Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
[h=2][/h]
Kijana pichani Nelson Fonangwan mwenye miaka 17 amefanya hivyo.Alikuwa amelala nyumbani kwao na kuamshwa na kelele za majirani ambao walikuwa wakiunguliwa na nyumba.
Aliamka na kwenda kuangalia nini kinaendelea akakuta nyumba ya jirani ikiungua na mama mwenye watoto wawili akihangaika kuvunja dirisha kwenda kumuokoa mtoto wake mdogo Adam mwenye miaka 2.
Mama alivunja dirisha bila mafanikio huku moto ukizidi kuwaka ndipo Nelson alipokuja akavunja dirisha na kuingia ndani kumuokoa mtoto.Mama akapiga simu 999 ikaja gari ya zimamoto.
Akisimulia moto ulivyotokea mama wa mtoto anasema alikuwa ameenda nje kutupa uchafu akiwa amemuacha mwanae mdogo jikoni.Kurudi mlango ukawa umejifunga na kumbe aliacha fying pan jikoni ikaanza kuungua na baadae moto kuanza kuwa mkubwa.Alijitahidi kuvunja dirisha na mkono ambao aliumia sana huku akipiga kelele ndio kijana Nelson kutokea na kumsaidia.
Tukio hili lilitokea nchini Uingereza maeneo ya Southampton.Kijana Nelson Fonangwan asili yake ni Cameroon.
Kijana pichani Nelson Fonangwan mwenye miaka 17 amefanya hivyo.Alikuwa amelala nyumbani kwao na kuamshwa na kelele za majirani ambao walikuwa wakiunguliwa na nyumba.
Aliamka na kwenda kuangalia nini kinaendelea akakuta nyumba ya jirani ikiungua na mama mwenye watoto wawili akihangaika kuvunja dirisha kwenda kumuokoa mtoto wake mdogo Adam mwenye miaka 2.
Mama alivunja dirisha bila mafanikio huku moto ukizidi kuwaka ndipo Nelson alipokuja akavunja dirisha na kuingia ndani kumuokoa mtoto.Mama akapiga simu 999 ikaja gari ya zimamoto.
Akisimulia moto ulivyotokea mama wa mtoto anasema alikuwa ameenda nje kutupa uchafu akiwa amemuacha mwanae mdogo jikoni.Kurudi mlango ukawa umejifunga na kumbe aliacha fying pan jikoni ikaanza kuungua na baadae moto kuanza kuwa mkubwa.Alijitahidi kuvunja dirisha na mkono ambao aliumia sana huku akipiga kelele ndio kijana Nelson kutokea na kumsaidia.
Tukio hili lilitokea nchini Uingereza maeneo ya Southampton.Kijana Nelson Fonangwan asili yake ni Cameroon.