Elections 2010 Mwakipesile atangaza rasmi kutokugombea ubunge wa Kyela 2010

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Hili wengine tuliandika tokea mwaka jana kwamba Mwakipesile hana mpango tena wa kugombea ubunge wa Kyela.
Sihitaji Ubunge Kyela 2010- Mwakipesile
Sunday, 07 June 2009 15:07 Na Mwandishi Wetu Mbeya

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Bw.John Mwakipesile ametangaza kuwa hana mpango wa kuwania ubunge Jimbo la Kyela mwakani kwani ameridhika na heshima aliyopewa na Rais Jakaya Kikwete, kumteua Mkuu wa Mkoa huo.

"Hivi ndugu zangu mimi nilikuwa mbunge kwa miaka 10 baada ya kufuatwa na kuombwa, baadaye nikashindwa kwenye kura za maoni,Rais akanipa heshima kuniteua kuwa Mkuu wa Mkoa hadi sasa, nirudi kugombea ubunge kwa ajili ya kutafuta nini? "Alihoji Bw. Mwakipesile hivi karibuni, wakati akizungumza na maaskofu wa madhehebu mbalimbali mkoani Mbeya, waliomtembelea nyumbani kwake.


Bw.Mwakipesile alitoa kauli hiyo wakati akijibu moja ya maswali ya maaskofu hao ambao aliwaalika kwa ajili ya chakula cha jioni na kubadilishana mawazo kuhusu mikakati mbalimbali ya maendeleo mkoani Mbeya.

Askofu huyo alitaka kujua mustakabali wa mkuu huyo wa mkoa kugombea ubunge Kyela kwenye Uchaguzi Mkuu ujao mwakani, baada ya kuwepo uvumi kwamba anajiandaa kurudi tena kupigania nafasi hiyo.


Bw. Mwakipesile alisema sasa ni miaka minne tangu ateuliwe kushika wadhifa huo na kutokana na mshikamano mzuri na wasaidizi wake, pamoja na wananchi, wamepata mafanikio makubwa hususani katika nyanja ya elimu.


Mkuu huyo wa mkoa ,alisema kuwa alipokea uteuzi wa Rais kwa hofu na heshima kubwa, hivyo anachofanya sasa ni kuhakikisha anachapa kazi ili 'kutomwangusha' Rais Kikwete aliyempa wadhifa huo.

"Maaskofu ninyi ni watumishi wa Mungu, hivyo kama naongopa katika ahadi yangu hii nianguke kwa kuwa hapa nazungumza na Mungu kutokana na uzito wa nafasi yenu. Nasema sina mpango tena kuwania ubunge Kyela kama ambavyo baadhi ya wanasiasa waoga wamekuwa wakinizushia,"alisema Bw. Mwakipesile.

Aliwataka wanasiasa kuacha malumbano yasiyo na msingi na kuchapa kazi waliyotumwa na wananchi na yeye kama Mkuu wa Mkoa, kazi yake kubwa ni kusukuma gurudumu la maendeleo katika wilaya,kata na vijiji vyote vya Mkoa wa Mbeya bila upendeleo wa aina yoyote.

Aliwahakikishia maaskofu hao kuwa kutokana na msimamo wake, hana ugomvi na mwanasiasa yeyote bali na anafanyakazi na wote
kuhakikisha wananchi wanapata maisha bora kama alivyo ahidi Rais Kikwete ambaye ndiye mwajiri wao.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mwenyekiti wa maaskofu hao, Mhashamu John Mwela, alieleza kufurahishwa na makaribisho ya mkuu huyo wa mkoa na kwamba ni kielelezo cha namna anavyowatambua na kuthamini mchango wao. Walimwahidi kuzidi kumpa ushirikiano mzuri katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa Mbeya na Watanzania kwa ujumla.
 
Kaona hataiweza tsunami ya mwana wa watu -- Dr HM. Sababu nyingine ni blah blah tu.
 
hivi hao maaskofu na viongozi wa kisiasa na serikali vipi?Yaani Askofu mzima anauliza swali la kijinga hivyo..Badala ya kuuliza ni lini serkilai itaaacha kukumbatia mafisadi au ni lini serikali italeta maendeleo?

Na mie nikirudi nitawaita
 
Enyi wenzetu wa mwaka 1930 kweusi na 1940 kweupe, ndoto za kudhani mnaweza kuhimili mikimiki ya kwenye majukwaa mwazitoa wapi?

Mwakipesile is history as far as Kyela politics is concerned. Ashukuru na aendelea kuimba wimbo wa 'ameniona, ameniona ...." kwa kupewa ukuu wa Mkoa.
 
2010 around ze corner

Wanaoona na kusoma alama za nyakati mapema ni bora wafanye hivyo la sivyo...............watahaibika.

Aibu yetu....................... Aibu yao ...........Aibu yao mwenyewe........

Na Bado tutasikia wengi
 
Hah ha ha ha,

Mwakipesile amegonga jackpot hapa kwenye PR. Kwa sasa hata isemwe nini, yeye kishatangulia na kusema kuwa hagombei.

Si-hasa mchezo mchafu
 
Hah ha ha ha,

Mwakipesile amegonga jackpot hapa kwenye PR. Kwa sasa hata isemwe nini, yeye kishatangulia na kusema kuwa hagombei.

Si-hasa mchezo mchafu

Mwakipesile aliwaambia Wapambe wake mwishoni mwa 2006 kwamba hatagombea ubunge tena Kyela. Wengi hawakuamini, hata mimi nilifikiri ni kama kawaida ya wanasiasa na kwamba baadaye angebadilika tu maana hata tunaowajua hapa JF nao wamebadilika na kuanza kusema wananchi wamewabembeleza.

Sababu alizotoa ni hizo hizo kwamba kupewa kuwa mkuu wa mkoa kwake ni faraja kubwa. Nafikiri alionja joto ya jiwe kwenye ubunge na sasa anaona anafaidi pesa za kwenye siasa bila bugudha za wananchi.
 
Bado siamini....Mh Kagasheki alisema haya baadaye akakanusha...Hata Mzee Kaunda alikuja kujikana mwenyewe akagombea uraisi Zambia na kupata aibu. Mwakipesile 2010 atakuja na visingizio wazee wameniomba and all those bla bla....!
 
Bado siamini....Mh Kagasheki alisema haya baadaye akakanusha...Hata Mzee Kaunda alikuja kujikana mwenyewe akagombea uraisi Zambia na kupata aibu. Mwakipesile 2010 atakuja na visingizio wazee wameniomba and all those bla bla....!
Masanilo,

Sitashangaa akibadilika, ila pia anajua kura zake hazitatimia 2010 kwasababu Kyela wakikutema mara moja sahau hiyo ya kurudi tena.

Mwaka kwenye politics ni muda mrefu sana, anaweza kuja na visingizio kibao vya kugombea, ndio siasa hizo, wanafikiri sisi wananchi ni wajinga na hatufikiri.
 
hivi hao maaskofu na viongozi wa kisiasa na serikali vipi?Yaani Askofu mzima anauliza swali la kijinga hivyo..Badala ya kuuliza ni lini serkilai itaaacha kukumbatia mafisadi au ni lini serikali italeta maendeleo?

Na mie nikirudi nitawaita

Rudi tu mapema ndugu, inaelekea wewe huna habari jinsi ufisadi/mafisadi walivyotumia vyombo vya dola katika vinyanganyiro tofauti mkoani Mbeya.
Hawa Maaskofu wako katibu sana na wananchi(kwa taarifa yako wanakutana kila jumapili).
Si jambo la kushangaza kwamba katika michakato ya kisiasa Mkuu wa Wilaya Kyela tayari ametemwa.Mkuu Mwakipesile amefanya jambo la busara kutamka na mapema azma yake ya kutogombea.
 
Rudi tu mapema ndugu, inaelekea wewe huna habari jinsi ufisadi/mafisadi walivyotumia vyombo vya dola katika vinyanganyiro tofauti mkoani Mbeya.
Hawa Maaskofu wako katibu sana na wananchi(kwa taarifa yako wanakutana kila jumapili).
Si jambo la kushangaza kwamba katika michakato ya kisiasa Mkuu wa Wilaya Kyela tayari ametemwa.Mkuu Mwakipesile amefanya jambo la busara kutamka na mapema azma yake ya kutogombea.

Kainzi kalikoazimwa toka kwa Mwanakijiji kamefanikiwa kuliona file la DC aliyeondolewa Kyela. Madai makubwa ni umalaya na kwamba eti alikuwa anatumia gari la serikali kufuata watoto wa shule mpaka kule Malawi. Hiyo taarifa iliandaliwa kule ofisi ya PM.

Kama kuthibitisha madai yao wakaweka na case yake ya kufumaniwa na mkewe. Hapo ngoma ikawa imeisha, jamaa akapigwa nje.

Siasa bwana kazi kweli kweli! CCM wakianza kufukuza malaya, mbona serikali na bunge litabaki tupu!
 
Hili wengine tuliandika tokea mwaka jana kwamba Mwakipesile hana mpango tena wa kugombea ubunge wa Kyela.


Du nimekubali kuwa una data mzee. hebu tupe wengine basi ambao hawangombei ili tupime basi kama form zinachukulika
 
Du nimekubali kuwa una data mzee. hebu tupe wengine basi ambao hawangombei ili tupime basi kama form zinachukulika

Umeanza tena matatizo yako? Angalia sana, ukifuata fuata watu utaishia kuumbuka maana data zote tunazo!
 
Msishangae atachaguliwa kuwa balozi wa Tanzania USA anytime from now.

Not a chance! Naweza kwenda mbali zaidi na kusema jamaa atatemwa kuwa mkuu wa mkoa kwenye mabadiliko yatakayofanywa na JK baada ya uchaguzi mwakani.
 
Amesahau kusema pia ataachana na kundi baya sana la mtandao....maana hilo ndilo analoliabudu kwa sasa angetubu na kuachana nao kama kweli alikuwa anatubu na kusema na Mungu mbele ya maaskofu.......aache unafiki wake.....
 
Wanasiasa hawaaminiki! Hawakawii kusema niliombwana wazee nigombee tena!
 
Back
Top Bottom