Mwakawago ataka wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
MWASISI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na aliyekuwa Katibu Mtendaji wa pili wa chama hicho, Balozi Daudi Mwakawago amewashauri viongozi wa serikali wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe katika nafasi wanazoshikilia kwa sasa ili kupisha uchunguzi huru kuhusu madai hayo.


Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalum nyumbani kwake jijini Dar es Salaam, Balozi Mwakawago alisema wale wote ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi kwanza wanapaswa kujibu tuhuma zinazowakabili na baada ya hapo wajiondoe katika nyadhifa zao ili uchunguzi huru ufanyike.


"Yule anayetuhumiwa jamii ingetegemea aseme kitu, ukinyamaza na kudhani tuhuma hizi zitaishia hewani, unajidanganya, zitaendelea kuwako, kwa maoni yangu naona tuhuma za kisiasa bora zingejibiwa kisiasa," alisema Balozi Mwakawago.


Alisema ili kuimarisha utawala bora nchini, ni wakati muafaka sasa wale ambao wametuhumiwa kwenda kwa Rais ambaye amewateua na kumueleza haja yao ya kujiondoa katika nafasi wanazoshikilia.


"Tujenge utamaduni wa uwajibikaji, wanatakiwa waende kwa aliyewateua, wamweleze kwamba wametuhumiwa na wameamua kukaa kando ili uchunguzi huru ufanyike. Wananchi wanawaangalia, wananchi sasa wanajua haki zao kuliko huko nyuma, viongozi lazima wafahamu hilo, pia wanafahamu dhana ya uwajibikaji kuliko hapo zamani," alisema.


Alisema kwa wale ambao wana dhana kwamba Mahakama itawasafisha wanajidanganya kwani katika siasa hakuna ushahidi wa Mahakama, na hata wakisafishwa na vyombo vya sheria bado wananchi wataendelea kuamini tuhuma hizo ni za kweli kwa kuwa bado wamekalia nyadhifa ambazo wametuhumiwa wakiziongoza.


"Ni kweli Mahakama inaweza kukusafisha, lakini pia ni vema kuwa makini maana ukienda Mahakamani, unaweza kuvuliwa nguo zaidi, tuhuma nyingi zaidi zinaweza kuibuka. Mahakama si mchezo itaenda kila eneo na mambo mengi yanaweza kuibuliwa," alisema.


Balozi Mwakawago ambaye ameshika nyadhifa za Katibu Mwenezi wa TANU, Katibu Mtendaji wa CCM, Waziri wa Habari katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, na Waziri wa Viwanda na Biashara katika serikali ya Awamu ya Pili, alisema katika siasa tuhuma hujitokeza pale ambapo wadau wanagundua kuwa kiongozi fulani ametoka katika mstari.


Akizungumzia kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu huko Uingereza, Balozi Mwakawago alisema haoni tatizo kwa mkataba kusainiwa nje ya nchi, ila tatizo ni kule kusainiwa katika hali ya usiri pasipo wananchi kupewa taarifa.


"Tatizo ambalo limejitokeza ni ile hali ya mkataba kusainiwa katika hali ya usiri, hakuna sababu ya mkataba kusainiwa kwa usiri na viongozi.


Viongozi wanasaini mikataba kwa niaba ya wananchi, hivyo wananchi wana haki kabisa ya kupata habari za mikataba ya maliasili zao," alisema.


Pia Balozi Mwakawago ambaye alikuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa miaka ya 90, alisema baada ya Rais Kikwete kuwaambia Watanzania kwamba kulikuwa na haja ya kuangalia upya mikataba ya madini kwani ilikuwa haiwanufaishi Watanzania wakati akihutubia Bunge, wananchi wengi waliingiwa na furaha kwa hiyo hatua ya kusaini mkataba mwingine katika kipindi kifupi kuliibua maswali mengi.


"Rais Kikwete aligusa hisia za watu, hivyo walishangaa pale walipoambiwa kwamba kuna mkataba mwingine ambao umesainiwa katika kipindi kifupi, ilibidi wajiulize kulikoni? alisema Balozi Mwakawago.


Tuhuma za ufisadi zilitolewa na Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa dhidi ya viongozi wa serikali na chama. Tokea tuhuma hizo zitolewe, baadhi ya waliotuhumiwa wamekana kuhusika nazo, na wengine wametishia kwenda Mahakamani.


source Mwananchi news paper
 
Posted Date::11/12/2007
Mwakawago azungumzia 'mafisadi',ataka kila mmoja ajibu tuhuma
*Ashauri wajiuzulu kupisha uchunguzi
*Asema mahakama haiondoi tuhuma za kisiasa

Na Mwandishi Wetu
Mwananchi

MWASISI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na aliyekuwa Katibu Mtendaji wa pili wa chama hicho, Balozi Daudi Mwakawago amewashauri viongozi wa serikali wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajiondoe katika nafasi wanazoshikilia kwa sasa ili kupisha uchunguzi huru kuhusu madai hayo.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalum nyumbani kwake jijini Dar es Salaam, Balozi Mwakawago alisema wale wote ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi kwanza wanapaswa kujibu tuhuma zinazowakabili na baada ya hapo wajiondoe katika nyadhifa zao ili uchunguzi huru ufanyike.

"Yule anayetuhumiwa jamii ingetegemea aseme kitu, ukinyamaza na kudhani tuhuma hizi zitaishia hewani, unajidanganya, zitaendelea kuwako, kwa maoni yangu naona tuhuma za kisiasa bora zingejibiwa kisiasa," alisema Balozi Mwakawago.

Alisema ili kuimarisha utawala bora nchini, ni wakati muafaka sasa wale ambao wametuhumiwa kwenda kwa Rais ambaye amewateua na kumueleza haja yao ya kujiondoa katika nafasi wanazoshikilia.

"Tujenge utamaduni wa uwajibikaji, wanatakiwa waende kwa aliyewateua, wamweleze kwamba wametuhumiwa na wameamua kukaa kando ili uchunguzi huru ufanyike. Wananchi wanawaangalia, wananchi sasa wanajua haki zao kuliko huko nyuma, viongozi lazima wafahamu hilo, pia wanafahamu dhana ya uwajibikaji kuliko hapo zamani," alisema.

Alisema kwa wale ambao wana dhana kwamba Mahakama itawasafisha wanajidanganya kwani katika siasa hakuna ushahidi wa Mahakama, na hata wakisafishwa na vyombo vya sheria bado wananchi wataendelea kuamini tuhuma hizo ni za kweli kwa kuwa bado wamekalia nyadhifa ambazo wametuhumiwa wakiziongoza.

"Ni kweli Mahakama inaweza kukusafisha, lakini pia ni vema kuwa makini maana ukienda Mahakamani, unaweza kuvuliwa nguo zaidi, tuhuma nyingi zaidi zinaweza kuibuka. Mahakama si mchezo itaenda kila eneo na mambo mengi yanaweza kuibuliwa," alisema.

Balozi Mwakawago ambaye ameshika nyadhifa za Katibu Mwenezi wa TANU, Katibu Mtendaji wa CCM, Waziri wa Habari katika Serikali ya Awamu ya Kwanza, na Waziri wa Viwanda na Biashara katika serikali ya Awamu ya Pili, alisema katika siasa tuhuma hujitokeza pale ambapo wadau wanagundua kuwa kiongozi fulani ametoka katika mstari.

Akizungumzia kusainiwa kwa mkataba wa mgodi wa dhahabu huko Uingereza, Balozi Mwakawago alisema haoni tatizo kwa mkataba kusainiwa nje ya nchi, ila tatizo ni kule kusainiwa katika hali ya usiri pasipo wananchi kupewa taarifa.

"Tatizo ambalo limejitokeza ni ile hali ya mkataba kusainiwa katika hali ya usiri, hakuna sababu ya mkataba kusainiwa kwa usiri na viongozi.

Viongozi wanasaini mikataba kwa niaba ya wananchi, hivyo wananchi wana haki kabisa ya kupata habari za mikataba ya maliasili zao," alisema.

Pia Balozi Mwakawago ambaye alikuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa miaka ya 90, alisema baada ya Rais Kikwete kuwaambia Watanzania kwamba kulikuwa na haja ya kuangalia upya mikataba ya madini kwani ilikuwa haiwanufaishi Watanzania wakati akihutubia Bunge, wananchi wengi waliingiwa na furaha kwa hiyo hatua ya kusaini mkataba mwingine katika kipindi kifupi kuliibua maswali mengi.

"Rais Kikwete aligusa hisia za watu, hivyo walishangaa pale walipoambiwa kwamba kuna mkataba mwingine ambao umesainiwa katika kipindi kifupi, ilibidi wajiulize kulikoni? alisema Balozi Mwakawago.

Tuhuma za ufisadi zilitolewa na Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa dhidi ya viongozi wa serikali na chama. Tokea tuhuma hizo zitolewe, baadhi ya waliotuhumiwa wamekana kuhusika nazo, na wengine wametishia kwenda Mahakamani.
 
...na wakati huo huo wasanii wanaendelea na usanii wao :(
 
You know I was thinking about Mwakawago.. amerudi lini toka Sierra Leone? au yuko nyumbani kwa likizo fupi....
 
Kweli kifo cha mende, yaani sasa mpaka Mwakawago naye, je na yeye anaweza akajibu yanayomuhusu kule ubalzoi wetu NY?

Anyways, mkuu alimaliza muda wake ubalozini kwetu NY, akapewa kazi na Kofi Annan, kuwa msaidizi wake Sierra Leone, ambako hakuelewana kabisa na baadhi ya seniors wa UN, huko hivyo alihamishiwa kwa muda visiwani Cape-Verde, mpaka alipomaliza mkataba wake na UN, alirudi nyumbani, ambako mpaka leo hajapewa chochote, ingawa amekuwa akijaribu sana lakini Mkapa, alikataa kabisa kuonana naye toka alipotoka ubalizini kwetu, Muungwana, ndio kabisaaa maana huyo mzee aliwahi kuwa bosi wa Muungwana zamani Dodoma CCM, alikuwa akimchukia sana Muungwana mpaka akamuhamishia Tunduru, kwa hiyo uwezekano wa hata Bodi hakuna,

Sasa najua yuko benchi, ila haya yamenishitua kutoka kwake, maana ya kwake ni aibu hata kusema, lakini ndio hivyo tena kifo cha mende!
 
Kweli kifo cha mende, yaani sasa mpaka Mwakawago naye, je na yeye anaweza akajibu yanayomuhusu kule ubalzoi wetu NY?

Anyways, mkuu alimaliza muda wake ubalozini kwetu NY, akapewa kazi na Kofi Annan, kuwa msaidizi wake Sierra Leone, ambako hakuelewana kabisa na baadhi ya seniors wa UN, huko hivyo alihamishiwa kwa muda visiwani Cape-Verde, mpaka alipomaliza mkataba wake na UN, alirudi nyumbani, ambako mpaka leo hajapewa chochote, ingawa amekuwa akijaribu sana lakini Mkapa, alikataa kabisa kuonana naye toka alipotoka ubalizini kwetu, Muungwana, ndio kabisaaa maana huyo mzee aliwahi kuwa bosi wa Muungwana zamani Dodoma CCM, alikuwa akimchukia sana Muungwana mpaka akamuhamishia Tunduru, kwa hiyo uwezekano wa hata Bodi hakuna,

Sasa najua yuko benchi, ila haya yamenishitua kutoka kwake, maana ya kwake ni aibu hata kusema, lakini ndio hivyo tena kifo cha mende!

Yamekushtua kwa kuwa ni mazuri!?
Je, unayaunga mkono haya aliyoyaongea kama yana umuhimu wa kusikilizwa na hatimaye kutekelezwa na viongozi wa juu wa Tanzania!?
 
Mkuu so far ninaheshimu sana wito kama huu ulipotolewa na Mwinyi, na Malecela, na ndipo hasa Mtandao waliposhituka, maana by then walikuwa wameowaomba wote wawili wawasaidie kwenye hilo lakini wote wakagoma,


lakini Butiku na huyu Mwakawago, I am not sure, kwa sababu wote wawili hawana rekodi nzuri kuhusiana na rushwa, na ninajua kuwa wamekuwa wakijaribu kila njia kupewa kazi ya ulaji na Mtandao lakini wameshindwa, ndio maana nina wasi wasi na kauli zao kama ni genuine!

Nafikiri na wewe unafahamu kuwa viongozi wetu wa juu sio wajinga kiasi hicho!
 
Mzee mwenzangu, ukweli wa hoja haujalishi nani anautoa. Hata akitokea jambazi aliyeko kifungoni akisema "walioiba na wenyewe washitakie" hatuwezi kumuambia "wewe jambazi na uko kifungoni kwa hiyo hoja yako haina maana". Hoja iangaliwe kwa uzito wake wenyewe bila kujali nani anaitoa. Hadi hivi sasa hatujasikia hoja za ufisadi kuhusu Mwakawago, Butiku, Warioba n.k isipokuwa kwa wale wachache waliobahatika "kuzifahamu". Hilo hata hivyo haliondoi ukweli kuwa Mwakawago anayo hoja au hana hoja.

Unafikiri kuwataka waliohusika wajibu hoja amekosea bila kuangalia kama yeye amewahi kutuhumiwa hoja na akakataa kujibu; na kama kuna hoja dhidi yake itolewe na yeye aambiwe ajibu. Lakini kujibu hoja kwa kukataa kujibu hoja kwa sababu aliyetoa hoja ana makosa fulani ni mbinu ambayo chama chetu kimejaribu sana na ninafikiri watu wameanza kutuelewa vizuri..
 
Mzee mwenzangu, ukweli wa hoja haujalishi nani anautoa. Hata akitokea jambazi aliyeko kifungoni akisema "walioiba na wenyewe washitakie" hatuwezi kumuambia "wewe jambazi na uko kifungoni kwa hiyo hoja yako haina maana". Hoja iangaliwe kwa uzito wake wenyewe bila kujali nani anaitoa. Hadi hivi sasa hatujasikia hoja za ufisadi kuhusu Mwakawago, Butiku, Warioba n.k isipokuwa kwa wale wachache waliobahatika "kuzifahamu". Hilo hata hivyo haliondoi ukweli kuwa Mwakawago anayo hoja au hana hoja.

Unafikiri kuwataka waliohusika wajibu hoja amekosea bila kuangalia kama yeye amewahi kutuhumiwa hoja na akakataa kujibu; na kama kuna hoja dhidi yake itolewe na yeye aambiwe ajibu. Lakini kujibu hoja kwa kukataa kujibu hoja kwa sababu aliyetoa hoja ana makosa fulani ni mbinu ambayo chama chetu kimejaribu sana na ninafikiri watu wameanza kutuelewa vizuri..

Ni kweli kabisa mzee, Hoja ya mtu haipaswi kupingwa kwa sababu mtoa hoja amepata kutenda kosa, hata kama kosa alilokwisha kulitenda huko zamani ni sawa kabisa na analolikemea hivi leo.

waswahili walisema "Mshikwa na ngozi ndiyo mwizi". kwa hiyo hawa walioshikwa na ngozi(waliotajwa kwenye list of shame),hawana budi kuithibitishia jamii kwamba wao ni watu safi,la sivyo jamii itaendelea kuwa na mashaka nao
 
Mkuu MMJ,

Sina tatizo na hoja za Butiku, na Mwakawago na sitegemei kuanzisha ishu behind it, lakini sasa isiwe hii ishu kichaka cha mafisadi wengine kujaribu kujificha kwenye migongo ya wengine,

Halafu kwa nini wamesubiri muda wote huu, mpaka baada ya rais na ccm kuchagua viongozi wake Dodoma, ndio wanaanza kujitokeza? I mean hoja ni hoja, lakini binafsi ninajaribu kuwa objective, na sauti zinazojotokeza this late, walikuwa wapi muda wote wakati wananchi wanyonge walipokuwa wakiwazomea viongozi wetu?

Yaaani mpaka waone kila mtu anasema ndio warudie kutafuta ushujaaa wa dakika ya mwisho ili wasiachwe? Sisi tumesema toka siku ya kwanza, liwalo na liwe, wao wamebana kimyaaa, sasa all over sudden kila kiongozi wa ana-something to say? Mkuu MMJ, hawa ni wanafiki, kiongozi wa kweli husema mapema, hasubiri mpaka apime upepo kwanza ili aone nani kasema nani hakusema, halafu ndio aseme maana sasa tutakuwa wengi!

Sawa hoja ni hoja, hata kama inatoka kwa jambazi, lakini wananchi tumechoshwa na hawa viongozi vinyonga kama Mwakawago, je wananchi waliokuwa wakiwazomea viongozi wangeshikwa na kufungwa angesema huyu?
 
Mkuu so far ninaheshimu sana wito kama huu ulipotolewa na Mwinyi, na Malecela, na ndipo hasa Mtandao waliposhituka, maana by then walikuwa wameowaomba wote wawili wawasaidie kwenye hilo lakini wote wakagoma,


lakini Butiku na huyu Mwakawago, I am not sure, kwa sababu wote wawili hawana rekodi nzuri kuhusiana na rushwa, na ninajua kuwa wamekuwa wakijaribu kila njia kupewa kazi ya ulaji na Mtandao lakini wameshindwa, ndio maana nina wasi wasi na kauli zao kama ni genuine!

Nafikiri na wewe unafahamu kuwa viongozi wetu wa juu sio wajinga kiasi hicho!

Mkuu heshima mbele,

Unajua binadamu wote hatuko perfect tuna kasoro zetu mbali mbali ambazo zinazidiana uzito. Siyajui aliyoyafanya Mwakawago alipokuwa pale UN, lakini bado aliyoyasema yana umuhimu mkubwa katika nchi yetu na yanastahili kupewa kipaumbele na viongozi wa Tanzania.

Hata Butiku naye pia ni kiongozi wa muda mrefu, sijui hali yake sasa hivi ikoje, lakini kama anataka kazi ana haki kabisa ya kuomba kuonana na wakubwa ili wamkumbuke asife na njaa hili hata Nyerere alikuwa analifanya sana kwa kusaidia watu waliokuwa na hali mbaya. Lakini wakati huo huo pamoja na njaa na shida zao zinazowakabili wana haki ya kukemea na kuulizia matukio mbali mbali ndani ya chama na serikali kwa manufaa ya Watanzania wote. Hawa kwa kuwa waliwahi kushika nafasi mbali mbali za juu katika serikali zilizopita labda wakitoa sauti zao zinaweza kupewa uzito mkubwa na ushauri wao ukatekelezwa.
 
Kwanza mimi naona ni sawa tu kwa Mwakawago kutoa maoni yake, ila inanishangaza kuona ni kwa nini imemchukua muda mrefu kusema hadharani kama kweli yeye anauzalendo na nchi hii.
Pili lazima wanaJF muelewe kuwa wana mtandao hawamwogopi mtu kwa kuwa wamemweka raisi kwenye viganja vyao kwa hiyo malalamiko tu hayatawafanya hawa jamaa kusalimu amri labda kuandaa mgomo au maandamano nchi nzima ama sivyo na hili nalo litapita kama lile la madawa ya kulevya.
Wembe.
 
Hakuna muda maalum wa mtu kukemea mabaya, ndani ya CCM wanaoyaona maovu ni wengi na asilimia kubwa hadi hii leo wengi wao wamekuwa mabubu. Bora Mwakawago ambaye amevumilia vya kutosha na sasa kuamua kutoa dukuduku lake. Ingekuwa vizuri kuhoji hao waliokuwa mabubu kukemea maovu chungu nzima ndani ya CCM na siyo Mwakawago eti alikuwa wapi siku zote. Mzee aliamua kuvumilia kwa matarajio kwamba viongozi watajirudi lakini naona usanii unaendelea tu.
 
Mkuu Bubu,

Viongozi wenye uchungu na nchi husema pale pale tu kabla moto haujapungua, huwa hawasubiri mpaka moto umesiha ndio wanajitokeza,

Huyu angekuwa mzalendo kweli basi angekemea Zitto, kusimamishwa bungeni kwanza, kabla hajaopngelea mafisadi, tunashukur kuwa amesema something, lakini no thank you too!
 
Mkuu Bubu,

Viongozi wenye uchungu na nchi husema pale pale tu kabla moto haujapungua, huwa hawasubiri mpaka moto umesiha ndio wanajitokeza,

Huyu angekuwa mzalendo kweli basi angekemea Zitto, kusimamishwa bungeni kwanza, kabla hajaopngelea mafisadi, tunashukur kuwa amesema something, lakini no thank you too!

Mkuu

Unajua Watanzania hatuna utamaduni wa namna hiyo, watu wengi huwa tunasemea pembeni kwa sababu ya uoga au uadilifu wa uongo na kweli. Kidogo kidogo nasi labda tutakuwa na utamaduni wa kukemea maovu bila woga wa kufukuzwa kazi au kupoteza maisha.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom