Mwakyembe amuumbua Moses Machali

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, kwa sasa Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe anajibu baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wabunge wakati wa mjadala wa wizara hiyo. Miongoni mwa hoja ni zile zilizotolewa na taarifa ya Kambi ya Upinzani iliyowasilishwa na Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Moses Machali. Miongoni mwa hoja za Machali ni juu ya UDA, DART, Ubungo Bus Terminal na Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba maeneo ambayo Mwakyembe amesema kuwa yana Wizara zake ( Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Elimu). Amemshangaa sana Machali kwa kuibua hoja ambazo hazipo kwenye wizara yake. Amesema kuwa Machali ameonesha umbumbumbu mkubwa sana. Hata hivyo amesema kuwa huenda hali hiyo imetokana na ugeni wake kwenye kazi ya Uwaziri Kivuli. Amemshauri Machali kujifunza kutoka kwake na wakati wote yupo tayari kumfundisha utendaji wa Wizara hiyo

Hawa ni aina ya Mawaziri Kivuli ambao Freeman Mbowe aliwatangaza kwa Mbwembwe
 
Miongoni mwa hoja za Machali ni juu ya UDA, DART, Ubungo Bus Terminal kwani ziko wizara gani kama siyo uchukuzi au mimi ndo sielewi, najua mradi wa DART uko chini ya wizara ya ujenzi kwa maana ya kuweka Miundo mbinu ya ujenzi, lakini Dart kama yenyewe na UDA ziko chini ya wizara ya Mwakyembe (Uchukuzi) Either wewe ndiye ambaye huelewi au hujatueleza kamuumbuaje maana hata papara zinaweza kukufanya ushindwe kutoa habari vizuri

Wadau, kwa sasa Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe anajibu baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wabunge wakati wa mjadala wa wizara hiyo. Miongoni mwa hoja ni zile zilizotolewa na taarifa ya Kambi ya Upinzani iliyowasilishwa na Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Moses Machali. Miongoni mwa hoja za Machali ni juu ya UDA, DART, Ubungo Bus Terminal na Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba maeneo ambayo Mwakyembe amesema kuwa yana Wizara zake ( Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Elimu). Amemshangaa sana Machali kwa kuibua hoja ambazo hazipo kwenye wizara yake. Amesema kuwa Machali ameonesha umbumbumbu mkubwa sana. Hata hivyo amesema kuwa huenda hali hiyo imetokana na ugeni wake kwenye kazi ya Uwaziri Kivuli. Amemshauri Machali kujifunza kutoka kwake na wakati wote yupo tayari kumfundisha utendaji wa Wizara hiyo

Hawa ni aina ya Mawaziri Kivuli ambao Freeman Mbowe aliwatangaza kwa Mbwembwe
 
Miongoni mwa hoja za Machali ni juu ya UDA, DART, Ubungo Bus Terminal kwani ziko wizara gani kama siyo uchukuzi au mimi ndo sielewi, najua mradi wa DART uko chini ya wizara ya ujenzi kwa maana ya kuweka Miundo mbinu ya ujenzi, lakini Dart kama yenyewe na UDA ziko chini ya wizara ya Mwakyembe (Uchukuzi) Either wewe ndiye ambaye huelewi au hujatueleza kamuumbuaje maana hata papara zinaweza kukufanya ushindwe kutoa habari vizuri
Magufuli alieleza vema juu ya miradi hiyo. Miradi ya Usafiri wa Jiji la Dar es Salaam upande wa Barabara ipo chini ya Wizara ya Ujenzi. Pia Miradi ya kupunguza msongamano wa jiji la Dar es Salaam ipo chini ya Wizara ya Ujenzi
 
Full pumba hapaaa kachukue buku saba zako fisi maji wewe, ww na hii pichu hamna tofauti
 

Attachments

  • 1401119448093.jpg
    1401119448093.jpg
    39.8 KB · Views: 161
Mwenye akili timamu hawezi kwenda ccm, ni bora abaki anauza machungwa kuliko kwenda ccm
 
Back
Top Bottom