Zanzibar 2020 Mwaka 2015, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo, mwaka huu wa 2020 watakuja na mbinu gani?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Wadau, hili ndio swali tunalopaswa kujiuliza kwa kuzingatia yaliyotokea mwaka 2015 ambapo matokeo ya uchaguzi yalifutwa na Bwana Jecha ambae ndio alikuwa kiongozi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Binafsi na ni imani yangu tuko wengi tunaoamini kuwa hata mwaka huu Maalim Seif atashinda uchaguzi huko Zanzibar kama dalili zinavyoonyesha.

Swali hapa ni je, safari hii atatangazwa mshindi iwapo atashinda?

Wasipomtangaza, wamejipanga kufanya nini au muda ndio utajua nini kifanyike?

Na wapinzani safari hii walivyopania, watakubali kutotangazwa washindi iwapo watakuwa na uhakika wameshinda huko Visiwani na hata huku Bara?

Pengine swali gumu kuliko yote ni je, Maalim Seif akiingia Ikulu ya Zanzibar, ataacha kuitisha kura ya maoni Wazanzibar waamue hatima ya Muungano?

Tuombe uzima kuona Taifa hili likirekodi historia mpya mwaka huu kuhusiana na maswala ya uchaguzi Bara na Visiwani.
 
Mbinu zimewaishia. Zile 1000 walizosema ziliisha mwaka 2015 ambapo ilibidi watunie ya mwisho kabisa ya kufuta uchaguzi. Sasa.mwaka huu sinui labda watumie mabomu na mizinga. Ambayo kihistoria haijawahi kushinda sehemu yoyote duniani.
 
Hujiulizi kwanini mwaka huu Kuna kundi linapiga kura tarehe 27 October, na jingine tarehe 28 huko visiwani?. Huku bara Raisi atakayeapishwa November tayari anafahamika tu. Wengine wanachamgamsha uchumi mikoani kuongeza mzunguko wa pesa mtaani.
 
Wewe umeambiwa uchaguzi utafanyika siku mbili. Siku ya Kwanza watapiga polisi na wasimamizi wa uchaguzi. Jiulize nani atasimamia uchaguzi wa siku ya kwanza. Kura za siku ya kwanza zitahifadhiwa wapi. Nani atashuhudia ujumlishaji wa kura za siku ya kwanza na siku ya pili?
 
Wewe umeambiwa uchaguzi utafanyika siku mbili.. Siku ya Kwanza watapiga polisi na wasimamizi wa uchaguzi. Jiulize nani atasimamia uchaguzi wa siku ya kwanza. Kura za siku ya kwanza zitahifadhiwa wapi. Nani atashuhudia ujumlishaji wa kura za siku ya kwanza na siku ya pili?
Kama ni hivyo basi imeshakula kwetu.
 
Hujiulizi kwanini mwaka huu Kuna kundi linapiga kura tarehe 27 October, na jingine tarehe 28 huko visiwani?. Huku bara Raisi atakayeapishwa November tayari anafahamika tu. Wengine wanachamgamsha uchumi mikoani kuongeza mzunguko wa pesa mtaani.
Uchaguzi siku mbili wamefeli kwahiyo hilo kundi la mwanzo watapiga vp kura za kumchagua mbunge na Rais wa mungano wakati itakua tarehe 28 haijafika
 
Wadau, hili ndio swali tunalopaswa kujiuliza kwa kuzingatia yaliyotokea mwaka 2015 ambapo matokeo ya uchaguzi yalifutwa na Bwana Jecha ambae ndio alikuwa kiongozi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Binafsi na ni imani yangu tuko wengi tunaoamini kuwa hata mwaka huu Maalim Seif atashinda uchaguzi huko Zanzibar kama dalili zinavyoonyesha.

Swali hapa ni je, safari hii atatangazwa mshindi iwapo atashinda?

Wasipomtangaza, wamejipanga kufanya nini au muda ndio utajua nini kifanyike?

Na wapinzani safari hii walivyopania, watakubali kutotangazwa washindi iwapo watakuwa na uhakika wameshinda huko Visiwani na hata huku Bara?

Pengine swali gumu kuliko yote ni je, Maalim Seif akiingia Ikulu ya Zanzibar, ataacha kuitisha kura ya maoni Wazanzibar waamue hatima ya Muungano?

Tuombe uzima kuona Taifa hili likirekodi historia mpya mwaka huu kuhusiana na maswala ya uchaguzi Bara na Visiwani.
Unasubiri ZEC watafananya nini au wazanzibari watafanya maamuzi gani ? Nawashauri wazanzibari wenzangu wafanye maamuzi magumu, huyo mtoto wa Mwinyi sidhani kama ana ufahamu wa matatizo waliyonayo wazanzibari. Ukimsikiliza ahana dira yoyote ya uongozi, ana mawazo ya kuwa kucopy na kupaste idea za mambo aliyojifunza kutoka Tanganyika.

Labda nimkubushe tuu kajisahau Zanzibar ni tofauti sana na Tanganyika. Kisiasa, sera za kiuchumi, silka na utamaduni. Zipo sehemu za Tanganyika na hata Kenya zinafanana na Zanzibar.

Kusema utaiga ajenda yako kuu ni kuiga uongozi wa Magufuli kwenda nao Zanzibar au kusema ajenda yako kuu ni kupigania rushwa. Mbona Zanzibar kuna matatizo yenye prio zaidi ya hili ? Nasisitiza priority/vipa umbele ni muhimu katika uongozi.

Mambo ni mengi, lakini kila kiongozi huchagua yale muhimu na kuanza kuyatanguliza. Nimalize kwa kuwakumbusha wazanzibari kama wana wajibu wa kuilinda demokrasia na uhuru na hadhi ya visiwa vya Zanzibar. Hili si jukumu la Magufuli wala Seif, ni kila mmoja kama mwananchi ana haki ya kuhakikisha anatekeleza jukumu lake kama yeye binafsi.
 
Nimesahau Zanzibar kwanza! Hii ndio iwe ajenda ya kila mzanzibari. Kiongozi asie na maslahi na wazanzibari aekwe kando kwa hali na mali.

Wasalaam
 
Kwa Sjingo upande Maalim atatangazwa lakini Serikali yake haitaachiwa kufanya yale ambayo itataka kufanya hususani yaliyo kwenye muungano.
Unasubiri ZEC watafananya nini au wazanzibari watafanya maamuzi gani ? Nawashauri wazanzibari wenzangu wafanye maamuzi magumu, huyo mtoto wa Mwinyi sidhani kama ana ufahamu wa matatizo waliyonayo wazanzibari. Ukimsikiliza ahana dira yoyote ya uongozi, ana mawazo ya kuwa kucopy na kupaste idea za mambo aliyojifunza kutoka Tanganyika.

Labda nimkubushe tuu kajisahau Zanzibar ni tofauti sana na Tanganyika. Kisiasa, sera za kiuchumi, silka na utamaduni. Zipo sehemu za Tanganyika na hata Kenya zinafanana na Zanzibar. Kusema utaiga ajenda yako kuu ni kuiga uongozi wa Magufuli kwenda nao Zanzibar au kusema ajenda yako kuu ni kupigania rushwa. Mbona Zanzibar kuna matatizo yenye prio zaidi ya hili ? Nasisitiza priority/vipa umbele ni muhimu katika uongozi.

Mambo ni mengi, lakini kila kiongozi huchagua yale muhimu na kuanza kuyatanguliza. Nimalize kwa kuwakumbusha wazanzibari kama wana wajibu wa kuilinda demokrasia na uhuru na hadhi ya visiwa vya Zanzibar. Hili si jukumu la Magufuli wala Seif, ni kila mmoja kama mwananchi ana haki ya kuhakikisha anatekeleza jukumu lake kama yeye binafsi.
 
Back
Top Bottom