Mwaka 2021 umeshika nafasi ya sita kwa joto zaidi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Utafiti wa hali ya joto duniani na mashirika mawili ya Marekani umeonyesha kuwa mwaka 2021 umeshika nafasi ya sita wenye joto zaidi duniani.

Takwimu za hivi karibuni zilizokusanywa na Shirika la taifa la Marekani linaloshughulikia utafiti wa anga za mbali, NASA na Idara ya Bahari na Anga ya Marekani, NOAA zinasisitiza kuhusu mzozo wa hali ya hewa duniani.

Kulingana na NASA, mwaka 2021 umefungana na mwaka 2018 kwa nafasi ya sita ambayo hutumia kipindi cha miaka 30.

Uchambuzi tofauti wa NOAA umeonyesha wastani wa hali ya joto kwa mwaka 2021 ulikuwa na nyuzi joto 1.51 za kipimo cha Celsius juu ya viwango vya karne ya 20, na kuufanya mwaka uliopita kuwa katika nafasi ya sita, mbele ya mwaka 2018.

Maafisa wamesema hiyo ni sehemu ya hali ya joto ya muda mrefu ambayo inaonyesha dalili za kuongezeka kasi.

DW Swahili
 
mwaka 2021 umeshika nafasi ya sita wenye joto zaidi duniani
Kwani kipimo ni kati ya dunia na sayari zingine, ama katika vipindi mbalimbali vya historia ya dunia. Your logic is purely poor!

You should have said, instead: ^mwaka 2021 umeshika nafasi ya sita wenye joto zaidi katika historia ya dunia,^ or something similar.
 
Mwaka 2021 ndo umeonyesha kuanza kwa matukio ya kuvunja rekodi kwenye viwango vya tabia nchi, ikiashiria kwamba dunia itaendelea kushuhudia madhara ya yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo viwango vya joto kali na baridi iliyopindukia, mvua zisizo tabirika, ukame, majanga ya mioto ya nyikani nk........kiimani pia ni dalili za kuelekea mwisho wa dunia kwa wale wanaoweza kusoma signal kadri ya maandiko.
 
Kwani kipimo ni kati ya dunia na sayari zingine, ama katikati vipindi mbalimbali vya historia ya dunia. Your logic is purely poor!

You should have said, instead: ^mwaka 2021 umeshika nafasi ya sita wenye joto zaidi katika historia ya dunia,^ or something similar.
Anzisha Uzi wako ielezee vizuri mkuu
 
Back
Top Bottom