Mvua zimerejea kwa kasi, ngoja tuone watakuja na kisingizio gani tena

Makombora ya kuzalisha mvua za kujaza mabwawa ya Umeme toka Vietinum sijui mchakato wa ununuzi wa Makombora hayo uliishia wapi?
Chini ya ccm hakuna kitu kinawezekana kwa manufaa ya watanzania
 
Dikiteta hakuruhusu ukarabati alilazimisha machine ziwe oni mwanzo mwisho mpaka ikachakaa,sasa tutatengeneza
 
Waliosema upinzani uko rohoni mwa wananchi walipatia vibaya sana.

Mkuu umechukua vizuri sana nafasi iliyoachwa wazi na CHADEMA kuihoji na kuikosoa serikali ya chama tawala. Congratulations. Kazi iendelee kwa kweli 😅.
 
Leo ukanda wote wa Pwani mvua kubwa sana inanyesha, pia kanda ya ziwa kwa muda wa wiki nzima mvua imenyesha sana.
Sasa ngoja tuone Tanesco na Dawasa watakuja na visingizio gani tena.

Maana Tanesco walifikia kusema mvua imegoma kunyesha mwaka huu sababu ya hayati Magufuli alikata miti millioni 4 kwenye pori la Selous!!
Hoja zao mfilisi. Tuwe tunachunuza uwiano wa hoja zao na historia zao. Wengine malinda mh
 
Utoto mwingine raha sana. Eti mvua zinanyesha ukanda wa Pwani na kanda ya Ziwa. Sijui hayo maji ya mvua za kanda ya ziwa na pwani yataimgia katika mito yetu ya Ruaha na Pangani kuliko na mabwawaya kuzalisha umeme.
Hujui kwamba pangani ipo pwani?
 
Hujui kwamba pangani ipo pwani?
Maji ya Mto Pangani yanatoka Arusha na Kilimanjaro. Yanaingia Bwawa la Nyumba ya Mungu. Then yanaingia Mto Pangani. Mto hauanzii mlangoni mwa Bahari. Huku Moshi na Arusha bado hatuna mvua. Ili Mto Pangani ujae maji mvua zinatakiwa kunyesha huku nyanda za juu Kaskazini Mashariki.
 
Maji ya Mto Pangani yanatoka Arusha na Kilimanjaro. Yanaingia Bwawa la Nyumba ya Mungu. Then yanaingia Mto Pangani. Mto hauanzii mlangoni mwa Bahari. Huku Moshi na Arusha bado hatuna mvua. Ili Mto Pangani ujae maji mvua zinatakiwa kunyesha huku nyanda za juu Kaskazini Mashariki.
Mkuu asante kwa jiografia
 

Similar Discussions

21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom