Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,062
- 2,289
Niliajiriwa na kampuni fulani ya binafsi hapa Dar. Taratibu zote za ajira zilifuatwa. Bahati mbaya nikiwa nimetimiza miezi miwili kukatokea kutoelewana pale kazini kati yangu na mmoja wa wamiliki wa kampuni. Baada ya siku mbili nikapewa barua ya kufukuzwa kazi. Nikaenda Tume ya Usuluhishi na Uamuzi kulalamika. Niliomba kurudishwa kazini kwa sababu taratibu za kufukuzwa hazikifuatwa kwa kuwa sikusikilizwa. Nikafuata taratibu zote. Usuluhishi ukaanza, haukuzaa matunda. Tukaanza Uamuzi, wakati inaanza kusikilizwa Mwamuzi akinitaka nitoe maelezo kuhusu haki yangu ya kurudishwa kazini wakati nimefanya miezi miwili tu. Wakati wa uamuzi wake akasema kuwa mfanyakazi aliyefanya kazi chini ya miezi sita hana haki ya kudai kurudishwa kazini wala kudai haki yoyote kwa kuwa haki ya kurudishwa kazini au kulipwa ni kwa waajiriwa waliofanya kazi zaidi ya miezi sita. Nikabaki hoi. Nikatafuta ufafanuzi kwa wansheria wakasema hilo jambo linajulikana kwenye duru za Kimahakama na kinachotakiwa ni mtu wa kufungua kesi ya kikatiba kupinga vifungu vinavyomnyima haki ya msingi mfanyakazi hata kama ameonewa. Akitokea mwanasheria ambaye angependa kusoma hukumu niliyopewa ani-pm nimtumie.