Philipo Mwakibinga
Senior Member
- May 13, 2013
- 111
- 175
Najua ukweli ni mchungu lakini nidawa hivyo lazima tuunywe ilitupone, na yeyote anayeshiriki kumnyima au kutompa dawa mgonjwa kwa wakati ni muuwaji na msababishaji wa madhara yeyote yanayoweza kumkuta mgonjwa.
CCM tufanye siasa tuache migogoro na marumbano baina yetu. Tuache siasa za kuviziana na umimi,siasa za nani katoka wapi na nani yuko wapi, siasa za nani alipitia chipukizi gani na nani anajua kufunga skafu.
Uchaguzi uliopita tulikuwa na hali mbaya bahati nzuri ni aliyekuwa Mwenyekiti wetu hayati J.P Magufuli kuamua kubeba mzigo ili chama kinusurike. Lazima tukubali hili na huo ndiyo ukweli kama nitachukiwa nichukiwe lakini itabidi nikumbushe hili maana tumejisahau kama siyokujisahaulisha kwa makusudi.
Magufuli aliagiza Wakurugenzi ilitushinde, sote tunajua alisema kuwa mkurugenzi anayemlipa mshahara na usafiri kisha akamtangaza mpinzani atafute kwa kwenda. Nani alikubali kutafuta kwa kwenda na akamtangaza mpinzani? Hili lilitusaidia sana kushinda chaguzi maana sote tunajua nguvu ya mkurugenzi katika chaguzi zetu kwa mujibu wa sheria za hapa TANZANIA.
Magufuli kumnadi mgombea kwa Wanachi. Tulipokuwa kwenye kampeni ilikuwa lazima useme kwa Wananchi kuwa huyu mgombea anapendwa na Magufuli. Hii ilisaidia sana kwani Magufuli aliaminiwa na kupendwa na Watanzania hivyo sifa ya kiongozi bora ilipimwa kutokana na imani ya Magufuli kwa kiongozi husika.
Mfano nipale Magufuli alisimama mwenyewe na kuwaambia Wananchi kuwa kama mnataka maendeleo nileteeni huyu au yule... nileteeni Gwajimaaaa.. nk, nk. Ndiyo maana wabunge wa CCM wanajua hili kuwa wapo baadhi yao wasingekua Wabunge kama asingekua Magufuli hapa nitamtaja Baba yangu Kabudi anakumbuka Rais alivyomnadi waziwazi hata kabla mbunge wa pale hajamaliza muda wake.
Hivyo ni ukweli usiopingika kuwa Magufuli alipambana na Upinzani huku wanachama tukiwa nyuma yake tukishangilia. Tunakumbuka nguvu ya upinzani kwanzia miaka ya 2010 namna ilivyodhoofishwa kwanzia mwaka 2015 baada ya kuwekewa vikwazo vya kisiasa kwakutumia dolla.
Tunakumbuka namna tulivyosumbuliwa na watu ambao kwamiaka hawakuwa na serikali na hawakufanya mikutano ya hadhara bali walishinda mahakamani kushughulikia kesi tulizowatungia wakati fulani ilikuwapunguza nguvu. Mfano ni zile walizoshinda na zingine kufutiwa. Tujihadhari uchaguzi ujao tuwe makini hali inaweza kuwa mbaya zaidi.
Leo nasikitika makundi yameanza mapema tena yenye uadui mkubwa sana. Kunawatu wameanza uchokonozi na wanatamani kuwe na CCM wazanzibar, CCM wabara. Wakati CCM wabara wao wanaccm nyingine nyingi humo humo kuna CCM mwendazake,CCM asili na CCM tumehamia. Kesho kutazuka CCM waislam na CCM wakristo tunakwenda wapi? Dalili hizi zinaonekana maana kila linalofanyika watu wanahesabiana, haya ni mambo ya ajabu ambaya zaidi naona viongozi wakongwe wenye hekima na busara zao wameamua kuyakalia kimya sijui kwa manufaa ya nani?
Baba wa Taifa hili Mwalimu Nyerere alipata kusema tuwaandae vijana watakao kuwa WAHASI DHIDI YA MFUMO KANDAMIZI. Kuendelea kuichekea Hii mifumo ya hovyo inayoanza kumea kwenye chama kwa ndoto za Udas na Udc ni ukosefu wa mipango na nikushiriki kwa makusudi kuhujumu nchi. Tanzania hii itabaki na sote tutapita, Mungu ameshatuonyesha dhahiri kuwa madaraka na jeuri mwisho wake ni mashada ya maua na matarumbeta basi! Kwasababu tuliishia kuyaona na kuyasikia kwa majirani kwa miaka yote.
Kama tutaacha kufanya siasa na kuendelea kushughurikiana kwa kushupaza shingozetu tutalia msiba usiona jina na usio na mzishi. Watanzania wa mwaka 1990 siyo hawa wa mwaka 2020 itafika sikumoja kukosa hata mjumbe wa kugombea kupitia ccm kwasababu watu watachoka. Afrika kulikuwa na vyama vingi tu vyaukombozi leo vikowapi? Dolla itashindwa kutulinda maana sikuhizi sote tunashare matatizo na shida tofauti na zamani. Tufanye siasa tuache haya tunayoyaanza sasa.
Viongozi tuliowaamini na kuwapa madaraka tuwasaidie na kuwakumbusha wanapokosea. Kuendelea kuwazodoa na kuwahujumu si busara kwani wao ni sehemu yetu. Watanzania wanaona na kusikia hatuna mtu wa kumsingizia endapo tutashindwa kufanya yale tuliyowaahidi. Kuna mambo ya msingi ya kushughurikia kuliko kutafutana na kusagiana kunguni wakati tukijua maisha ya siasa ni mafupi sana kuliko hata maisha ya funza. Unayemuonea leo na kumdharau kesho anakua mkuu wako na akitaka kukunyoosha anakunyoosha mno. Tujifunze kupitia matukio makubwa yaliyotupita hivi karibuni.
Wanaccm tushughulikie matatizo ya watu bado mambo hayajakaa sawa kwenye mfumo mzima wa maisha. Bado hali za bidhaa na bei zake siyo rafiki kila kukicha, uwajibikaji kwa viongozi wetu unaporomoka hata mh rais amegusia hili mara kadhaa kuwa kuna mambo yameanza kujitokeza hayakuwepo hapo nyuma.
Sikuzote mtoto wa Samaki huwa anahusiwa kuchunga mdomo maana ndoano huwa karibu.
Philipo Mwakibinga
0758910403.
CCM tufanye siasa tuache migogoro na marumbano baina yetu. Tuache siasa za kuviziana na umimi,siasa za nani katoka wapi na nani yuko wapi, siasa za nani alipitia chipukizi gani na nani anajua kufunga skafu.
Uchaguzi uliopita tulikuwa na hali mbaya bahati nzuri ni aliyekuwa Mwenyekiti wetu hayati J.P Magufuli kuamua kubeba mzigo ili chama kinusurike. Lazima tukubali hili na huo ndiyo ukweli kama nitachukiwa nichukiwe lakini itabidi nikumbushe hili maana tumejisahau kama siyokujisahaulisha kwa makusudi.
Magufuli aliagiza Wakurugenzi ilitushinde, sote tunajua alisema kuwa mkurugenzi anayemlipa mshahara na usafiri kisha akamtangaza mpinzani atafute kwa kwenda. Nani alikubali kutafuta kwa kwenda na akamtangaza mpinzani? Hili lilitusaidia sana kushinda chaguzi maana sote tunajua nguvu ya mkurugenzi katika chaguzi zetu kwa mujibu wa sheria za hapa TANZANIA.
Magufuli kumnadi mgombea kwa Wanachi. Tulipokuwa kwenye kampeni ilikuwa lazima useme kwa Wananchi kuwa huyu mgombea anapendwa na Magufuli. Hii ilisaidia sana kwani Magufuli aliaminiwa na kupendwa na Watanzania hivyo sifa ya kiongozi bora ilipimwa kutokana na imani ya Magufuli kwa kiongozi husika.
Mfano nipale Magufuli alisimama mwenyewe na kuwaambia Wananchi kuwa kama mnataka maendeleo nileteeni huyu au yule... nileteeni Gwajimaaaa.. nk, nk. Ndiyo maana wabunge wa CCM wanajua hili kuwa wapo baadhi yao wasingekua Wabunge kama asingekua Magufuli hapa nitamtaja Baba yangu Kabudi anakumbuka Rais alivyomnadi waziwazi hata kabla mbunge wa pale hajamaliza muda wake.
Hivyo ni ukweli usiopingika kuwa Magufuli alipambana na Upinzani huku wanachama tukiwa nyuma yake tukishangilia. Tunakumbuka nguvu ya upinzani kwanzia miaka ya 2010 namna ilivyodhoofishwa kwanzia mwaka 2015 baada ya kuwekewa vikwazo vya kisiasa kwakutumia dolla.
Tunakumbuka namna tulivyosumbuliwa na watu ambao kwamiaka hawakuwa na serikali na hawakufanya mikutano ya hadhara bali walishinda mahakamani kushughulikia kesi tulizowatungia wakati fulani ilikuwapunguza nguvu. Mfano ni zile walizoshinda na zingine kufutiwa. Tujihadhari uchaguzi ujao tuwe makini hali inaweza kuwa mbaya zaidi.
Leo nasikitika makundi yameanza mapema tena yenye uadui mkubwa sana. Kunawatu wameanza uchokonozi na wanatamani kuwe na CCM wazanzibar, CCM wabara. Wakati CCM wabara wao wanaccm nyingine nyingi humo humo kuna CCM mwendazake,CCM asili na CCM tumehamia. Kesho kutazuka CCM waislam na CCM wakristo tunakwenda wapi? Dalili hizi zinaonekana maana kila linalofanyika watu wanahesabiana, haya ni mambo ya ajabu ambaya zaidi naona viongozi wakongwe wenye hekima na busara zao wameamua kuyakalia kimya sijui kwa manufaa ya nani?
Baba wa Taifa hili Mwalimu Nyerere alipata kusema tuwaandae vijana watakao kuwa WAHASI DHIDI YA MFUMO KANDAMIZI. Kuendelea kuichekea Hii mifumo ya hovyo inayoanza kumea kwenye chama kwa ndoto za Udas na Udc ni ukosefu wa mipango na nikushiriki kwa makusudi kuhujumu nchi. Tanzania hii itabaki na sote tutapita, Mungu ameshatuonyesha dhahiri kuwa madaraka na jeuri mwisho wake ni mashada ya maua na matarumbeta basi! Kwasababu tuliishia kuyaona na kuyasikia kwa majirani kwa miaka yote.
Kama tutaacha kufanya siasa na kuendelea kushughurikiana kwa kushupaza shingozetu tutalia msiba usiona jina na usio na mzishi. Watanzania wa mwaka 1990 siyo hawa wa mwaka 2020 itafika sikumoja kukosa hata mjumbe wa kugombea kupitia ccm kwasababu watu watachoka. Afrika kulikuwa na vyama vingi tu vyaukombozi leo vikowapi? Dolla itashindwa kutulinda maana sikuhizi sote tunashare matatizo na shida tofauti na zamani. Tufanye siasa tuache haya tunayoyaanza sasa.
Viongozi tuliowaamini na kuwapa madaraka tuwasaidie na kuwakumbusha wanapokosea. Kuendelea kuwazodoa na kuwahujumu si busara kwani wao ni sehemu yetu. Watanzania wanaona na kusikia hatuna mtu wa kumsingizia endapo tutashindwa kufanya yale tuliyowaahidi. Kuna mambo ya msingi ya kushughurikia kuliko kutafutana na kusagiana kunguni wakati tukijua maisha ya siasa ni mafupi sana kuliko hata maisha ya funza. Unayemuonea leo na kumdharau kesho anakua mkuu wako na akitaka kukunyoosha anakunyoosha mno. Tujifunze kupitia matukio makubwa yaliyotupita hivi karibuni.
Wanaccm tushughulikie matatizo ya watu bado mambo hayajakaa sawa kwenye mfumo mzima wa maisha. Bado hali za bidhaa na bei zake siyo rafiki kila kukicha, uwajibikaji kwa viongozi wetu unaporomoka hata mh rais amegusia hili mara kadhaa kuwa kuna mambo yameanza kujitokeza hayakuwepo hapo nyuma.
Sikuzote mtoto wa Samaki huwa anahusiwa kuchunga mdomo maana ndoano huwa karibu.
Philipo Mwakibinga
0758910403.