Masaningala
JF-Expert Member
- Nov 19, 2010
- 543
- 199
WanaJF, maveterani na wageni waliojiunga na forum hivi karibuni, ninawapa salaam za kheri ya mwaka mpya. Mimi ni mmoja wa wageni ambao najitokeza mbele yenu kwa kuanza mwaka mpya 2011 kwa kujitambulisha kwenu kama mwenzenu mjenga nchi mwenye nia ya kushiriki katika kuleta mageuzi ya nchi yetu ili iwe na siasa safi, kwa madhumuni ya kufanikisha na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi (kuondoa umaskini), maendeleo ya kiroho (spirituality), na kudumisha utamaduni wa Kitanzania. Ni matumaini yangu kuwa nitashirikiana na wote ndani ya forum hii kwa lengo la kubadilishana mawazo kwa lengo la kujenga Tanzania (Tanganyika na Zanzibar).
Mwaka 2011 nauona ni mwaka wa Mchakato wa Katiba Mpya, Mawazo na Maamuzi Mapya ikiambatana na Uwajibikaji Mpya. Tujiandae katika haya.
Mwaka 2011 nauona ni mwaka wa Mchakato wa Katiba Mpya, Mawazo na Maamuzi Mapya ikiambatana na Uwajibikaji Mpya. Tujiandae katika haya.