Uchaguzi 2020 Mwaka huu hakuna Uchaguzi rahisi kama wengi tulivyodhani

EJM_

JF-Expert Member
Jul 8, 2011
3,836
2,090
Wiki moja tu iliyopita wengi wetu tulikuwa tunaamini uchaguzi wa mwaka huu utakuwa na landslide victory kwa CCM hasa kwenye nafasi ya Urais

Nachelea kusema hata Rais Magufuli mwenyewe aliamini atashinda kwa kishindo. Lakini tangu Tundu Lissu amerudi, mapokezi aliyoyapata mpaka kwenye tukio la kupitishwa kuwa mgombea Urais kupitia chama chake cha CHADEMA hali ya hewa imebadilika kabisa.

Nimeanza kuona kuanzia mtaani mpaka humu kwenye social media mitizamo imebadilika na kuona sasa uchaguzi sio rahisi tena kama ilivyodhaniwa

Baada ya hotuba ya kukubali kupeperusha bendera ya chama chake, Lissu aliongea mambo ambayo yametengeneza ajenda ambazo kwa kiasi kikubwa zimewashtua pia viongozi wa CCM. Hata ukiangalia press ya leo ya Polepole kuna dalili za kupanic ambazo zimefanya asiwe na ajenda maalum zaidi ya kuruka huku na huku.

Siasa ni mchezo usiotabirika na tukio moja linaweza kubadili mustakabali mzima wa muelekeo.

Na tusubiri tuone.
 
Unajua kutokuogopa hatari ni moja ya ugonjwa wa akili, lakini kuna watu wanahisi kwamba mwaka huu mambo yako sawa.

Tukicheza vibaya tu, nchi hii inaweza ikaingia kubaya ambako hakutakuwa na mtu kuirudisha kwenye mstari wake.

Lakini kuna wapumbavu bado wanaamini kwamba mambo yatakuwa kama siku zote au miaka mitano iliyopita.

I hope I'm wrong, lakini Tanzania inapita kipindi kigumu sana kwenye historia yake.
 
Unajua kutokuogopa hatari ni moja ya ugonjwa wa akili, lakini kuna watu wanahisi kwamba mwaka huu mambo yako sawa.
Tukicheza vibaya tu, nchi hii inaweza ikaingia kubaya ambako hakutakuwa na mtu kuirudisha kwenye mstari wake.
Lakini kuna wapumbavu bado wanaamini kwamba mambo yatakuwa kama siku zote au miaka mitano iliyopita.
I hope I'm wrong, lakini Tanzania inapita kipindi kigumu sana kwenye historia yake.
Good thinking
 
Unajua kutokuogopa hatari ni moja ya ugonjwa wa akili, lakini kuna watu wanahisi kwamba mwaka huu mambo yako sawa.
Tukicheza vibaya tu, nchi hii inaweza ikaingia kubaya ambako hakutakuwa na mtu kuirudisha kwenye mstari wake.
Lakini kuna wapumbavu bado wanaamini kwamba mambo yatakuwa kama siku zote au miaka mitano iliyopita.
I hope I'm wrong, lakini Tanzania inapita kipindi kigumu sana kwenye historia yake.
Upo sahihi kabisa mkuu apa CCM ikicheza vibaya inakwenda kutuingiza zaidi ya Zimbabwe tuna kodolewa macho kuliko wakati wowote ule!
Sijuwi nani aliwatuma wampige jamaa risasi!
 
Unajua kutokuogopa hatari ni moja ya ugonjwa wa akili, lakini kuna watu wanahisi kwamba mwaka huu mambo yako sawa.

Tukicheza vibaya tu, nchi hii inaweza ikaingia kubaya ambako hakutakuwa na mtu kuirudisha kwenye mstari wake.

Lakini kuna wapumbavu bado wanaamini kwamba mambo yatakuwa kama siku zote au miaka mitano iliyopita.

I hope I'm wrong, lakini Tanzania inapita kipindi kigumu sana kwenye historia yake.
Dah!...huu uchaguzi huenda ukabadilisha siasa za hili taifa kwa kiasi kikubwa.
 
Unajua kutokuogopa hatari ni moja ya ugonjwa wa akili, lakini kuna watu wanahisi kwamba mwaka huu mambo yako sawa.

Tukicheza vibaya tu, nchi hii inaweza ikaingia kubaya ambako hakutakuwa na mtu kuirudisha kwenye mstari wake.

Lakini kuna wapumbavu bado wanaamini kwamba mambo yatakuwa kama siku zote au miaka mitano iliyopita.

I hope I'm wrong, lakini Tanzania inapita kipindi kigumu sana kwenye historia yake.

Waswahili wanasema muungwana akiangukwa na taulo huchutama, kuna watu wanatakiwa wafanye hili kwenye kipindi hiki hasa polisi, wakurugenzi, NEC na msajili wa vyama.

Kuna chance kubwa ya kufanya uchaguzi ukawa huru na bado wakashinda but lazima waondoe hofu kwanza
 
Upo sahihi kabisa mkuu apa CCM ikicheza vibaya inakwenda kutuingia zaidi ya Zimbabwe tuna kodolewa macho kuliko wakati wowote ule!
Sijuwi nani aliwatuma wampige jamaa risasi!
Ni hatari kubwa mnoo .. Lile tukio limezalisha Chuki katika vifua vya watu wengi sana dhidi ya Serikali kuu

Hata hivyo pia hatujui nyuma ya lissu kuna kina nani Toka katika mataifa makubwa ambao wanampa support .. kama jiwe amevuruga mahusiano yake na nchi zinazo itawala hii dunia trust me jamaa wanaweza kumtumia lissu kumng'oa jiwe madarakani ...

Kama ccm haijajiandaa mapema mwaka huu itakula kwao na wataimba hallelujah
 
Yaani huu ni uchaguzi mwepesi kwa CCM tangu mfumo wa vyama vingi uanze, kwasababu hadi muda huu tayari tumeishashinda nafasi ya URAIS tunachohangaika nacho nikuhakikisha hakuna hata Jimbo linaenda upinzani hiyo ndiyo kazi ngumu iliyoko mbele ya CCM.
 
Back
Top Bottom