mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,767
- 7,115
Wana JF
Umuofia kwenyu,
Tanzania siku za nyuma ilikuwa na ukame wa kutisha, mifugo ilikufa sana hata wanyama wa porini nao walikufa. Tuliimizana sana kupanda miti kuondoa majangwa, watu waliitikia, sasa mvua inanyesha kila mkoa ni jambo la neema na kumshukru Mungu.
Nchi yetu imegubikwa na rushwa, hatuna wazalendo kabisaa, mvua zinazoendelea zinatuonyesha miundombinu mibovu ambayo wasimamizi wake aidha walichukua wakandarasi feki au rushwa ilitamalaki wakajenga vitu vinavyokinzana na uhalisia wa mazingira.
Kila siku tunashuhudia barabara zikibomoka. Wamejenga madaraja mabovu, barabara zimepunjwa vifusi zinaelea, mikondo ya maji inazidiwa hii yote ni kwa sababu ya 10% au ma-engineer feki.
Juzi tuliona Rais wetu akitaka kumtumua waziri, mwaka juzi tuliona Makonda akiwasimamisha makandarasi lakini baadae waliachiwa waendelee sijui naye alipata hiki kijiti au mule amekuta ni kampuni za wakubwa wake.
Sasa hivi barabara za mitaani zimefumuka vibaya lakini za Tanroad zina uhafadhali sijui TARURA ndio kuna mulungula zaidi mpaka wanapata kandarasi hovyo.
Umuofia kwenyu,
Tanzania siku za nyuma ilikuwa na ukame wa kutisha, mifugo ilikufa sana hata wanyama wa porini nao walikufa. Tuliimizana sana kupanda miti kuondoa majangwa, watu waliitikia, sasa mvua inanyesha kila mkoa ni jambo la neema na kumshukru Mungu.
Nchi yetu imegubikwa na rushwa, hatuna wazalendo kabisaa, mvua zinazoendelea zinatuonyesha miundombinu mibovu ambayo wasimamizi wake aidha walichukua wakandarasi feki au rushwa ilitamalaki wakajenga vitu vinavyokinzana na uhalisia wa mazingira.
Kila siku tunashuhudia barabara zikibomoka. Wamejenga madaraja mabovu, barabara zimepunjwa vifusi zinaelea, mikondo ya maji inazidiwa hii yote ni kwa sababu ya 10% au ma-engineer feki.
Juzi tuliona Rais wetu akitaka kumtumua waziri, mwaka juzi tuliona Makonda akiwasimamisha makandarasi lakini baadae waliachiwa waendelee sijui naye alipata hiki kijiti au mule amekuta ni kampuni za wakubwa wake.
Sasa hivi barabara za mitaani zimefumuka vibaya lakini za Tanroad zina uhafadhali sijui TARURA ndio kuna mulungula zaidi mpaka wanapata kandarasi hovyo.