Mwaka 2025: Selemani Jaffo ni mgombea wa CCM urais(?)

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
15,635
29,967
Ni pale ambapo huwa namtafuta mchora ramani wa CCM na kugundua kuwa watakuwa wana nguvu ya ziada ,
Kwa kuwa ni mapema mno na ndo Mheshimiwa ana mwaka mmoja madarakani, ni kawaida ya CCM kujitokeza watu wa kugombea nafasi za juu na maandaliz huanza mapema mno,

Tetesi za utaratibu unaosukwa mpaka najiuliza sana kuwa nani hasa uwa anawashauri katika masuala haya, maana mnapoanza kuhisi wameishiwa wanakuwa na mtu mpya ambaye ni wa kushangaza ambaye hakutegemewa,

Nilitamani nitaje jina lake lakin naona nisije nikasababisha akaanza kuchafuliwa na timu mbali mbali zinazosaka madaraka, nimeainisha kifupi tu cha jina lake , kuwa ndiye atakaye shika wadhifa wa juu baada ya uongozi wa Mh tuliyenaye, kutokana na habari za karibu nilizonazo zimeonesha kuwa mpango wa kumuandaa kijana Huyo kujiandaa kisaikolojia kwa awamu ijayo,

Miongozo na mienendo aliyopewa kijana huyo ni siri ambazo hapaswi kuzijua mwingine,

Sifa zake zilizoina haraka haraka
1. Ni msomi
2. Mtaratibu mwenye maamuzi sahihi
3. Afya njema na mungu tunaomba amlinde sana
4. Ni dini Fulani ambayo sitaki kuitaja,
6. Ni wa kanda ile ya upande unaoonekana kupata marais wengi kutoka.upande uo,
7. Si msemaji ni mtendaji tu.
8. Ni mtiifu kwa wananchi

Safari imeanza, sasa, asante jopo la wazee 13 kuendelea kutuletea vijana na kuwaandaa


Kila la heri SULEIMAN JAFFO
 
Kama sio January makamba basi ni Jafo suleiman maana ndio wanatokea ukanda wa pwani unaotoa marais wengi kama wakina mwinyi, mkapa, Kikwete

Japo pia siwezi kumsahau na Shamshi vuai Naodha japo safari hii kaachwa kwenye baraza la mawaziri sijui tatizo nini?!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom