Mwaka Mmoja wamechelewa!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Mhariri
Daily News; Wednesday,July 23, 2008 @20:01

JANA katika gazeti hili tuliripoti kwamba wanafunzi takribani 10,000 waliojiunga na vyuo vya elimu ya juu mwaka jana walifanya udanganyifu na kujipatia mikopo ya elimu zaidi ya mara moja.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, wengi wa wanafunzi walipata mikopo hiyo kwa njia ya udanganyifu kutokana na kudahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja.

Katika mazingira ya mwaka huu ambako kuna zaidi ya wanafunzi 18,000 waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja, kuna hatari kwamba huenda kukawa na idadi kubwa ya wanafunzi wasio waaminifu ambao wanaweza kutumia fursa hiyo kuiba fedha kwa kisingizio kwamba hiyo ni mikopo.

Tuonavyo sisi, inabidi matukio haya ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kuchukua mikopo zaidi ya mara moja yachukuliwe kama makosa ya jinai ambayo yanastahili kufanyiwa kazi na vyombo ya sheria. Tusipofanya hivyo kuna hatari ya kulea kizazi ambacho hakina woga wala aibu kudokoa na kujipatia fedha za umma kwa njia za uongo na ulaghai.


Lililo baya ni kwamba uhalifu huu unafanyika wakati serikali ikiwa lawamani kila kukicha kwamba haitoi fedha za kutosha kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi watokao familia zisizo na uwezo kifedha kupata mikopo ya kuwaendeleza kielimu.

Sisi sote ni mashuhuda wa jinsi ambavyo wanafunzi katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu wanavyofanya maandamano, migomo na vurugu kwa madai ambayo kwa njia moja au nyingine yanahusiana na utoaji mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.

Kwamba mwaka huu kuna wanafunzi zaidi ya 18,000 waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja ni ishara kwamba upo uwezekano wa kuwapo kwa matukio mengine mengi ya udanganyifu katika uchukuaji wa mikopo. Hili tunaamini ni changamoto kwa Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi kulifanyia kazi na kama tulivosema si kwa maneno matupu bali kuliweka wazi kwa waombaji kwamba atakayebainika akifanya udanganyifu atachukuliwa hatua za kisheria na ikiwezekana anyimwe fursa ya kupata mikopo hiyo.

Tunaamini kwamba bila kuchukua hatua kali kama hizo hatutatenda haki kwa walipa kodi na maelfu ya wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo ya juu kwa kukosa mikopo ambayo kumbe inatumbuliwa na wenzao wasio waaminifu.

My Take:
a. Wamechelewa mwaka mmoja nyuma. Tulipoandika na kutoa ushahidi wa majina kuwa kuna kupewa mikopo mara mbili si walituambia tunawazushia? Wakati tunafuatilia wale vijana wa Ukraine 29 ambao waliambiwa serikali haina fedh hadi wakarudishwa nyumbani leo hii ndio wameamka kuangalia?

b. Ni uongo na uonevu kuwabebesha lawama wanafunzi wakati tulionesha tatizo lilipo. Tatizo haliko kwa wanafunzi, liko kwenye Bodi ya Mikopo. Tulipiga kelele na kuonesha hilo kwa data zilizowazi wakatukebehi, kweli wanafikiri kwa vile Daily News limeandika ndiyo mambo yatakuwa tofauti?

c. Tulipotoa taarifa za wizi wa fedha hizi kwa ushirikiano na watu wa bodi ya mikopo, tukataja na majina ya mifano na TAKUKURU wakasema wanafuatilia hizo kesi zimeishia wapi?

Tukubali tu, tunalo hili, tena tumelala nalo.
 
Mhariri
Daily News; Wednesday,July 23, 2008 @20:01

JANA katika gazeti hili tuliripoti kwamba wanafunzi takribani 10,000 waliojiunga na vyuo vya elimu ya juu mwaka jana walifanya udanganyifu na kujipatia mikopo ya elimu zaidi ya mara moja.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, wengi wa wanafunzi walipata mikopo hiyo kwa njia ya udanganyifu kutokana na kudahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja.

Katika mazingira ya mwaka huu ambako kuna zaidi ya wanafunzi 18,000 waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja, kuna hatari kwamba huenda kukawa na idadi kubwa ya wanafunzi wasio waaminifu ambao wanaweza kutumia fursa hiyo kuiba fedha kwa kisingizio kwamba hiyo ni mikopo.

Tuonavyo sisi, inabidi matukio haya ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kuchukua mikopo zaidi ya mara moja yachukuliwe kama makosa ya jinai ambayo yanastahili kufanyiwa kazi na vyombo ya sheria. Tusipofanya hivyo kuna hatari ya kulea kizazi ambacho hakina woga wala aibu kudokoa na kujipatia fedha za umma kwa njia za uongo na ulaghai.


Lililo baya ni kwamba uhalifu huu unafanyika wakati serikali ikiwa lawamani kila kukicha kwamba haitoi fedha za kutosha kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi watokao familia zisizo na uwezo kifedha kupata mikopo ya kuwaendeleza kielimu.

Sisi sote ni mashuhuda wa jinsi ambavyo wanafunzi katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu wanavyofanya maandamano, migomo na vurugu kwa madai ambayo kwa njia moja au nyingine yanahusiana na utoaji mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.

Kwamba mwaka huu kuna wanafunzi zaidi ya 18,000 waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja ni ishara kwamba upo uwezekano wa kuwapo kwa matukio mengine mengi ya udanganyifu katika uchukuaji wa mikopo. Hili tunaamini ni changamoto kwa Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi kulifanyia kazi na kama tulivosema si kwa maneno matupu bali kuliweka wazi kwa waombaji kwamba atakayebainika akifanya udanganyifu atachukuliwa hatua za kisheria na ikiwezekana anyimwe fursa ya kupata mikopo hiyo.

Tunaamini kwamba bila kuchukua hatua kali kama hizo hatutatenda haki kwa walipa kodi na maelfu ya wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo ya juu kwa kukosa mikopo ambayo kumbe inatumbuliwa na wenzao wasio waaminifu.

My Take:
a. Wamechelewa mwaka mmoja nyuma. Tulipoandika na kutoa ushahidi wa majina kuwa kuna kupewa mikopo mara mbili si walituambia tunawazushia? Wakati tunafuatilia wale vijana wa Ukraine 29 ambao waliambiwa serikali haina fedh hadi wakarudishwa nyumbani leo hii ndio wameamka kuangalia?

b. Ni uongo na uonevu kuwabebesha lawama wanafunzi wakati tulionesha tatizo lilipo. Tatizo haliko kwa wanafunzi, liko kwenye Bodi ya Mikopo. Tulipiga kelele na kuonesha hilo kwa data zilizowazi wakatukebehi, kweli wanafikiri kwa vile Daily News limeandika ndiyo mambo yatakuwa tofauti?

c. Tulipotoa taarifa za wizi wa fedha hizi kwa ushirikiano na watu wa bodi ya mikopo, tukataja na majina ya mifano na TAKUKURU wakasema wanafuatilia hizo kesi zimeishia wapi?

Tukubali tu, tunalo hili, tena tumelala nalo.

naona kijiji chetu kitapata haki yake ikiwa ni pamoja na kurudishwa kwa mashamba yetu yaliyoporwa na mafisadi
 
Kama ni kweli ni jambo la kusikitisha sana na tabia za kifisadi ni mambo kama haya na hao wanafunzi should suffer the consequence la sivyo watakuwa time bomb,lakini wakati huo huo hii inaonyesha incompetency ya hiyo bodi ya mikopo...waanze kwa kuweka sheria wazi kuwa mwanafunzi yeyote anayecheza huu mchezo mchafu akishikwa anapoteza haki zake zote za kupata mikopo hapo hapo laini above all lazima waweke sawa system yao ya kutoa mikopo ili kuzuia nonsense kama hizi maana wanao lose ni wengi
 
Ndo tatizo la taasisi zetu hapa TZ mpaka watu wapige kelele weeeeee ndo wanazibuka hivi aaah na tusipo piga kelele wao nao wanabaki kimya.Yaani viongozi wamezoea au wanatabia ya kufanya kazi kwa kusimamiwa na kusukumwa kama punda hivi hivi na wao wana baki kimya.Tatizo lina ripotiwa mapema lakini kulishughulikia inachukua mwaka.Angalia sasa wananfunzi wangapi ambao hawajapata mikopo kwa ajili ya uzembe wa hii bodi ni wengi sana angalia wengine wanapewa mara 2 hadi 3 kufatilia hawafatilii naona ni bora kuisafisha kabisa hii bodi ya mikopo hatuna uongozi kule wote wazembe tu.
 
wanafunzi mbona wanauanza ufisadi mapema!
mwanafunzi anayefanya hivi leo sidhani kama akipewa madaraka akapata kijinafasi cha kufisidi atashindwa.

tabia hii ni ya kukemewa...........na ni aibu kubwa kwa jamii yetu.
 
That means more than 10,000 Tanzanians were denied right for their education! I can’t believe this!
 
Nimeiona audited report yao sehemu ila haionyeshi kama kuna upotevu huo?

sasa sijui na auditors hawakuona hilo ,ngoja nitafute taarifa ile.
 
Mpaka Kieleweke, huwezi kuona hiyo kwenye audit report, kwa sababu unaangalia kutoka upande wa utoaji wa fedha badala ya Upokeaji. Wao wataweza kuonesha kiasi gani kilitoka na kiasi gani kilibakia. Sidhani kama wanaonesha majina ya wanafunzi wote waliopokea fedha hizo au vyuo vilivyopokea.
 
Mwanakijiji,mimi nina taarifa zenye idadi ya wanavyuo waliopokea mikopo kwa kila chuo.

Naweza kutumia takwimu hizo na kulinganisha na takwimu za idadi ya wanafunzi walioko kwenye vyuo husika na hapo tutaweza kuona ukweli kwani kama idadi ya waliolipwa ni kubwa kuliko idadi ya walioko vyuoni then tutaweza kufanya conclusions.

Itanichukua muda kidogo kuifanya hiyo analysis.
 
Nimeiona audited report yao sehemu ila haionyeshi kama kuna upotevu huo?

sasa sijui na auditors hawakuona hilo ,ngoja nitafute taarifa ile.

Kosa kubwa ambalo tumeendelea kulifanya tangu zamani ni kuunda TAASISI au SHIRIKA la UMMA kufanya AUDIT kwenye TAASISI/SHIRIKA jingine la UMMA. Tulikuwa na TAC kwa ajili ya MASHIRIKA ya UMMA; yote sasa hivi hayapo. Tukawa na COASCO kwa ajili ya VYAMA VYA USHIRIKA; vyote sasa hivi havipo. Tumekuwa na CAG kwa ajili ya IDARA na WIZARA za SERIKALI; wizi uko palepale hadi KESHO. Hatujifunzi tu tukabadili mfumo wa UKAGUZI na UDHIBITI wa RASILIMALI za NCHI?
 
Mwanakijiji,mimi nina taarifa zenye idadi ya wanavyuo waliopokea mikopo kwa kila chuo.

Naweza kutumia takwimu hizo na kulinganisha na takwimu za idadi ya wanafunzi walioko kwenye vyuo husika na hapo tutaweza kuona ukweli kwani kama idadi ya waliolipwa ni kubwa kuliko idadi ya walioko vyuoni then tutaweza kufanya conclusions.

Itanichukua muda kidogo kuifanya hiyo analysis.


Tunakusubili mzee, tuletee data tafadhali! Lakini si kweli kwamba wanafunzi wote wanapata mikopo, wengine wanasomeshwa na wazazi au wafadhili wao. Hapo itabidi uwe careful kuchambua ni wangapi wanajisomesha wenyewe kupitia wafadhili wao!
 
Mhariri
Daily News; Wednesday,July 23, 2008 @20:01

JANA katika gazeti hili tuliripoti kwamba wanafunzi takribani 10,000 waliojiunga na vyuo vya elimu ya juu mwaka jana walifanya udanganyifu na kujipatia mikopo ya elimu zaidi ya mara moja.

.................................................

Tuonavyo sisi, inabidi matukio haya ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kuchukua mikopo zaidi ya mara moja yachukuliwe kama makosa ya jinai ambayo yanastahili kufanyiwa kazi na vyombo ya sheria. Tusipofanya hivyo kuna hatari ya kulea kizazi ambacho hakina woga wala aibu kudokoa na kujipatia fedha za umma kwa njia za uongo na ulaghai.


.......................................

Hivi hicho kizazi hakipo sasa? EPA, Richmond, Kiwira, IPTL, Radar, Ndege ya Rais, Shekilango Road, Buzwagi, ATCL, BOT Twin Towers, ....... etc.

May be hapa ni watoto wanafuata nyayo za wazazi wao.

Kama akina RA, ENL, ANBEM, Yona, Chenge, Karamagi, Nchimbi, Warioba (Mzumbe) na akina Chitalilo wanadunda bila ya hofu, kwa nini wengine wasiweze pia?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom