Mvuto wa CHADEMA kwa wananchi utaiangamiza CCM-Dk Bana

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, amesema wimbi la vijana wa CCM kukikimbia na kujiunga na Chadema ni dalili mbaya na kukitaka chama hicho kuwavua magamba wanachama wao wanaowatuhumu kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya ufisadi badala ya kusubiri wajivue wenyewe.

Dk. Bana, alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam pembeni mwa mkutano wa mtengamano wa kisiasa wa Afrika Mashariki.

Alisema kuna watu wengi wanaotaka kukihama CCM na kujiunga na Chadema hivi sasa, lakini wanashindwa kufanya hivyo kutokana na ugumu wa mioyo yao kisiasa.

“CCM isisubiri wanachama wao wenyewe kujivua gamba na kisha vigogo kuanza kusema kwamba watu wa aina hiyo walikuwa hawawahitaji badala yake chama kiwavue kabla,” alisema Dk. Bana.

Alifafanua kuwa wimbi hilo la vijana pamoja na watu wengine kutamani kuhama CCM na kujiunga na Chadema linatokana na chama hicho cha upinzani kwa sasa kuonekana kuwa na mvuto.

Aliongeza kuwa ni vigumu kwa baadhi ya wanachama wa CCM kukubali ukweli huo kwamba Chadema kina mvuto, lakini alisema watu wenye akili ndani ya CCM wanaijua dhana hiyo.

“Watu wenye akili ndani ya CCM wanajua Chadema kina mvuto na hili wimbi la vijana na watu wengine kukihama CCM siyo dalili nzuri hususani utakapofika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015,” alisema.

Alisema Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ulidhihirisha kwamba Chadema kilipata mvuto mkubwa kwa wananchi baada ya kuibuka na ushindi katika majimbo mbalimbali na kuongeza idadi ya wabunge wake.

“Mwaka 1995 hadi mwaka 2000 wanachama wa upinzani walikuwa wanahama katika vyama vyao na kujiunga na CCM, lakini hivi sasa upepo umebadilika ambapo sasa wanahama kutoka CCM na kwenda Chadema, hii ni dalili kwamba wanakiona kama chama mbadala,” alisema.


Source:Nipashe
 
Hayo ni maoni yake. Ukweli CCM imeenea nchi nzima; pwani hadi bara, mashariki - magharibi, kaskazini - kusini
 
Huyu Bwana nafikiri anasoma alama za nyakati kwani kwenye utafiti wao wa 2010 alivikandia sana vyama vya upinzani na sasa ameona dola inakaribia kuchukuliwa na upinzani sasa naye amehamia huko ili asije kosa ugali wake.
 
Siku za CCM zinahesabika, ushahidi ni uozo ktk matumizi ya serikali na kushindwa kuchukua hatua. Fisadi hawezi kumchukulia fisadi mwenzake hatua. Heko CDM watanzania wengi wapo nyuma yako: Tumaini jipya.
 
Hayo ni maoni yake. Ukweli CCM imeenea nchi nzima; pwani hadi bara, mashariki - magharibi, kaskazini - kusini


"Watu wenye akili ndani ya CCM wanajua Chadema kina mvuto na hili wimbi la vijana na watu wengine kukihama CCM siyo dalili nzuri hususani utakapofika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015," alisema.
 
Naona mpaka Dr.Bana naye amechanganyikiwa na M4C. Kunakipindi alikuwa anatoa tathimini za ajabuajabau huku akiibeba CCM. Sasa ameshindwa kuipaka mafuta mafuta CCM kwa mgongo wa chupa. Wamegundua hata wasiposema wao, mawe yataelezea ilivyo.
 
Hakuna siri CCM sasa ni chama mfu kama hata wanazi wa chama kama Dr Bana wameanza kukubaliana na hali halisi basi wakati umesha fika
 
Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, amesema wimbi la vijana wa CCM kukikimbia na kujiunga na Chadema ni dalili mbaya na kukitaka chama hicho kuwavua magamba wanachama wao wanaowatuhumu kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya ufisadi badala ya kusubiri wajivue wenyewe.

Dk. Bana, alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam pembeni mwa mkutano wa mtengamano wa kisiasa wa Afrika Mashariki.

Alisema kuna watu wengi wanaotaka kukihama CCM na kujiunga na Chadema hivi sasa, lakini wanashindwa kufanya hivyo kutokana na ugumu wa mioyo yao kisiasa.

“CCM isisubiri wanachama wao wenyewe kujivua gamba na kisha vigogo kuanza kusema kwamba watu wa aina hiyo walikuwa hawawahitaji badala yake chama kiwavue kabla,” alisema Dk. Bana.

Alifafanua kuwa wimbi hilo la vijana pamoja na watu wengine kutamani kuhama CCM na kujiunga na Chadema linatokana na chama hicho cha upinzani kwa sasa kuonekana kuwa na mvuto.

Aliongeza kuwa ni vigumu kwa baadhi ya wanachama wa CCM kukubali ukweli huo kwamba Chadema kina mvuto, lakini alisema watu wenye akili ndani ya CCM wanaijua dhana hiyo.

“Watu wenye akili ndani ya CCM wanajua Chadema kina mvuto na hili wimbi la vijana na watu wengine kukihama CCM siyo dalili nzuri hususani utakapofika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015,” alisema.

Alisema Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ulidhihirisha kwamba Chadema kilipata mvuto mkubwa kwa wananchi baada ya kuibuka na ushindi katika majimbo mbalimbali na kuongeza idadi ya wabunge wake.

“Mwaka 1995 hadi mwaka 2000 wanachama wa upinzani walikuwa wanahama katika vyama vyao na kujiunga na CCM, lakini hivi sasa upepo umebadilika ambapo sasa wanahama kutoka CCM na kwenda Chadema, hii ni dalili kwamba wanakiona kama chama mbadala,” alisema.


Source:Nipashe

Hawezi kuwa bana huyo.
Naona kadri muda unavyokwenda mbele,M4C inagusa kila mtu na inazalisha hofu miyoni mwao.Kila mtu anaanza kujikomba CDM.
Kesho kutwa Paramagama nae lazima atatoa ushuhuda wake.
 
Hayo ni maoni yake. Ukweli CCM imeenea nchi nzima; pwani hadi bara, mashariki - magharibi, kaskazini - kusini

Mbona vyama vingi vilivyopigania UHURU i.e KANU and like,mbona vyote vilienea enzi hizo!!Wananchi walijitolea mpaka ng'ombe,pesa,rasilimali watu lakini haohao walikitoa madarakani.
 
Back
Top Bottom