TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,866
- 5,742
Nimewaza sana,
Chaguzi zilizotangulia, Vyama vya upinzani nchini vilitumia sana changamoto za kisiasa, Kiuchumi na Kijamii zilizokuwa zikiikabili nchi yetu katika kuandaa ilani za Uchaguzi za vyama vyao.
1. Huduma duni za Afya, Elimu, Umeme,Maji, barabara zilikuwa ni changamoto sana awamu zilizopita.
2. Mfumuko wa bei, uzembe kazini, miungu watu kwenye taasisi za Umma, unyanyasaji wa wafanyabiashara ndogo ndogo(Mama ntilie, Bodaboda, Wamachinga
) , watu kunyang'anywa mali zao(Mashamba, nyumba, viwanja) ni mambo ambayo yalikuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa kawaida.
3. Ufisadi, rushwa, ukwepaji kodi halikadhalika yalikuwa na matatizo sugu nchini.
4. Matumizi mabaya ya rasimali za taifa(Madini, Gesi, misitu, Mbuga za Wanyama) vilevile kwa muda mrefu yamekuwa donda ndugu.
5. Kukosekana kwa uwekezaji wenye kujenga uchumi endelevu wa taifa kama Ndege, Reli, Umeme ni miongoni mwa mambo ambayo waliumiza sana vichwa vya viongozi wetu bila ya mafanikio.
Wapinzani walitumia changamoto hizi kuwaonesha wananchi kuwa Serikali inayoongozwa na CCM kwa vipindi vyote ilifikia kikomo na isingeweza kukabiliana na changamoto hizi. Ilani za Vyama hivi zimekuwa zikizimulika changamoto hizi.
Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Bulldozer, Jiwe, Watapata tabu sana, Dkt. John Pombe Magufuli imedhihirisha kwa vitendo ndani ya kipindi cha miaka miwili na nusu kuwa inawezekana. Wote wanaobeza namna Serikali hii inavyokabiliana na changamoto hizi, wanatapatapa tu, wengine wanaukubali utekelezaji huu ila wanafanya propaganda tu japo nao waendelee kuonekana kuwa wapo lakini kimsingi kisiasa wamefilisika.
Natafakari tu, 2020 wapinzani watakuwa na kipi cha kuandika kwenye ilani zao.
Chaguzi zilizotangulia, Vyama vya upinzani nchini vilitumia sana changamoto za kisiasa, Kiuchumi na Kijamii zilizokuwa zikiikabili nchi yetu katika kuandaa ilani za Uchaguzi za vyama vyao.
1. Huduma duni za Afya, Elimu, Umeme,Maji, barabara zilikuwa ni changamoto sana awamu zilizopita.
2. Mfumuko wa bei, uzembe kazini, miungu watu kwenye taasisi za Umma, unyanyasaji wa wafanyabiashara ndogo ndogo(Mama ntilie, Bodaboda, Wamachinga
) , watu kunyang'anywa mali zao(Mashamba, nyumba, viwanja) ni mambo ambayo yalikuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa kawaida.
3. Ufisadi, rushwa, ukwepaji kodi halikadhalika yalikuwa na matatizo sugu nchini.
4. Matumizi mabaya ya rasimali za taifa(Madini, Gesi, misitu, Mbuga za Wanyama) vilevile kwa muda mrefu yamekuwa donda ndugu.
5. Kukosekana kwa uwekezaji wenye kujenga uchumi endelevu wa taifa kama Ndege, Reli, Umeme ni miongoni mwa mambo ambayo waliumiza sana vichwa vya viongozi wetu bila ya mafanikio.
Wapinzani walitumia changamoto hizi kuwaonesha wananchi kuwa Serikali inayoongozwa na CCM kwa vipindi vyote ilifikia kikomo na isingeweza kukabiliana na changamoto hizi. Ilani za Vyama hivi zimekuwa zikizimulika changamoto hizi.
Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Bulldozer, Jiwe, Watapata tabu sana, Dkt. John Pombe Magufuli imedhihirisha kwa vitendo ndani ya kipindi cha miaka miwili na nusu kuwa inawezekana. Wote wanaobeza namna Serikali hii inavyokabiliana na changamoto hizi, wanatapatapa tu, wengine wanaukubali utekelezaji huu ila wanafanya propaganda tu japo nao waendelee kuonekana kuwa wapo lakini kimsingi kisiasa wamefilisika.
Natafakari tu, 2020 wapinzani watakuwa na kipi cha kuandika kwenye ilani zao.