa halmashauri ya jiji la Mbeya, Vicent Msolla amezitaja changamoto zinazolikabili zoezi hilo, huku meya wa jiji la Mbeya, Mchungaji David Mwashilindi akiahidi halmashauri yake kuongeza kasi ya usajili wa vizazi na vifo.


Chanzo: ITV
 
Waziri amesema wasirudishwe kwenye deski la uhakimu kuendelea kuamua mashtaka kwa kuwa tayari wananchi hawana imanani nao. Waziri ameagiza wapangiwe kazi nyingine. Hapo sio kuwafukuza kazi!
 
Waziri hana mamlaka yoyote ya kumfukuza hakimu.

Cha ajabu waziri mwenyewe mwanasheria, anajua mamlaka ya tume ya utumishi ya mahakama na mamlaka ya jaji mkuu.

Mbona yeye alipata kashfa ya kuleta mabehewa feki ya treni pamoja na kununua kiwanja kule,ina maana yeye ni bora sana?

Mahakama imewakuta hawana hatia,lakini waziri mwenye phd ya sheria anasema kuna mahakama ya wananchi eti haiwaamini.

Kama wasomi viongozi wako hivi,watanzania tumekula hasara,huyu ndio atasimamia utawala wa sheria kweli?matamko mengine yanadhalilisha serikali na usomi wa mtu.

Wananchi wenyewe ni hawa wana ccm ambai hunyoosha mikono na kuchongea wenzao kwenye ziara za makonda? Wakijua wana dalili za kushindwa kesi wanaandika barua ya kutuhumu kuombwa rushwa,hakimu anafukuzwa.

Kama hakuna security of tenure, basi hakuna haki.

Hii nchi itabaki kuwa gofu milele.
 
Kama ni hivyo tunaomba na wale wabunge wote waliowahi kushitakiwa kwa tuhuma za rushwa na kufutiwa kesi zao, nao wasirudi tena bungeni kuendelea na kazi zao za kujadili na kupitishwa sheria za nchi.. Hali kadhalika mawaziri na viongozi wengine pia.. Kusiwe na double standard kwa hili..

Tuone kama atabaki mtu..
 
waziri hana mamlaka yoyote ya kumfukuza hakimu.

cha ajabu waziri mwenyewe mwanasheria,anajua mamlaka ya tume ya utumishi ya mahakama na mamlaka ya jaji mkuu.

mbona yeye alipata kashfa ya kuleta mabehewa feki ya treni pamoja na kununua kiwanja kule,ina maana yeye ni bora sana?

mahakama imewakuta hawana hatia,lakini waziri mwenye phd ya sheria anasema kuna mahakama ya wananchi eti haiwaamini.

kama wasomi viongozi wako hivi,watanzania tumekula hasara,huyu ndio atasimamia utawala wa sheria kweli?matamko mengine yanadhalilisha serikali na usomi wa mtu.

wananchi wenyewe ni hawa wana ccm ambai hunyoosha mikono na kuchongea wenzao kwenye ziara za makonda? Wakijua wana dalili za kushindwa kesi wanaandika barua ya kutuhumu kuombwa rushwa,hakimu anafukuzwa.

kama hakuna security o ftenure,basi hakuna haki

Hii nchi itabaki kuwa gofu milele
Hawa watakwenda mahakamani na watashinda kesi na kudai fidia. Hizi ni gharama za kujitakia. Haya maamuzi yanasababisha kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa serikali. Je ni nani atakayeweza kugharamia maamuzi kama haya??!! Obvious ni mlipa kodi ndiye atakayeumia, Waziri anatakiwa atafakari kabla ya kutekeleza.
 
Waziri wa Sheria kavunja sheria.

Kawafukuza kazi wenzie kwa kuhisiwa tu japo hawana hatia yoyote.

Utawala wa sheria uko wapi hapo?

Sasa mbona mawaziri hutoka povu na kelele za "sijiuzuru ng'o" wakituhumiwa makosa mbali mbali?

Mbona Mwakyembe hakufukuzwa kazi au kujiuzuru baada ya tuhuma za ufisadi akiwa Waziri wa Mawasiliano??
 
Okay,hata yeye anatuhumiwa kununua mabehewa mabovu. Naye atumbuliwe? Kwa hili la Rushwa liko wazi sana na ni mahakimu wengi na majaji wanachukua kitu kidogo. Kama huamini gonga gari ya mtu iharibike ila usisababishe madhara kwa binadamu, ukubali Bima ya gari yako kukarabati gari uliyogonga.

Mkifika mahakamani ili taratibu zifuatwe, kabla hujalipa faini kuna pesa lazima utaambiwa uitoe.Ukishatoa ndio unapewa account kwenda kulipa faini ya serikali. Usipotoa utazungushwa wee, muda utaisha na utarudishwa rumande na kupangiwa siku nyingine kusikilizwa kesi yako.

Kwenye mgawo hakimu anachukua chake na polisi mwenye faili lako analamba chake.Hii imenikera sana,halafu hiyo faini ni ndogo sana ukilinganisha na mpunga wanaokuchomoka hao jamaa.
 
na wale waliotajwa na mbowe kupewa milioni kumi

kuna wale wabunge waliopelekwa mahakama ya kisutu kwa kumuomba rushwa mkurugenzi morogoro
 
Back
Top Bottom