"Mvua ya madawati" yaanza kunyesha manispaa ya Kinondoni

Bukanga

JF-Expert Member
Dec 13, 2010
2,857
1,934
Kuanzia leo tarehe 04 july 2016,tumeanza kupokea madawati kutoka kwa wazabuni 11,waliopata kazi ya kutengeneza madawati,na kutakiwa kumaliza ndani ya kipindi cha wiki tatu.

Hivyo manispaa ya kinondoni inarajia kupokea madawati kumi na sita elfu ( 16,000) huku muda waliopewa kutumia kwa utengenezaji ukiwa umekaribia kuisha.

Magari mbalimbali tangia asubuhi ya leo yamekuwa yakipishana ofisi za halmashauri kukabidhi mzigo wa madawati ya shule za msingi na sekondari.
dawa.jpg

dawa2.jpg

Source; Lord Mayor Boniface Jacob

CC Mkaruka okonkwo jr
 
Hongereni kwa hatua hiyo, na niwahase mtumie juhudi hiyo hiyo ama zaidi katika utatuzi wa kero zinazowakabili wananchi wa kinondoni
 
Tafsiri yake zaidi ya miaka 50 toka nchi yetu ilipopata huru wanafunzi wengi kama siyo wote kwa sehemu zingine walikuwa wakikaa chini au kukalia majabali na LEO KARNE YA 21 NDIYO MAFANIKIO YA MADAWATI TENA KWA WANANCHI WENYEWE KUJICHANGA NA SIYO SERIKALI.
Eee Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema na Fadhila zako tunakuomba utoe adhabu yako stahiki kwa wale wote waliotufikisha hapa na katika hali hii ya kufedhehesha ilikhali ulitujalia nchi yenye kujaa maziwa na asali tele na kila aina ya Rasilimali.
 
Hivi hapo Makonda hajapitusha bakuli la kuomba hela za ulaji kama kawaida yao?? Maana yeye anafukuza ombaomba mjini halafu yeye anatokea channel ten anaomba asaidiwe. Jamani kuto kujitambua kuna shida sana.
Hakuna kuomba kidogo kuomba ni kuomba tuuu!! Style ndizo hutofautiana.
 
Hivi hapo Makonda hajapitusha bakuli la kuomba hela za ulaji kama kawaida yao?? Maana yeye anafukuza ombaomba mjini halafu yeye anatokea channel ten anaomba asaidiwe. Jamani kuto kujitambua kuna shida sana.
Hakuna kuomba kidogo kuomba ni kuomba tuuu!! Style ndizo hutofautiana.
Huyo hana bajeti yoyote ndio maana anashinda mitaani akiombaomba yet anasema Meya atafute kazi ya kufanya...

Bure kabisa...
 
Hili wala si jambo la kusifia...
Hawa wanaotengenezewa ndio hao hao watakaokuja kuitwa vilaza!..
Wengine baadae watakuja kuwa waalimu lakini watabezwa na kudharauliwa
Watakuja kusomea fani mbalimbali lakini wataonekana hawana uwezo na mchango katika taifa!!
Miaka zaidi ya 50 ya uhuru isingefaa wakati huu uwe ndio wa kushangilia kupata madawati angali hiyo miti na rasilimali nyingine zilikwepo miaka mingi iliyopita..
Bado tuna safari ndefu ya kulikomboa taifa hili la Tanzania kielimu...
 
Regional
Commissio-
ners
Act No.15
of 1984
Art.9
61.
-(1) There shall be a Regional Commissioner for each region
within
the United Republic who, subject to subarticle (3), shall be a leader
in the
Government of the United Republic.
(2) Regional Commissioners in Mainland Tanzania shall be appointe
d by
the President, after consultation with the Prime Minister.
(3) Regional Commissioners in Tanzania Zanzibar shall be appointe
d by
the President of Zanzibar, after consultation with the President.
(4) Without prejudice to the provisions of subarticle (5), every Reg
ional
Commissioner shall have the duty to supervise the discharge of all
the duties and
functions of the Government of the United Republic in the region assigne
d to him
and for that purpose, he shall discharge all duties and functions specif
ied by or
under any written law as being functions of a Regional Commissioner
, and shall
exercise all such powers specified by any law enacted by Parliament.
(5) In addition to his duties and functions specified in the precedin
g
provisions of this Article, a Regional Commissioner for any regi
on in Tanzania
Zanzibar shall discharge the duties and functions of the Revolutionar
y
Government of Zanzibar which shall be assigned to him by the Pre
sident of
Zanzibar and in accordance with the Constitution of Zanzibar, 1984, or any
law
enacted by the House of Representatives.
CHAPTER THREE
THE LEGISLATURE OF THE UNTIED REPU
 
Kwa hiyo miaka 50 bila madawati itufanye tusitengeneze madawati? Mnaobeza mna mawazo gani mbadala?
 
hivi BAVICHA walishawahi kufikiria hili swala la madawati TANZANIA limetoa ajira ngapi kupitia wazabuni waliopata kazi karibia wilaya zote Tanzania,au wao wanasubiria kuongelea mabaya tuu,mazuri hawayaoni??
 
Wilaya ya Kinondoni...ule mpango wa Mulongo wa Magufuli wa kuwasafirisha walimu bure uliishia wapi eti???
 
Tamko la Rais Magufuli katika ubora wake.

Tukiamua tunaweza kama kuna political will!
Indeed- Miracle hizo zinaendelea. Hongerah sana Mh. Magufuli ' tuwainue watoto kutoka chini wakae kwenye madawati' Magufuli ( PhD- 2015)
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom