jamadari
JF-Expert Member
- Feb 13, 2010
- 295
- 92
Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya
Serikali imesema haina uwezo wa kumaliza tatizo la mgawo wa maji uliolikumba jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani na badala yake inasubiri mvua zinyeshe
Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani imekumbwa na mgawo wa maji tangu juzi kutokana na kuharibika kwa mtambo wa kusukuma maji wa Ruvu chini na kupungua kwa kina cha maji.
Kauli hiyo ya serikali ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya, alipozungumza na NIPASHE baada ya kutembelea ofisi za Dawasco, jijini Dar es Salaam.
Profesa Mwandosya alisema wanatarajia mvua zikinyesha ndizo zitakazotatua tatizo la kuwepo mgawo wa maji kwa kuwa kina cha maji Ruvu chini kimepungua kutokana na ukame.
Aliongeza kuwa mgawo uliotangazwa na Dawasco juzi unaweza kuendelea kuwepo kwa kuwa hakuna vyanzo vingine vya maji vya akiba ambavyo wanaweza kuvitumia kama njia mbadala ya kutatua tatizo la maji.
Kuhusu utendaji wa watumishi wa Dawasco, Profesa Mwandosya aliwaasa kufanya kazi na kujiepusha na vitendo vya kuomba rushwa kutoka kwa wateja ili wawape huduma.
Alikiri kuwa kuna baadhi ya watendaji wachache wanaotumia vibaya jukumu walilopewa la kuwapatia maji Watanzania na kuamua kujikita katika vitendo vya rushwa.
Aidha, aliwataka watumishi kuwa wepesi wa kukagua maeneo yote ilipopita miundombinu ya maji kubaini mabomba yaliyopasuka ili waweze kuyaziba haraka.
Aliwaambia kuwa maji mengi ya Dawasco yanapotea njiani kabla ya kumfikia mteja hatua ambayo alisema inazua mgogoro mkubwa kati ya wateja na shirika hilo.
Aliwaka watumishi hao kuacha tabia ya kuwapa Ankara za malipo wateja kila mwezi huku hawawapatii maji kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kuwaibia.
CHANZO: NIPASHE
Watanzania Ngojeni Mvua anayoteremsha Mwenyeezi Mungu inyeshe ndio huo mgao wa Maji utakwisha kazi kweli Waziri huyo anasema hivyo ? Kazi kweli Nchi yetu hiyooo imekufaaaaaaaaaaa